士師記 6 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

士師記 6:1-40

士師基甸

1後來,以色列人又做耶和華視為惡的事,耶和華就把他們交在米甸人手中,受他們統治七年。 2米甸人勢力強盛,以色列人只好躲進山裡,藏在洞穴和營寨中。 3每當他們撒種的時候,米甸人、亞瑪力人及東方人就前來進犯, 4在他們境內安營,摧毀他們遠至迦薩一帶的莊稼,不給他們留下任何糧食,也不留下一隻羊、一頭牛或驢。 5入侵者帶著牲畜和帳篷像蝗蟲一樣湧來,人和駱駝不計其數,摧毀了整個地區。 6以色列人因米甸人的入侵而極其貧乏,就呼求耶和華。

7以色列人因米甸人的入侵而呼求耶和華的時候, 8耶和華就差遣先知對他們說:「以色列的上帝耶和華說,『我曾把你們從受奴役之地——埃及領出來, 9將你們從埃及人及一切欺壓者的手中拯救出來,為你們趕走敵人,把他們的土地賜給你們。』 10我曾對你們說,『我是你們的上帝耶和華。你們雖然住在亞摩利人的地方,但不可祭拜他們的神明。』你們卻充耳不聞。」

11一天,耶和華的天使來到俄弗拉,坐在亞比以謝族人約阿施的橡樹下。約阿施的兒子基甸因為要躲避米甸人,正躲在榨酒池裡打麥子。 12耶和華的天使向基甸顯現,說:「英勇的戰士啊,耶和華與你同在。」 13基甸說:「我主啊,如果耶和華與我們同在,我們怎會有這些遭遇?我們的祖先曾告訴我們有關耶和華帶領他們離開埃及的事,如今祂那些奇妙的作為在哪裡呢?現在祂已經丟棄我們,把我們交在米甸人手裡。」 14耶和華轉向他,說:「你盡自己的力量去從米甸人手中拯救以色列人吧,我現在派你去。」 15基甸說:「主啊,我出身於瑪拿西支派最貧窮的家族,在家裡最微不足道,我怎能拯救以色列人呢?」 16耶和華說:「我必與你同在,你必如擊打一人一樣擊打米甸人。」 17基甸說:「如果我在你面前蒙恩,求你給我一個憑據,使我知道與我說話的真是你耶和華。 18請你在這裡等一等,讓我回去拿禮物獻給你。」耶和華說:「我必等你回來。」

19基甸回家預備了一隻山羊羔,用十公斤麵粉做了無酵餅,把肉放進籃子,把湯盛在壺中,然後拿到橡樹下獻給耶和華的天使。 20上帝的天使對基甸說:「把肉和無酵餅放在這磐石上,把湯倒在上面。」他一一照做。 21耶和華的天使伸出手中的杖碰了一下餅和肉,火就從磐石中噴出來燒盡了它們。耶和華的天使也不見了。 22基甸發現他果然是耶和華的天使,便說:「唉!主耶和華啊,不好了,我面對面見了你的天使。」 23耶和華對他說:「放心吧,不用害怕,你不會死。」 24基甸在那裡為耶和華築了一座壇,稱之為「耶和華賜平安」。這壇如今仍在亞比以謝族的俄弗拉

25那天晚上,耶和華吩咐基甸:「牽來你父親的第二頭牛,就是那頭七歲的牛,拆毀你父親為巴力築的祭壇,砍倒壇旁的亞舍拉神像。 26然後,在這座山頂上把石頭堆放整齊,為你的上帝耶和華築一座祭壇,用砍倒的亞舍拉神像作柴,把那頭牛獻作燔祭。」 27於是,基甸帶了十個僕人遵命而行。不過,他因為害怕家人和城中的人,不敢在白天行動,便在夜間行動。

28第二天清早,城裡的人發現巴力的祭壇已經被人拆毀,壇旁的亞舍拉神像被砍倒,第二頭公牛被獻在新建的祭壇上。 29他們彼此議論說:「這是誰幹的?」他們仔細調查後得知是約阿施的兒子基甸所為, 30便對約阿施說:「把你兒子交出來!他拆毀了巴力的祭壇,砍倒了壇旁的亞舍拉神像,我們要處死他!」 31約阿施對氣勢洶洶的人群說:「你們這樣做是要為巴力辯護嗎?是要救它嗎?誰為巴力辯護,今天早晨就處死誰。有人拆毀巴力的祭壇,如果它是神明,就讓它為自己辯護吧!」 32因此,那天他們稱基甸耶路·巴力,意思是「讓巴力為自己辯護」,因為他拆毀了巴力的祭壇。

