啟示錄 16 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

啟示錄 16:1-21

1我聽見殿中有宏亮的聲音對七位天使說:「去將那盛滿上帝烈怒的七個碗傾倒在地上。」

2第一位天使離去,將碗倒在了地上,那些有怪獸的印記、敬拜獸像的人身上長出奇痛無比的毒瘡。

3第二位天使將碗倒在了海洋裡,海水變得像死人的血,海中的活物都死光了。

4第三位天使將碗倒在了江河與水泉裡,水就變成了血。 5我聽見掌管各水源的天使說:

「昔在今在的聖者啊!

你是公義的,

因為你施行了審判。

6由於他們流了眾聖徒和先知們的血,

現在你使他們喝血,

這正是他們應得的報應。」

7我又聽見從祭壇發出的聲音說:

「是的,全能的主上帝,

你的判決真實公義。」

8第四位天使將碗倒在太陽上,太陽就變得炙熱如火,可以灼傷人。 9人們被炙熱灼傷,就褻瀆掌管這些災禍的上帝的名,他們毫無悔意,不肯歸榮耀給上帝。

10第五位天使將碗倒在那海中怪獸的座位上,牠的國便被黑暗籠罩,牠的國民痛苦難當,咬自己的舌頭。 11他們因為痛苦和毒瘡就褻瀆天上的上帝,不肯為自己的所作所為悔改。

12第六位天使將碗倒在幼發拉底大河上,河水立刻乾了,為東方各國的王預備了道路。 13我又看見三個像青蛙一樣的污鬼分別從巨龍、怪獸和假先知的口裡跳出來。 14其實牠們都是鬼魔的靈,能行奇蹟。牠們到普天下召集各王,預備在全能上帝的大日子來臨時聚集爭戰。

15「看啊!我要像賊一樣出其不意地來到。那警醒等候,看守自己衣裳,不致赤身行走蒙受羞辱的人有福了。」

16鬼魔把眾王召集到一個希伯來話叫哈米吉多頓的地方。

17第七位天使將碗倒在空中時,從殿裡的寶座上傳出響亮的聲音說:「成了!」 18隨後雷電交加,伴隨著巨響,還有空前劇烈的大地震。 19巴比倫大城裂作三段,其他各國的城邑也都倒塌了。上帝並沒有忘記巴比倫大城的罪惡,要把那杯盛滿祂烈怒的酒給她喝。 20海島都沉沒了,山嶺也都不見了, 21又有重達三十四公斤16·21 三十四公斤」希臘文是「一他連得」。的巨型冰雹從天而降,打在世人身上。世人無法忍受這極大的災禍,就褻瀆上帝。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 16:1-21

Mabakuli Saba Ya Ghadhabu Ya Mungu

116:1 Ufu 15:1; 11:19; 15:1; 16:2-21; Za 79:6; Sef 3:8Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mle Hekaluni ikiwaambia wale malaika saba, “Nendeni, mkayamwage duniani hayo mabakuli saba ya ghadhabu ya Mungu.”

216:2 Ufu 8:7; 13:15; 17; Kut 9:9-11Malaika wa kwanza akaenda akalimwaga hilo bakuli lake juu ya nchi. Majipu mabaya yenye maumivu makali yakawapata wale watu wote waliokuwa na chapa ya yule mnyama na walioabudu sanamu yake.

316:3 Kut 7:17-21; Ufu 6:11Malaika wa pili akalimwaga bakuli lake baharini, nayo ikabadilika kuwa damu kama ya mtu aliyekufa na kila kiumbe hai kilichokuwa ndani ya bahari kikafa.

416:4 Ufu 8:10Malaika wa tatu akalimwaga bakuli lake katika mito na chemchemi za maji, nazo zikawa damu. 516:5 Ufu 15:3-4; 15:3; 1:4; 15:4; 6:10Ndipo nikamsikia malaika msimamizi wa maji akisema:

“Wewe una haki katika hukumu hizi ulizotoa,

wewe uliyeko, uliyekuwako, Uliye Mtakatifu,

kwa sababu umehukumu hivyo;

616:6 Isa 49:26kwa kuwa walimwaga damu ya watakatifu wako

na manabii wako,

nawe umewapa damu wanywe

kama walivyostahili.”

