創世記 39 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

創世記 39:1-23

約瑟遭陷害

1約瑟以實瑪利商人帶到埃及,賣給了法老的內臣護衛長波提乏2約瑟住在他的埃及主人家中,耶和華與他同在,使他凡事亨通。 3他主人看出耶和華與他同在,使他凡事亨通, 4就賞識他,讓他服侍自己,派他管理自己家中一切事務。 5自從埃及波提乏約瑟管理自己家中一切事務以後,耶和華因為約瑟的緣故而賜福他主人家,使他主人家裡和田間的一切都蒙福。 6於是,波提乏把一切事都交給約瑟管理,除了自己要吃的食物以外,什麼也不管。

約瑟體格健壯,相貌英俊。 7後來,波提乏的妻子看中了約瑟,向他眉目傳情,要引誘他上床。 8約瑟拒絕了她,說:「我主人信任我,把家裡一切事都交給我管理。 9在這家裡,沒有人比我權力更大了,我主人把一切都交給了我,唯獨你除外,因為你是他的妻子。我怎能做這種醜事得罪上帝呢?」 10但她還是每天勾引約瑟約瑟不從,並儘量避開她。

11一天,約瑟進屋裡辦事,那時屋裡沒有其他人。 12波提乏的妻子抓住約瑟的外衣,硬要與他上床。約瑟丟下外衣擺脫她逃了出去。 13她見約瑟丟下外衣逃了出去, 14就叫來家裡的人,對他們說:「你們看,我丈夫帶回家的這個希伯來人戲弄我們!他進來要與我上床,我就大聲呼喊, 15他聽見我大聲喊叫,就把衣服丟在我這裡,逃了出去。」 16她把約瑟的外衣留在身邊,等她丈夫回來後, 17就對他說:「你帶回來的那個希伯來人進來要戲弄我, 18我大聲喊叫,他就把衣服丟在我這裡,逃了出去。」

19波提乏聽了妻子講述約瑟如何對待她之後,勃然大怒, 20約瑟關進王囚禁犯人的監牢。 21約瑟坐牢的時候,耶和華與他同在,恩待他,使監獄長賞識他。 22監獄長把獄中所有囚犯及一切事務都交給約瑟管理。 23凡交到約瑟手中的事情,監獄長都很放心,因為耶和華與約瑟同在,使他凡事亨通。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 39:1-23

Yosefu Na Mke Wa Potifa

139:1 Mwa 37:36Wakati huu Yosefu alikuwa amechukuliwa mpaka Misri. Mmisri aliyeitwa Potifa aliyekuwa mmojawapo wa maafisa wa Farao, mkuu wa ulinzi, akamnunua Yosefu kutoka kwa Waishmaeli waliomleta Misri.

2Bwana alikuwa pamoja na Yosefu, naye akastawi, Yosefu akaishi nyumbani kwa bwana wake Mmisri. 339:3 Mwa 21:22; Za 1:3Potifa alipoona kuwa Bwana alikuwa pamoja na Yosefu na kwamba Bwana alimfanikisha kwa kila kitu alichokifanya, 439:4 1Fal 11:28Yosefu alipata kibali machoni pa Potifa, akamfanya mhudumu wake. Potifa akamweka kuwa msimamizi wa nyumba yake, naye akamkabidhi kuwa mwangalizi wa kila kitu alichokuwa nacho. 539:5 2Sam 6:11; Za 128:4Kuanzia wakati huo Potifa alipomweka Yosefu kuwa msimamizi wa nyumba na mali zake zote alizokuwa nazo, Bwana aliibariki nyumba ya Mmisri huyo kwa sababu ya Yosefu. Baraka ya Bwana ilikuwa juu ya kila kitu alichokuwa nacho Potifa, nyumbani na shambani. 6Kwa hiyo Potifa akamwachia Yosefu uangalizi wa kila kitu alichokuwa nacho, Yosefu alipokuwa katika uongozi, Potifa hakuwa na sababu ya kujishughulisha na kitu chochote isipokuwa chakula alichokula.

Yosefu alikuwa mwenye umbo zuri na sura ya kuvutia; 7baada ya kitambo mke wa Potifa akamtamani Yosefu, akamwambia, “Njoo, ukutane nami kimwili!”

839:8 Mit 6:23-24Lakini Yosefu akakataa. Akamwambia yule mwanamke, “Mimi nikiwa katika uongozi, bwana wangu hahusiki na kitu chochote katika nyumba hii, kila kitu alicho nacho amenikabidhi. 939:9 Hes 22:34Hapa nyumbani hakuna aliye mkuu kuliko mimi. Bwana wangu hakunizuilia kitu chochote isipokuwa wewe, kwa kuwa wewe ni mke wake. Nitawezaje basi kufanya uovu huu na kutenda dhambi dhidi ya Mungu?” 10Ingawa yule mwanamke aliendelea kumshawishi Yosefu siku baada ya siku, Yosefu alikataa kukutana naye kimwili wala kukaa karibu naye.

1139:11 Kut 18:20Siku moja Yosefu akaingia ndani ya nyumba kufanya kazi zake, wala hapakuwepo na mfanyakazi yeyote ndani ya nyumba. 1239:12 Mit 7:13; 2Tim 2:22Mke wa Potifa akashika vazi Yosefu alilokuwa amevaa, akamwambia, “Njoo tukutane kimwili!” Lakini Yosefu akaacha vazi lake mkononi mwa huyo mwanamke, akatoka nje ya nyumba akikimbia.

13Yule mwanamke alipoona kwamba Yosefu amemwachia vazi lake mkononi na kukimbilia nje ya nyumba, 1439:14 Kum 22:24, 27akawaita watumishi wake wa nyumbani, akawaambia, “Tazameni! Huyu Mwebrania ameletwa hapa kutudhihaki! Aliingia hapa ndani ili akutane nami kimwili, lakini nikapiga kelele. 15Aliposikia kelele za kuomba msaada, akaacha vazi lake kando yangu akakimbilia nje.”

16Yule mwanamke akaliweka lile vazi karibu naye mpaka Potifa aliporudi nyumbani. 1739:17 Kut 20:16; Mwa 14:13Ndipo akamweleza kisa hiki, akisema: “Yule mtumwa wa Kiebrania uliyetuletea alinijia ili kunidhihaki. 18Lakini mara nilipopiga kelele kuomba msaada, akaliacha vazi lake kando yangu akakimbia nje ya nyumba.”

19Potifa aliposikia kisa hiki mkewe alichomweleza, akisema, “Hivi ndivyo mtumwa wako alivyonitenda.” Hasira ya Potifa ikawaka. 2039:20 Za 105:18Potifa akamchukua Yosefu na kumweka gerezani, mahali ambapo wahalifu wa mfalme walikuwa wamefungwa.

Lakini wakati Yosefu alipokuwa huko gerezani, 2139:21 Kut 3:21; Mit 16:7Bwana alikuwa pamoja naye, akamhurumia na kumpa kibali mbele ya msimamizi wa gereza. 22Kwa hiyo msimamizi wa gereza akamweka Yosefu awe mkuu wa wafungwa pamoja na kusimamia yote ambayo yalitendeka mle gerezani. 2339:23 Mwa 21:20; Hes 14:43Msimamizi wa gereza hakujishughulisha tena na kitu chochote kilichokuwa chini ya uangalizi wa Yosefu, kwa sababu Bwana alikuwa pamoja na Yosefu akimfanikisha kwa kila alichofanya.