33那時,米甸人、亞瑪力人及東方人一起過了約旦河,在耶斯列的平原安營。 34耶和華的靈降在基甸身上,他就吹起號角,號召亞比以謝族的人跟從他。 35他派人走遍瑪拿西亞設西布倫拿弗他利各支派召集軍隊,得到了人們的回應。 36基甸對上帝說:「若如你所言,你要用我去拯救以色列人, 37求你給個憑據。我把一團羊毛放在麥場上,若明天早晨只是羊毛上有露水,地面卻是乾的,我就知道,如你所言,你要用我去拯救以色列人。」 38果然如此,基甸一早醒來,從羊毛中擠出滿滿一碗露水。 39基甸又對上帝說:「求你不要發怒,容許我再試一次,這次讓羊毛是乾的,地面有露水。」 40那天晚上,耶和華就照他所求使地面佈滿露水,唯獨羊毛是乾的。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waamuzi 6:1-40

Gideoni

16:1 Amu 2:11; Mwa 25:2; Hes 25:15-18Waisraeli wakafanya tena yaliyo maovu mbele za Bwana, naye kwa miaka saba Bwana akawatia mikononi mwa Wamidiani. 26:2 1Sam 13:6; Isa 5:30; 8:21; 26:16; 27:3; 2:19; Yer 48:28; 49:8; Ay 24:8; Yer 41:9; Ebr 11:38Mkono wa Midiani ukawa na nguvu dhidi ya Israeli na kwa ajili ya Wamidiani, Waisraeli wakajitengenezea mahali pa kujificha milimani, kwenye mapango na ngome. 36:3 Hes 13:29; Mwa 25:6; Isa 11:14; Yer 49:28Kila wakati Waisraeli walipopanda mazao mashambani, Wamidiani, Waamaleki na mataifa mengine ya mashariki walivamia nchi yao. 46:4 Law 26:16; Kum 28:30, 51; Isa 10:6; 42:22; Mwa 10:19Wakapiga kambi katika mashamba yao na kuharibu mazao ya nchi yote hadi kufikia Gaza, wala hawakuacha kiumbe chochote kilicho hai kwa Waisraeli, iwe kondoo au ngʼombe au punda. 56:5 Kum 28:42; Amu 8:10; Isa 21:7; 60:6; Yer 49:28Walipanda na mifugo yao na mahema yao, mfano wa makundi ya nzige. Ilikuwa haiwezekani kuwahesabu watu na ngamia zao; wakavamia nchi ili kuiharibu. 6Waisraeli wakafanywa kuwa maskini sana na Wamidiani, hata Israeli wakamlilia Bwana kuomba msaada.

76:7 Amu 3:9Waisraeli walipomlilia Bwana kwa sababu ya Wamidiani, 86:8 Kum 18:15; 1Fal 20:13, 22; 2Fal 17:13, 23; Neh 9:29; Yer 25:5; Ay 36:10; Eze 18:30-31; Amu 2; 1Bwana akawapelekea nabii, ambaye aliwaambia, “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: Niliwapandisha mtoke Misri, toka nchi ya utumwa. 96:9 Neh 10:9; Za 136:24; 44:2Nikawanyakua kutoka mikononi mwa Wamisri na kutoka mikononi mwa watesi wenu wote. Nikawafukuza watoke mbele yenu nami nikawapa ninyi nchi yao. 106:10 Kut 20:5; Yos 24:15; Yer 10:2Nikawaambia, ‘Mimi ndimi Bwana Mungu wenu; msiiabudu miungu ya Waamori, ambayo mnakaa katika nchi yao!’ Lakini ninyi hamkuitii sauti yangu.”

