創世記 46 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

創世記 46:1-34

以色列全家下埃及

1以色列帶著他所有的一切來到別示巴,向他父親以撒的上帝獻祭。 2晚上,上帝在異象中對他說:「雅各雅各!」他說:「我在這裡。」 3上帝說:「我是上帝,是你父親的上帝,不要害怕下到埃及,因為我要使你在那裡成為大族。 4我必跟你一起下到埃及,也必帶領你回來,約瑟必為你送終。」

5於是,雅各別示巴啟程。以色列的兒子們帶著父親和妻兒,乘坐法老送來的車, 6帶著在迦南獲得的牲畜和財物前往埃及。這樣,雅各帶著他所有的子孫, 7就是他的兒子、孫子、女兒和孫女一起去了埃及

8以下是去埃及以色列人,即雅各和他後代的名字。

雅各的長子是呂便9呂便的兒子是哈諾法路希斯倫迦米10西緬的兒子是耶姆利雅憫阿轄雅斤瑣轄迦南女子生的掃羅11利未的兒子是革順哥轄米拉利12猶大的兒子是俄南示拉法勒斯謝拉俄南死在了迦南法勒斯的兒子是希斯倫哈姆勒13以薩迦的兒子是陀拉普瓦約伯伸崙14西布倫的兒子是西烈以倫雅利15這些都是利亞巴旦·亞蘭雅各生的兒孫,加上女兒底娜共有三十三人。

16迦得的兒子是洗非芸哈基書尼以斯本以利亞羅底亞列利17亞設的兒子是音拿亦施瓦亦施韋比利亞和他們的妹妹西拉比利亞的兒子是希別瑪結18這些是悉帕雅各生的兒孫,共有十六人,悉帕拉班給女兒利亞的婢女。

19雅各的妻子拉結生的兒子是約瑟便雅憫20約瑟埃及生的兒子是瑪拿西以法蓮,他們的母親是城祭司波提非拉的女兒亞西納21便雅憫的兒子是比拉比結亞實別基拉乃幔以希羅實姆平戶平亞勒22這些是拉結雅各生的兒孫,共有十四人。

23的兒子是戶伸24拿弗他利的兒子是雅薛沽尼耶色示冷25這些是辟拉雅各生的兒孫,共有七人,辟拉拉班給女兒拉結的婢女。

26雅各一同到埃及去的兒孫共有六十六人,他的兒媳婦除外。 27加上約瑟埃及生的兩個兒子,雅各一家來到埃及的共有七十人。

28雅各猶大先去見約瑟,請他派人引路到歌珊去。他們來到歌珊29約瑟備好車前去迎接父親以色列。父子重逢,約瑟抱住父親哭了很久。 30以色列約瑟說:「我現在看到你還活著,就是死也安心了。」

31約瑟對他的弟兄們和其他家人說:「我要去告訴法老,你們已經從迦南來到我這裡。 32你們是牧人,以畜牧為業,已經把羊群、牛群和所有的一切都帶來了。 33等法老召見你們,問你們以什麼為業, 34你們要說,『僕人們跟我們的祖先一樣,從小以畜牧為業。』這樣,你們就可以住在歌珊,因為埃及人厭惡牧羊的。」

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 46:1-34

Yakobo Aenda Misri

1Hivyo Israeli akaondoka na vyote vilivyokuwa mali yake, naye alipofika Beer-Sheba, akamtolea dhabihu Mungu wa Isaki baba yake.

246:2 Mwa 15:1Mungu akanena na Israeli katika maono usiku na kusema, “Yakobo! Yakobo!”

Akajibu, “Mimi hapa.”

346:3 Mwa 12:2; 28:13Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu wa baba yako, usiogope kushuka Misri, kwa maana huko nitakufanya taifa kubwa. 446:4 Mwa 5:16Nitashuka Misri pamoja nawe, nami hakika nitakurudisha tena Kanaani. Mikono ya Yosefu mwenyewe ndiyo itakayofunga macho yako.”

546:5 Mwa 45:19Ndipo Yakobo akaondoka Beer-Sheba nao wana wa Israeli wakamchukua baba yao Yakobo na watoto wao na wake zao katika magari ya kukokotwa yale Farao aliyokuwa amempelekea kumsafirisha. 646:6 Kum 26:5; Mdo 7:15Wakachukua pia mifugo yao na mali walizokuwa wamezipata Kanaani, Yakobo na uzao wake wote wakashuka Misri. 7Akawachukua wanawe na binti zake, wajukuu wake wa kiume na wa kike, yaani uzao wake wote mpaka Misri.

8Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli (Yakobo na wazao wake), waliokwenda Misri:

Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo.

9Wana wa Reubeni ni:

Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi.

1046:10 Kut 6:15Wana wa Simeoni ni:

Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani.

11Wana wa Lawi ni:

Gershoni, Kohathi na Merari.

1246:12 1Nya 2:5; Mt 1:3Wana wa Yuda ni:

Eri, Onani, Shela, Peresi na Zera (lakini Eri na Onani walifariki katika nchi ya Kanaani).

Wana wa Peresi ni:

Hesroni na Hamuli.

13Wana wa Isakari ni:

Tola, Puva, Yashubu na Shimroni.

1446:14 Mwa 30:20Wana wa Zabuloni ni:

Seredi, Eloni na Yaleeli.

1546:15 Mwa 30:21Hawa ndio wana wa Lea aliomzalia Yakobo huko Padan-Aramu pamoja na binti yake Dina. Jumla ya wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu.

1646:16 Hes 26:15Wana wa Gadi ni:

Sefoni, Hagi, Shuni, Esboni, Eri, Arodi na Areli.

1746:17 Mwa 30:13Wana wa Asheri ni:

Imna, Ishva, Ishvi na Beria.

Dada yao alikuwa Sera.

Wana wa Beria ni:

Heberi na Malkieli.

18Hawa ndio watoto Zilpa aliomzalia Yakobo, ambao Labani alimpa binti yake Lea; jumla yao walikuwa kumi na sita.

19Wana wa Raheli mke wa Yakobo ni:

Yosefu na Benyamini. 2046:20 Mwa 41:51Huko Misri, Asenathi binti wa Potifera, aliyekuwa kuhani wa mji wa Oni,46:20 Yaani Heliopoli (Mji wa Jua). alimzalia Yosefu wana wawili, Manase na Efraimu.

2146:21 1Nya 7:6-12Wana wa Benyamini ni:

Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu na Ardi.

22Hawa ndio wana wa Raheli aliomzalia Yakobo; jumla yao ni kumi na wanne.

23Mwana wa Dani ni:

Hushimu.

2446:24 Mwa 30:8Wana wa Naftali ni:

Yaseeli, Guni, Yeseri na Shilemu.

2546:25 Mwa 30:8Hawa walikuwa wana wa Bilha aliomzalia Yakobo, ambaye Labani alikuwa amempa Raheli binti yake; jumla yao walikuwa saba.

2646:26 Kut 1:5; Kum 10:22Wote waliokwenda Misri pamoja na Yakobo, waliokuwa wazao wake hasa pasipo kuhesabu wakwe zake, walikuwa watu sitini na sita. 2746:27 Mdo 7:14Pamoja na wana wawili waliozaliwa na Yosefu huko Misri, jumla yote ya jamaa ya Yakobo, waliokwenda Misri, walikuwa sabini.

2846:28 Mwa 45:10Basi Yakobo akamtanguliza Yuda aende kwa Yosefu ili amwelekeze njia ya Gosheni. Walipofika nchi ya Gosheni, 2946:29 Mwa 29:11gari kubwa zuri la Yosefu liliandaliwa, naye akaenda Gosheni kumlaki baba yake Israeli. Mara Yosefu alipofika mbele yake, alimkumbatia baba yake, akalia kwa muda mrefu.

3046:30 Mwa 44:28Israeli akamwambia Yosefu, “Sasa niko tayari kufa, kwa kuwa nimejionea mwenyewe kwamba bado uko hai.”

3146:31 Mwa 45:10Ndipo Yosefu akawaambia ndugu zake na watu wa nyumbani mwa baba yake, “Nitapanda kwa Farao na kumwambia, ‘Ndugu zangu na watu wa nyumbani mwa baba yangu, waliokuwa wakiishi katika nchi ya Kanaani, wamekuja kwangu. 3246:32 Mwa 42:20Watu hao ni wachunga mifugo, huchunga mifugo, wamekuja na makundi ya kondoo, mbuzi na ngʼombe pamoja na kila kitu walicho nacho.’ 3346:33 Mwa 47:3Farao atakapowaita na kuwaulizeni, ‘Kazi yenu ni nini?’ 3446:34 Mwa 43:32Mjibuni, ‘Watumwa wako wamekuwa wachunga mifugo tangu ujana wetu mpaka sasa, kama baba zetu walivyofanya.’ Ndipo mtakaporuhusiwa kukaa katika nchi ya Gosheni, kwa kuwa wachunga mifugo wote ni chukizo kwa Wamisri.”