創世記 29 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

創世記 29:1-35

雅各到達舅父家

1雅各繼續前行,來到東方人住的地方, 2看見田間有一口井,有三群羊臥在井邊,因為當地人用那口井的水飲羊。井口蓋著一塊大石頭。 3羊群聚集在井旁的時候,牧人就把石頭挪開飲羊,隨後再把石頭挪回原處。

4雅各問牧人:「弟兄們,你們是從哪裡來的?」他們說:「我們是從哈蘭來的。」 5雅各問道:「你們認識拿鶴的孫子拉班嗎?」他們說:「我們認識。」 6雅各又問:「他好嗎?」他們回答說:「很好。你看,他的女兒拉結帶著羊群來了。」 7雅各對他們說:「太陽還高,不到把羊關起來的時候,你們飲了羊,再放牠們去吃草吧!」 8他們說:「不行,要等所有的羊群到齊,有人挪開井口的石頭後,才能飲羊。」

9他們還在說話的時候,拉結就帶著她父親的羊群來到井邊,她是個牧羊女。 10雅各看見表妹拉結和舅父拉班的羊群來了,就上前把井口的石頭挪開,飲他舅父的羊。 11他親吻拉結,並放聲大哭。 12雅各告訴拉結自己是她父親的外甥,是利百加的兒子。拉結便跑去告訴她父親。

13拉班聽見外甥雅各來了,就跑去迎接他,擁抱他,親吻他,然後把他接到自己家裡。雅各把事情的經過告訴他。 14拉班高興地說:「你真是我的骨肉之親啊!」雅各拉班家裡住了一個月。

雅各娶妻

15一天,拉班對他說:「雖然我們是親戚,也不能讓你白白地替我工作。告訴我,你希望得到什麼報酬?」 16拉班有兩個女兒,大的叫利亞,小的叫拉結17利亞兩眼無神29·17 兩眼無神」或譯「兩眼很美麗」。,而拉結長得美麗出眾。 18雅各愛上了拉結,於是對拉班說:「我願意為你工作七年,請你把拉結許配給我。」 19拉班說:「把她嫁給你比嫁給外人好,你就留下來吧!」 20雅各為了拉結拉班工作了七年。因為他深愛拉結,所以這七年在他眼中就像短短的幾天。

21一天,雅各拉班說:「期限已經滿了,現在請把我妻子給我,我好和她同房。」 22於是,拉班就擺設宴席款待當地的人。 23到了晚上,拉班卻把女兒利亞送給雅各雅各和她同房。 24拉班又把自己的婢女悉帕送給女兒利亞做婢女。

25第二天早上,雅各才發現娶的是利亞,就對拉班說:「你對我做的是什麼事啊!我服侍你不就是為了拉結嗎?你為什麼騙我?」 26拉班說:「依照本地的習俗,妹妹不能比姐姐先出嫁。 27等這七天的婚期過了,我就把拉結也許配給你,你再替我工作七年。」

28雅各同意了。過了七天,拉班把女兒拉結嫁給雅各29又把自己的婢女辟拉送給拉結30雅各也和拉結同房,他深愛拉結,勝過愛利亞。他又替拉班工作了七年。

雅各的兒女

31耶和華看見利亞失寵,就使利亞生育,但拉結卻不生育。 32利亞懷孕生了一個兒子,給孩子取名叫呂便29·32 呂便」意思是「看,一個兒子」,此詞發音像希伯來文「他看見了我的痛苦」一詞的發音。。她說:「耶和華看見了我的痛苦,現在我丈夫一定會愛我。」 33她又懷孕生了一個兒子,就說:「耶和華聽見了我丈夫不愛我,所以又給我這個兒子。」於是,她給孩子取名叫西緬29·33 西緬」意思是「聽見」。34她又再度懷孕,生了一個兒子,就說:「這次我丈夫一定會依戀我,因為我給他生了三個兒子。」於是,他給孩子取名叫利未29·34 利未」意思是「聯合」。35後來,利亞再次懷孕,生了一個兒子,她說:「這次我要讚美耶和華!」於是,她給孩子取名叫猶大29·35 猶大」意思是「讚美」。。之後,利亞停止了生育。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 29:1-35

Yakobo Awasili Padan-Aramu

129:1 Mwa 25:6Kisha Yakobo akaendelea na safari yake na akafika kwenye nchi za mataifa ya mashariki. 2Huko akaona kisima katika shamba, pamoja na makundi matatu ya kondoo yamelala karibu na kisima hicho kwa sababu walikuwa wanakunywa maji kutoka kwenye kisimani hicho. Jiwe lililokuwa mdomoni mwa kisima lilikuwa kubwa. 3Wakati kondoo wanapokuwa wamekusanyika hapo, wachungaji huvingirisha jiwe hilo kutoka kwenye mdomo wa kisima na kunywesha kondoo. Kisha hulirudisha jiwe mahali pake juu ya mdomo wa kisima.

429:4 Mwa 42:7; Amu 19:17Yakobo aliwauliza wachungaji, “Ndugu zangu, ninyi mmetoka wapi?”

Wakamjibu, “Tumetoka Harani.”

5Aliwaambia, “Je, mnamjua Labani, mjukuu wa Nahori?”

Wakamjibu, “Ndiyo, tunamfahamu.”

629:6 Mwa 30:22-27; Kut 2:16Kisha Yakobo akawauliza, “Je, yeye ni mzima?”

Wakasema, “Ndiyo, ni mzima, na hapa yuaja Raheli binti yake akiwa na kondoo.”

7Akasema, “Tazama, jua bado liko juu, si wakati wa kukusanya mifugo. Nywesheni kondoo na mwarudishe malishoni.”