716:7 Ufu 9:6; 15:3; 19:2Nikasikia madhabahu ikiitikia,

“Naam, Bwana Mungu Mwenyezi,

hukumu zako ni kweli na haki.”

816:8 Ufu 8:12; 14:18Malaika wa nne akamimina bakuli lake kwenye jua, nalo likapewa nguvu za kuwaunguza watu kwa moto. 916:9 Ufu 2:21; 11:13Watu wakaunguzwa na hilo joto kali, wakalaani Jina la Mungu, aliyekuwa na uwezo juu ya mapigo haya, tena wakakataa kutubu na kumtukuza Mungu.

1016:10 Ufu 13:2; 9:2Malaika wa tano akamimina bakuli lake kwenye kiti cha enzi cha yule mnyama, nao ufalme wake ukagubikwa na giza. Watu wakatafuna ndimi zao kwa ajili ya maumivu, 1116:11 Ufu 11:13; 2:21; 16:9, 21wakamlaani Mungu wa mbinguni kwa sababu ya maumivu na majeraha yao, wala hawakutubu kwa ajili ya matendo yao maovu.

1216:12 Ufu 9:14; Isa 41:2Malaika wa sita akamimina bakuli lake kwenye mto mkubwa Frati, maji yake yakakauka ili kutayarisha njia kwa ajili ya wafalme watokao Mashariki. 1316:13 Ufu 12:3; 13:1; 19:20Kisha nikaona roho wachafu watatu waliofanana na vyura wakitoka katika kinywa cha lile joka na katika kinywa cha yule mnyama na katika kinywa cha yule nabii wa uongo. 1416:14 1Tim 4:1; Ufu 17:14Hizo ndizo roho za pepo wachafu zitendazo miujiza. Nazo huwaendea wafalme wa ulimwengu wote na kuwakusanya tayari kwa ajili ya vita katika siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.

1516:15 Lk 12:3“Tazama, naja kama mwizi! Amebarikiwa yeye akeshaye na kuziweka tayari nguo zake ili asiende uchi na kuonekana aibu yake.”

1616:16 Ufu 9:11; Amu 5:19Ndipo wakawakusanya wafalme pamoja mahali paitwapo Armagedoni16:16 Armagedoni au Har-Magedoni ina maana Mlima Megido, mahali pa kinabii ambapo wafalme wote wa dunia watakusanyika kwa vita katika siku ya Mungu Mwenyezi. kwa Kiebrania.

1716:17 Efe 2:2; Ufu 14:15; 11:15; 21:6Malaika wa saba akamimina bakuli lake angani na sauti kubwa ikatoka mle hekaluni katika kile kiti cha enzi, ikisema, “Imekwisha kuwa!” 1816:18 Ufu 4:5; 6:12; Dan 12:1Kukawa na mianga ya umeme wa radi, ngurumo, radi na tetemeko kubwa la ardhi. Hapajawa kamwe na tetemeko la ardhi kama hilo tangu mwanadamu awepo duniani, hivyo lilikuwa tetemeko kubwa ajabu. 1916:19 Ufu 17:18; 18:5; 14:8Ule mji mkubwa ukagawanyika katika sehemu tatu, nayo miji ya mataifa ikaanguka. Mungu akaukumbuka Babeli Mkuu na kumpa kikombe kilichojaa mvinyo wa ghadhabu ya hasira yake. 2016:20 Ufu 6:14Kila kisiwa kikatoweka wala milima haikuonekana. 2116:21 Eze 13:13; Kut 9:23-25Mvua kubwa ya mawe yenye uzito wa talanta moja16:21 Talanta moja ni kama kilo 34. ikashuka kutoka mbinguni, ikawaangukia wanadamu. Nao wanadamu wakamlaani Mungu kwa ajili ya hayo mapigo ya mvua ya mawe, kwa sababu pigo hilo lilikuwa la kutisha.