列王紀下 17 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

列王紀下 17:1-41

何細亞做以色列王

1猶大亞哈斯執政第十二年,以拉的兒子何細亞撒瑪利亞登基做以色列王,執政九年。 2他做耶和華視為惡的事,不過沒有他之前的以色列諸王那麼敗壞。 3亞述撒縵以色攻打以色列何細亞納貢稱臣。 4然而,何細亞差遣使者向埃及求援,不再像往年那樣向亞述王進貢。亞述王發現後,把他抓起來囚在獄中。 5亞述王攻打以色列全境,並圍困撒瑪利亞三年。 6何細亞執政第九年,撒瑪利亞淪陷。亞述王把以色列人擄到亞述,安置在哈臘歌散哈博河一帶以及瑪代人的各城。

以色列人的罪惡史

7以色列人之所以有如此下場,是因為他們的上帝耶和華領他們出埃及,從埃及王法老手中救出他們,他們卻犯罪得罪祂。他們祭拜別的神明, 8效法耶和華在他們面前趕走的外族人的風俗和以色列諸王奉行的習俗。 9以色列人暗中做不義之事,冒犯他們的上帝耶和華。從瞭望塔到堅城,他們在各地建邱壇, 10在各高崗上、綠樹下立神柱和亞舍拉神像, 11在各邱壇燒香,如同耶和華在他們面前趕走的外族人一樣。他們邪惡的行為激怒了耶和華。 12儘管耶和華警告他們不可祭拜偶像,他們仍然執迷不悟。

13耶和華藉著祂的眾先知和先見警告以色列人和猶大人說:「你們要離開惡道,遵守我的誡命和律例,即我吩咐你們祖先遵守並藉著我的僕人——眾先知傳給你們的律法。」 14但他們充耳不聞,像他們祖先一樣頑固不化,不信靠他們的上帝耶和華, 15拒絕遵守祂的律例和祂與他們祖先所立的約,無視祂的警告。他們隨從虛無的偶像,自己也變得虛無。他們違背耶和華的命令,去效法周圍的外族人。 16他們把他們的上帝耶和華的誡命拋諸腦後,鑄造了兩個金牛犢,還造了亞舍拉神像。他們祭拜巴力和天上的萬象, 17把自己的兒女燒死獻作祭物。他們占卜,行邪術,出賣自己去做耶和華視為惡的事,惹祂發怒。

18因此,耶和華非常憤怒,從祂面前趕走以色列人,只留下猶大一個支派。 19猶大人也不遵守他們的上帝耶和華的誡命,反而效法以色列人的惡行。 20於是,耶和華棄絕了以色列全族,使他們飽嚐痛苦,任人宰割,直至把他們從自己眼前趕走。 21祂使以色列大衛家分裂出來,以色列人便擁立尼八的兒子耶羅波安為王。耶羅波安誘使以色列人遠離耶和華,使他們犯了大罪。 22以色列人沉溺於耶羅波安所犯的一切罪中,始終不肯回頭, 23直到耶和華把他們從自己眼前趕走,正如祂藉自己的僕人——眾先知對他們的警告。這樣,以色列人被擄到亞述,至今仍住在那裡。

外族人移居撒瑪利亞

24亞述王把巴比倫古他亞瓦哈馬西法瓦音等地的一些居民遷移到撒瑪利亞各城,代替以色列人。 25剛遷居到那裡的時候,他們不敬拜耶和華,所以耶和華差遣獅子闖入他們當中,咬死了一些人。 26有人稟告亞述王說:「你遷移到撒瑪利亞各城的那些人不知道當地神明的規矩,所以神明就差遣獅子闖入他們當中,咬死了一些人。」 27亞述王便下令:「派一位被擄來的祭司回去,讓他住在那裡,把當地神明的規矩教導給他們。」 28於是,有一位從撒瑪利亞被擄走的祭司回去住在伯特利,教導他們怎樣敬拜耶和華。

29可是,這些從各地遷來的民族都在所住的各城為自己製造神像,供奉在撒瑪利亞人在高崗上建造的神廟中。 30巴比倫人造疏割·比訥神像,古他人造匿甲神像,哈馬人造亞示瑪神像, 31亞瓦人造匿哈他珥他神像,西法瓦音人焚燒兒女向他們的神明亞得米勒亞拿米勒獻祭。 32他們也敬拜耶和華,卻委任各種人做祭司,在高崗上的神廟為他們獻祭。 33他們就這樣既敬拜耶和華,又各按各的風俗供奉自己的神明。

34直到現在,他們仍然執迷不悟,不敬畏耶和華,也不遵行耶和華賜給雅各子孫的律例、典章、法度和誡命。耶和華曾給雅各取名叫以色列35與他的子孫立約,吩咐他們:「不可祭拜其他神明,不可跪拜和供奉他們,也不可向他們獻祭。 36耶和華伸出大能的臂膀把你們領出埃及,你們要敬拜祂,要向祂跪拜、獻祭。 37你們要永遠謹遵祂所定的律例、典章、法度和誡命,不可祭拜其他神明。 38不可忘記我與你們立的約,不可祭拜其他神明。 39我是你們的上帝耶和華,你們要敬拜我,我必從一切仇敵手中救你們。」 40但是他們沒有聽從,依然仿效先前的風俗。 41那些移民到撒瑪利亞各城的外族人既敬拜耶和華,又供奉自己的偶像。直到今日,他們的子孫仍是這樣。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 17:1-41

Hoshea, Mfalme Wa Mwisho Katika Israeli

117:1 2Fal 15:30Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Ahazi mfalme wa Yuda, Hoshea mwana wa Ela akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, akatawala kwa miaka tisa. 217:2 Kum 4:25Akafanya maovu machoni pa Bwana, lakini si kama wafalme wengine wa Israeli waliomtangulia.