116:11 Mwa 16:7; Yos 18:23; Amu 7:14; 8:13, 29; Hes 26:30; Amu 7:1; 8; 1; Ebr 11:32; Rut 2:17; 3:2; 1Sam 23:1; Neh 13:15; Isa 16:10; 63:3; Mao 1:15; Yoe 3:13Malaika wa Bwana akaja akaketi chini ya mti wa mwaloni huko Ofra, ambao ulikuwa mali ya Yoashi, Mwabiezeri, ambako Gideoni mwanawe alikuwa akipepeta ngano penye shinikizo la kukamulia zabibu, ili kuificha Wamidiani wasiione. 126:12 Yos 1:5; Rut 2:4; 1Sam 10:7; Za 129:8; Amu 11:1; Lk 1:11, 28Malaika wa Bwana alipomtokea Gideoni, akamwambia, “Bwana yu pamoja nawe, Ewe shujaa mwenye nguvu.”

136:13 Yos 3:5; 2Sam 7:22; Za 44; 1; 78:3; Kum 31:17; 2Nya 15; 2Gideoni akajibu, “Ee Bwana wangu, kama Bwana yu pamoja nasi, mbona mambo haya yote yametutokea? Yako wapi basi yale matendo yake makuu baba zetu waliyotusimulia juu yake waliposema, ‘Je, Bwana hakutupandisha kutoka Misri?’ Lakini sasa Bwana ametuacha na kututia katika mkono wa Midiani.”

146:14 Ebr 11:34; Amu 10:1; 1Fal 14:27Bwana akamgeukia na kusema “Enenda kwa uwezo wako huu, ukawaokoe Israeli kutoka mikononi mwa Wamidiani. Je, si mimi ninayekutuma wewe?”

156:15 Isa 60:22; 1Sam 9:20-21Gideoni akauliza, “Ee Bwana wangu, nitawezaje kuwaokoa Israeli? Ukoo wangu ndio dhaifu kuliko zote katika Manase, nami ndiye mdogo wa wote katika jamaa yangu.”

166:16 Kut 3:12; Hes 14:43; Yos 1:5Bwana akamjibu, “Nitakuwa pamoja nawe, nawe utawapiga Wamidiani kana kwamba walikuwa ni mtu mmoja.”

176:17 Mwa 24:14; Kut 3; 12; 4:8Gideoni akajibu, “Kama basi nimepata kibali machoni pako, nipe ishara kuonyesha kweli kwamba ni wewe unayesema nami. 18Tafadhali ninakuomba usiondoke hapa mpaka nitakaporudi na kukuletea sadaka yangu na kuiweka mbele yako.”

Naye Bwana akamwambia, “Nitangoja mpaka utakaporudi.”

196:19 Mwa 18:7-8; Law 19:36; Amu 13:15Gideoni akaingia ndani ya nyumba yake na kuandaa mwana-mbuzi pamoja na kuoka mikate isiyotiwa chachu kutokana na efa moja6:19 Efa moja ni sawa na lita 22. ya unga. Akaweka nyama kwenye kikapu na mchuzi kwenye chungu, akamletea huyo malaika hapo nje chini ya mti wa mwaloni na kumpa.

206:20 Amu 13:19Malaika wa Mungu akamwambia, “Itwae nyama na mikate isiyotiwa chachu, uviweke juu ya mwamba huu na umimine huo mchuzi juu yake.” Gideoni akafanya hivyo. 216:21 Kut 4:2; Law 9:24Malaika wa Bwana akainyoosha fimbo iliyokuwa mkononi mwake, ncha yake ikagusa ile nyama na ile mikate isiyotiwa chachu, nao moto ukatoka kwenye mwamba ukateketeza ile nyama na ile mikate. Malaika wa Bwana akatoweka kutoka machoni pake. 226:22 Kum 13:16; Mwa 32:30; 11:32Gideoni alipotambua kuwa ni malaika wa Bwana, akapiga kelele kwa mshangao, akasema, “Ole wangu, Bwana Mwenyezi! Kwa kuwa nimemwona malaika wa Bwana uso kwa uso!”

236:23 Dan 10:19; Mwa 16:13; Kum 5:26Lakini Bwana akamwambia, “Amani iwe kwako! Usiogope. Hutakufa.”

246:24 Mwa 22:14; Yos 18:23Hivyo Gideoni akamjengea Bwana madhabahu mahali pale na kupaita, Yehova-Shalom.6:24 Yehova-Shalom maana yake Bwana ni Amani. Mpaka leo ingalipo imesimama huko Ofra ya Waabiezeri.