8Walijibu, “Haiwezekani, mpaka kondoo wote wakusanyike na jiwe liwe limevingirishwa kutoka mdomo wa kisima. Ndipo tutanywesha kondoo.”

9Alipokuwa akizungumza nao, Raheli akaja pamoja na kondoo wa baba yake, kwa maana alikuwa mchunga kondoo. 10Yakobo alipomwona Raheli binti Labani, ndugu wa mama yake, pamoja na kondoo wa Labani, alikwenda na kulivingirisha jiwe kutoka mdomoni mwa kisima na kuwanywesha kondoo wa mjomba wake. 1129:11 Mwa 33:4Kisha Yakobo akambusu Raheli na akaanza kulia kwa sauti. 1229:12 Mwa 24:28; Lk 15:20Yakobo alikuwa amemwambia Raheli kuwa yeye alikuwa jamaa ya baba yake, na kwamba ni mwana wa Rebeka. Basi Raheli alikimbia na kumweleza baba yake.

1329:13 Mwa 24:29; Lk 15:20Mara Labani aliposikia habari kuhusu Yakobo, mwana wa ndugu yake, aliharakisha kwenda kumlaki. Akamkumbatia na kumbusu, halafu akamleta nyumbani kwake, kisha Yakobo akamwambia mambo yote. 1429:14 Amu 9:2; Isa 58:7Ndipo Labani akamwambia, “Wewe ni nyama yangu na damu yangu mwenyewe.”

Yakobo Awaoa Lea Na Raheli

Baada ya Yakobo kukaa kwa Labani mwezi mzima, 15Labani akamwambia, “Kwa vile wewe ni jamaa yangu, ndiyo sababu unifanyie kazi bila ujira? Niambie ujira wako utakuwa nini.”

1629:16 Mwa 30:9; Rut 4:2, 11Labani alikuwa na binti wawili, binti mkubwa aliitwa Lea na binti mdogo aliitwa Raheli. 17Lea alikuwa na macho dhaifu, lakini Raheli alikuwa na umbo la kupendeza na mzuri wa sura. 1829:18 Mwa 24:67; Hos 12:12Yakobo akampenda Raheli, akamwambia Labani, “Nitakutumikia kwa miaka saba kwa ajili ya kumpata Raheli binti yako mdogo.”

19Labani akasema, “Ni bora zaidi nikupe Raheli kuliko kumpa mtu mwingine yeyote. Kaa pamoja na mimi hapa.” 20Kwa hiyo Yakobo akatumika miaka saba ili kumpata Raheli, lakini ilionekana kwake kama siku chache tu kwa sababu ya upendo wake kwa Raheli.

2129:21 Amu 15:1Ndipo Yakobo akamwambia Labani, “Nipe mke wangu. Muda wangu umekamilika, nami nataka nikutane naye kimwili.”

2229:22 Amu 14:10; Yn 2:1-2Basi Labani akaalika watu wote wa mahali pale na akafanya karamu.

23Lakini ilipofika jioni, akamchukua Lea binti yake akampa Yakobo, naye Yakobo akakutana naye kimwili. 24Naye Labani akamtoa Zilpa, mtumishi wake wa kike, kuwa mtumishi wa Lea, binti yake.

2529:25 Mwa 12:18; 27:36Kesho yake asubuhi, Yakobo akagundua kuwa amepewa Lea! Basi Yakobo akamwambia Labani, “Ni jambo gani hili ulilonitendea? Nilikutumikia kwa ajili ya Raheli, sivyo? Kwa nini umenidanganya?”

2629:26 1Sam 14:49; 2Sam 6:23Labani akajibu, “Si desturi yetu kumwoza binti mdogo kabla ya kumwoza binti mkubwa. 27Maliza juma la arusi ya binti huyu, kisha pia nitakupa huyu binti mdogo, kwa kutumika miaka mingine saba.”

28Naye Yakobo akafanya hivyo. Akamaliza juma na Lea, kisha Labani akampa Raheli binti yake kuwa mke wake. 2929:29 1Nya 5:1; Mwa 16:1Labani akamtoa Bilha mtumishi wake wa kike kwa Raheli ili kuwa mtumishi wake. 30Pia Yakobo akakutana na Raheli kimwili, naye akampenda Raheli zaidi kuliko Lea. Yakobo akamtumikia Labani kwa miaka mingine saba.

Wana Wa Yakobo

3129:31 Kum 21:15-17; Za 127:3Bwana alipoona kwamba Lea hapendwi, akampa watoto, lakini Raheli alikuwa tasa. 3229:32 Mwa 30:23; Hes 1:5Lea akapata mimba akazaa mwana. Akamwita Reubeni,29:32 Reubeni maana yake Ona mwana, yaani Yehova ameangalia taabu yangu. kwa maana alisema, “Ni kwa sababu Bwana ameona huzuni yangu. Hakika mume wangu sasa atanipenda.”

3329:33 Kut 6:15; 1Nya 4:24Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Kwa sababu Bwana alisikia kwamba sipendwi, amenipa tena huyu mwana.” Kwa hiyo akamwita Simeoni.29:33 Simeoni maana yake Anasikia, yaani sasa ataungana nami kama Raheli.

34Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Sasa afadhali mume wangu ataambatana na mimi, kwa sababu nimemzalia wana watatu.” Kwa hiyo akamwita Lawi.29:34 Lawi maana yake Nimeunganishwa, yaani na mume wangu.

3529:35 Mwa 49:8; Mt 1:2-3Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Wakati huu nitamsifu Bwana.” Kwa hiyo akamwita Yuda.29:35 Yuda maana yake Sifa, yaani Nitamsifu Yehova. Kisha akaacha kuzaa watoto.