317:3 Hos 10:14; Amu 3:15Mfalme Shalmanesa wa Ashuru akainuka dhidi ya Mfalme Hoshea, ambaye hapo mbeleni alikuwa mtumwa wake na kumlipa ushuru. 417:4 Za 146:3; Hos 13:10Lakini mfalme wa Ashuru akagundua kuwa Hoshea alikuwa msaliti, kwa kuwa alikuwa ametuma wajumbe kwa So mfalme wa Misri, naye hakuendelea kulipa ushuru kwa mfalme wa Ashuru tena kama alivyokuwa anafanya kila mwaka. Kwa hiyo Shalmanesa akamkamata na kumtia gerezani. 5Mfalme wa Ashuru akaishambulia nchi yote, akapigana dhidi ya Samaria na kuizunguka kwa majeshi miaka mitatu. 617:6 2Fal 15:29; Isa 10:9Katika mwaka wa tisa wa Hoshea, mfalme wa Ashuru akaiteka Samaria na kuwahamishia Waisraeli huko Ashuru. Akawaweka huko Hala, na Gozani karibu na Mto Habori, na katika miji ya Wamedi.

Israeli Inakwenda Uhamishoni Kwa Sababu Ya Dhambi

717:7 Yos 7:11; Kut 14:15-31Yote haya yalitokea kwa sababu Waisraeli walikuwa wametenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wao, ambaye alikuwa amewapandisha kutoka Misri akiwatoa chini ya utawala wa nguvu wa Farao mfalme wa Misri. Waliabudu miungu mingine 817:8 Law 18:3; Kum 9:4na kufuata desturi za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao, pamoja na desturi ambazo wafalme wa Israeli walizileta. 917:9 2Fal 18:8Waisraeli wakafanya vitu kwa siri dhidi ya Bwana Mungu wao, ambavyo havikuwa sawa. Kuanzia kwenye mnara wa ulinzi hadi kwenye mji wenye maboma walijijengea wenyewe mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji yao yote. 1017:10 Kut 34:13; Mik 5:14Wakaweka mawe ya kuabudiwa na nguzo za Ashera juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila mti uliotanda. 11Wakafukiza uvumba kila mahali palipoinuka, kama yalivyofanya yale mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao. Wakafanya mambo maovu ambayo yalimghadhibisha Bwana. 1217:12 Kut 20:4Wakaabudu sanamu, ingawa Bwana alikuwa amesema, “Msifanye mambo haya.” 1317:13 1Sam 9:9; Yer 18:11; Zek 1:4Bwana akawaonya Israeli na Yuda kupitia kwa manabii na waonaji wake wote: “Acheni njia zenu mbaya. Shikeni amri na maagizo yangu, kufuatana na sheria yangu yote niliyowaagiza baba zenu kuitii ambayo niliileta kwenu kupitia kwa watumishi wangu manabii.”

1417:14 Kut 32:9; Mdo 7:15Lakini hawakusikiliza, walikuwa na shingo ngumu kama baba zao, ambao hawakumtegemea Bwana Mungu wao. 1517:15 Law 26:11; Kum 32:21Walizikataa amri zake, na agano alilokuwa amelifanya na baba zao, na maonyo aliyokuwa amewapa. Wakafuata sanamu zisizofaa, nao wenyewe wakawa hawafai. Wakayaiga mataifa yaliyowazunguka, ingawa Bwana alikuwa amewaonya akiwaambia, “Msifanye kama wanavyofanya,” nao wakafanya mambo ambayo Bwana alikuwa amewakataza wasifanye.

1617:16 Kut 32:4; Yer 2:5Wakayaacha maagizo yote ya Bwana Mungu wao na kujitengenezea sanamu mbili, walizozisubu katika sura ya ndama na nguzo ya Ashera. Wakasujudia mianga yote ya angani, na wakamtumikia Baali. 1717:17 Kum 18:10-12; Rum 7:14Wakawatoa kafara wana wao na mabinti zao katika moto. Wakafanya uaguzi na uchawi, nao wakajiuza wenyewe katika kutenda uovu machoni pa Bwana, wakamghadhibisha.

18Basi Bwana akawakasirikia sana Israeli na kuwaondoa kwenye uwepo wake. Ni kabila la Yuda tu lililobaki; 19na hata hivyo nao Yuda hawakuzishika amri za Bwana Mungu wao. Wakafuata desturi ambazo Israeli walikuwa wamezianzisha. 2017:20 2Fal 17:6Kwa hiyo Bwana aliwakataa watu wote wa Israeli; akawatesa na kuwaachia katika mikono ya wateka nyara hadi alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake.