256:25 Kut 34:13; Amu 2:13; Kum 2:13; 7:5Usiku ule ule Bwana akamwambia, “Mchukue ngʼombe dume wa baba yako, yaani, yule wa pili mwenye miaka saba, na ubomoe madhabahu ya Baali aliyo nayo baba yako, na ukaikate Ashera iliyo karibu nayo. 266:26 Mwa 8:20Kisha mjengee Bwana Mungu wako, madhabahu halisi, kwa taratibu zake, juu ya huu mwamba. Kwa kutumia kuni za hiyo nguzo ya Ashera uliyoikatakata, mtoe sadaka huyo dume wa pili kuwa sadaka ya kuteketezwa.”

27Basi Gideoni akawachukua watumishi wake kumi na kufanya kama Bwana alivyomwambia. Lakini kwa kuwa aliwaogopa jamaa yake na watu wa mji, akafanya haya usiku badala ya mchana.

286:28 1Fal 16:32; 2Fal 21:3Watu wa mji walipoamka asubuhi, tazama madhabahu ya Baali imebomolewa na nguzo ya Ashera iliyokuwa karibu nayo imekatwakatwa na yule ngʼombe wa pili ametolewa sadaka juu ya madhabahu yaliyojengwa upya!

29Wakaulizana, “Ni nani aliyetenda mambo haya?”

Walipochunguza kwa makini, wakaambiwa, “Ni Gideoni mwana wa Yoashi, ndiye alitenda hivi.”

30Watu wa mji wakamwambia Yoashi, “Mlete mwanao hapa. Ni lazima afe, kwa sababu amebomoa madhabahu ya Baali na kukatakata nguzo ya Ashera iliyokuwa karibu nayo.”

316:31 1Sam 24:15; Za 43:1; Yer 30:13Lakini Yoashi akauambia ule umati uliokuwa umezunguka ukiwa kinyume naye, “Je, ninyi mtamtetea Baali? Mnajaribu kumwokoa? Yeyote mwenye kumpigania atauawa kufikia kesho asubuhi! Kama Baali ni mungu kweli, anaweza kujitetea mwenyewe wakati mtu anapobomoa madhabahu yake.” 326:32 Amu 7:1; 8:29, 35; 9:1; 1Sam 12:11Basi siku ile wakamwita Gideoni “Yerub-Baali,” yaani, “Baali na ashindane naye,” kwa sababu alibomoa madhabahu yake.

336:33 Hes 13:29; Mwa 25:6; Yos 15:56; Eze 25:4; Hos 1:5Basi Wamidiani wote, Waamaleki na mataifa mengine ya mashariki wakaunganisha majeshi yao, wakavuka ngʼambo ya Yordani na kupiga kambi katika Bonde la Yezreeli. 346:34 Amu 3:10; Yos 6:20; Amu 3:27; Yos 17:2Ndipo Roho wa Bwana akamjia Gideoni, akapiga tarumbeta, akiwaita Waabiezeri ili wamfuate. 356:35 Yos 17:7; Amu 4:6; 7:23Akatuma wajumbe waende katika Manase yote, akiwataka wachukue silaha na pia katika Asheri, Zabuloni na Naftali, nao wakakwea ili kukutana nao.

36Gideoni akamwambia Mungu, “Kama utawaokoa Waisraeli kwa mkono wangu, kama ulivyoahidi: 376:37 Ay 31:20; Hes 18; 27; 2Sam 6:6; 24:16; Mwa 24; 14tazama, nitaweka ngozi ya kondoo kwenye kiwanja cha kupuria nafaka, na kama utakuwepo umande juu ya ngozi tu, nayo ardhi yote ikiwa kavu, ndipo nitakapojua kuwa utaokoa Israeli kwa mkono wangu, kama ulivyosema.” 38Hivyo ndivyo ilivyotokea. Gideoni akaamka asubuhi na mapema kesho yake, akaikamua ile ngozi, umande ukatoka, maji ya kujaa bakuli.

396:39 Mwa 18:32Kisha Gideoni akamwambia Bwana, “Usinikasirikie. Ninaomba nifanye ombi moja lingine. Niruhusu nifanye jaribio jingine moja kwa ngozi hii. Wakati huu uifanye ngozi hii kavu na ardhi yote ifunikwe na umande.” 406:40 Kut 4:3-7; Isa 28:7Usiku ule Mungu akafanya hivyo. Ngozi ile ilikuwa kavu, nayo ardhi yote ikafunikwa na umande.