創世記 8 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

創世記 8:1-22

洪水消退

1上帝眷顧挪亞及方舟裡的野獸和牲畜,使風吹在大地上,水便開始消退。 2深淵的泉源和天上的水閘都關閉了,大雨也停了。 3地上的洪水慢慢消退,過了一百五十天,水退下去了。 4七月十七日,方舟停在亞拉臘山上。 5水繼續消退,到十月一日,山頂都露出來了。

6又過了四十天,挪亞打開方舟的窗戶, 7放出一隻烏鴉。牠一直在空中飛來飛去,直到地上的水都乾了。 8後來,挪亞放出一隻鴿子,以便瞭解地面的水是否已經消退。 9但遍地都是水,鴿子找不到歇腳的地方,就飛回了方舟,挪亞伸手把鴿子接進方舟裡。 10過了七天,挪亞再把鴿子放出去。 11到了黃昏,鴿子飛回來,嘴裡啣著一片新擰下來的橄欖葉,挪亞便知道地上的水已經退了。 12等了七天,他又放出鴿子,這一次,鴿子沒有回來。

13挪亞六百零一歲那年的一月一日,地上的水乾了。挪亞打開方舟的蓋觀望,看見地面都乾了。 14到了二月二十七日,大地完全乾了。 15上帝對挪亞說: 16「你與妻子、兒子和兒媳可以出方舟了。 17你要把方舟裡的飛禽走獸及爬蟲等所有動物都帶出來,讓牠們在地上多多繁殖。」 18於是,挪亞與妻子、兒子和兒媳都出了方舟。 19方舟裡的飛禽走獸和爬蟲等所有地上的動物,都按種類出了方舟。

挪亞獻祭

20挪亞為耶和華築了一座壇,在上面焚燒各種潔淨的牲畜和飛鳥作為燔祭。 21耶和華聞到這燔祭的馨香,心想:「雖然人從小就心存惡念,但我再不會因為人的緣故而咒詛大地,再不會毀滅一切生靈。 22只要大地尚存,播種收割、夏熱冬寒、白晝黑夜必永不停息。」

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 8:1-22

Mwisho Wa Gharika

18:1 Mwa 9:15; 19:29; 21:1; 30:22; Kut 2:23-24; Ay 12:15; 14:13; Rut 4:13; Nah 1:4; 1Sam 1:11, 19; 2Fal 20:3; 1Nya 16:15; Neh 1:8; 5:19; 13:11-31; Hes 10:9; Za 66:6; 105:42; 106:4; Lk 1:54, 72; Kut 14:21; Yos 2:10; 3:16; Isa 11:15; 44:27Mungu akamkumbuka Noa na wanyama wote wa porini na wa kufugwa waliokuwa naye ndani ya safina, akatuma upepo ukavuma katika dunia, nayo maji yakaondoka. 28:2 Mwa 7:4, 11Zile chemchemi zilizo chini sana ya ardhi pamoja na malango ya mafuriko ya mbinguni yakawa yamefungwa nayo mvua ikawa imekoma kunyesha kutoka angani. 38:3 Mwa 7:24Maji yakaendelea kupungua taratibu katika nchi. Kunako mwisho wa siku ya 150, maji yalikuwa yamepungua, 48:4 Mwa 7:11, 20; 2Fal 19:37; Yer 51:27katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa saba, safina ikatua katika milima ya Ararati. 5Maji yakaendelea kupungua hadi mwezi wa kumi, na siku ya kwanza ya mwezi wa kumi, vilele vya milima vikaonekana.

6Baada ya siku arobaini Noa akafungua dirisha alilokuwa amelifanya katika safina 78:7 Amu 11:15; Kum 14:14; 1Fal 17:4-6; Ay 38:41; Za 147:9; Mit 30:17; Isa 34:11; Lk 12:24na akamtoa kunguru, akawa akiruka kwenda na kurudi mpaka maji yalipokwisha kukauka juu ya nchi. 88:8 Ay 30:31; Za 55:6; 74:19; Wim 2:12-14; Isa 38:14; 59:11; 60:8; Yer 48:28; Eze 7:16; Nah 2:7; Hos 7:11; 11:11; Mt 3:16; 10:16; Yn 1:32Kisha akamtoa hua ili aone kama maji yameondoka juu ya uso wa ardhi. 9Lakini hua hakupata mahali pa kutua kwa kuwa maji yalienea juu ya uso wa dunia yote, kwa hiyo akarudi kwa Noa ndani ya safina. Noa akanyoosha mkono akamchukua yule hua akamrudisha ndani ya safina. 10Noa akangojea siku saba zaidi kisha akamtoa tena hua kutoka safina. 11Wakati hua aliporejea kwa Noa jioni, alikuwa amechukua katika mdomo wake jani bichi la mzeituni, lililochumwa wakati ule ule! Ndipo Noa akajua ya kuwa maji yameondoka juu ya uso wa dunia. 12Akangojea siku saba zaidi na akamtuma tena hua, lakini wakati huu hua hakurudi tena kwa Noa.

138:13 Mwa 5:32Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza ya mwaka 601, wa kuishi kwake Noa, maji yalikuwa yamekauka duniani. Kisha Noa akafungua mlango wa safina akaona ya kuwa uso wa ardhi ulikuwa umekauka. 148:14 Mwa 7:11Katika siku ya ishirini na saba ya mwezi wa pili dunia ilikuwa imekauka kabisa.

15Ndipo Mungu akamwambia Noa, 168:16 Mwa 7:13“Toka ndani ya safina, wewe na mkeo na wanao na wake zao. 178:17 Mwa 1:22Utoe nje kila aina ya kiumbe hai aliye pamoja nawe: Ndege, wanyama na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi, ili wakazae, na kuongezeka na kuijaza tena dunia.”

188:18 1Pet 3:20; 2Pet 2:5Kwa hiyo Noa akatoka nje pamoja na mkewe, wanawe na wake zao. 19Wanyama wote na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi na ndege wote, kila kitu kiendacho juu ya nchi, aina moja baada ya nyingine vikatoka katika safina, kila aina ya kiumbe, kimoja baada ya kingine.

Noa Atoa Dhabihu

208:20 Mwa 12:7-8; 13:18; 22:9; 26:25; 33:20; 35:7; 7:8; 22:2-13; Kut 17:15; 24:4; 10:25; 20:24; 40:29; Ay 42:8; Law 1:3; 4:29; 6:8-13; Hes 6:11; Amu 6:26; 11:31; 1Sam 20:29Kisha Noa akamjengea Bwana madhabahu, akachukua baadhi ya wale wanyama na ndege wote walio safi, akatoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu. 218:21 Kut 29:18, 25; Law 1:9, 13; 2:9; 4:31; Hes 15:3, 7; 2Kor 2:15; Mwa 3:17; 6:5; 9:11-15; Yer 17:9; Za 51:5; Mt 15:19; Rum 1:21; Yer 44:11; Isa 54:9Bwana akasikia harufu nzuri ya kupendeza, naye akasema moyoni mwake, “Kamwe sitailaani tena ardhi kwa sababu ya mwanadamu, hata ingawa kila mwelekeo wa moyo wake ni mbaya tangu ujana. Kamwe sitaangamiza tena viumbe hai vyote kama nilivyofanya.

228:22 Yos 3:15; Za 67:6; 74:17; Yer 5:24; Zek 14:8; Mwa 1:14“Kwa muda dunia idumupo,

wakati wa kupanda na wa kuvuna,

wakati wa baridi na wa joto,

wakati wa kiangazi na wa masika,

usiku na mchana

kamwe havitakoma.”