2117:21 1Sam 15:27; 1Fal 12:20Alipokwisha kuwatenga Israeli mbali na nyumba ya Daudi, wakamfanya Yeroboamu mwana wa Nebati kuwa mfalme wao. Yeroboamu akawashawishi Israeli waache kumfuata Bwana na akawasababisha kutenda dhambi kuu. 22Nao Israeli wakadumu katika dhambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati, nao hawakuziacha 2317:23 Eze 39:23-24; Amu 6:8hadi Bwana alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake, kama vile alivyokuwa ameonya kupitia watumishi wake wote manabii. Hivyo watu wa Israeli wakaondolewa kutoka nchi yao kwenda uhamishoni Ashuru, nao wako huko mpaka sasa.

Samaria Inakaliwa Tena

2417:24 2Fal 18:34; Amo 6:2Mfalme wa Ashuru akawaleta watu kutoka Babeli, Kutha, Ava, Hamathi na Sefarvaimu na kuwaweka katika miji ya Samaria badala ya Waisraeli. Wakaimiliki Samaria na kuishi katika miji yake. 2517:25 Mwa 37:20; Yer 50:17Wakati walianza kuishi humo, hawakumwabudu Bwana, kwa hiyo akatuma simba miongoni mwao, wakawaua baadhi ya watu. 26Habari ikapelekwa kwa mfalme wa Ashuru, kusema: “Watu uliowahamisha na kuwaweka katika miji ya Samaria hawajui kile Mungu wa nchi hiyo anachokitaka. Ametuma simba miongoni mwao, ambao wanawaua, kwa sababu watu hawajui anachokitaka.”

27Ndipo mfalme wa Ashuru akaamuru hivi: “Mtwae mmoja wa makuhani uliowachukua mateka kutoka Samaria ili arudi kuishi humo na awafundishe watu kile ambacho Mungu wa nchi anataka.” 28Basi mmoja wa makuhani ambaye alikuwa amepelekwa uhamishoni kutoka Samaria akaja kuishi Betheli na kuwafundisha jinsi ya kumwabudu Bwana.

2917:29 Yer 2:28; Mik 4:5Hata hivyo, kila kikundi cha taifa lililoletwa Samaria kilitengeneza miungu yao wenyewe katika miji kadhaa mahali walipoishi, nao wakaiweka mahali pa ibada za miungu ambapo watu wa Samaria walikuwa wametengeneza katika mahali pa juu. 30Watu kutoka Babeli wakamtengeneza Sukoth-Benothi kuwa mungu wao, watu kutoka Kutha wakamtengeneza Nergali, na watu kutoka Hamathi wakamtengeneza Ashima; 3117:31 2Fal 17:24Waavi wakatengeneza Nibhazi na Tartaki, nao Wasefarvi wakachoma watoto wao kama kafara kwa Adrameleki na Anameleki, miungu ya Sefarvaimu. 3217:32 1Fal 12:31Walimwabudu Bwana, lakini pia waliteua aina zote za watu wao ili kuwawakilisha kama makuhani katika mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu pa ibada. 33Walimwabudu Bwana, lakini pia waliitumikia miungu yao kulingana na desturi za mataifa walikotoka.

3417:34 Mwa 17:5; 1Fal 18:31Mpaka leo wanashikilia desturi zao za zamani. Hawamwabudu Bwana wala kuzishika hukumu na maagizo, sheria na amri ambazo Bwana aliwapa uzao wa Yakobo, ambaye alimwita Israeli. 3517:35 Kut 20:3Wakati Bwana alipofanya Agano na Waisraeli, aliwaamuru akisema: “Msiiabudu miungu mingine yoyote wala kuisujudia, wala kuitumikia wala kuitolea dhabihu. 3617:36 Kum 3:20; Za 136:12Bali imewapasa kumwabudu Bwana aliyewapandisha kutoka Misri kwa uwezo wake mkuu na kwa mkono wake ulionyooshwa. Kwake yeye mtasujudu na kwake yeye mtatoa dhabihu. 3717:37 Kum 5:32; Law 19:37Imewapasa daima kuwa waangalifu kutunza hukumu na maagizo, sheria na amri alizowaandikia. Msiabudu miungu mingine. 3817:38 Kum 6:12Msisahau agano nililofanya nanyi, wala msiabudu miungu mingine. 39Bali, mtamwabudu Bwana Mungu wenu, kwani yeye ndiye atakayewakomboa kutoka mikononi mwa adui zenu wote.”

40Hata hivyo hawakusikiliza, lakini waliendelea na desturi zao za awali. 4117:41 1Fal 18:21; Mt 6:24Hata wakati watu hawa walipokuwa wanamwabudu Bwana, walikuwa bado wakitumikia sanamu zao. Mpaka leo watoto wao na watoto wa watoto wao wanaendelea kufanya kama baba zao walivyofanya.