出埃及記 35 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

出埃及記 35:1-35

安息日的條例

1摩西招聚以色列全體會眾,對他們宣佈說:「以下是耶和華吩咐你們遵守的事。 2一週可以工作六天,但第七天是聖日,是你們為耶和華守安息的日子。凡在這一天工作的,必被處死。 3在安息日,家家戶戶都不可生火。」

為造聖幕奉獻

4摩西以色列全體會眾說:「以下是耶和華給你們的吩咐。

5「凡慷慨樂捐的,都可以把下列物品獻給耶和華為禮物,即金,銀,銅, 6細麻線,山羊毛,藍色、紫色和朱紅色的線, 7染成紅色的公羊皮,海狗皮,皂莢木, 8燈油,製作膏油和香的香料, 9鑲嵌在以弗得和胸牌上的紅瑪瑙及其他寶石。

10「你們當中的能工巧匠都要來建造耶和華所吩咐的物件, 11即聖幕和聖幕的罩棚、頂蓋、鉤子、木板、橫閂、柱子和底座; 12約櫃和抬約櫃的橫杠、施恩座和遮掩約櫃的幔子; 13桌子和抬桌子的橫杠、桌上的一切器具和供餅; 14燈臺和燈臺用的器具、燈盞和燈油; 15香壇和抬香壇的橫杠、膏油和芬芳的香;聖幕門口的簾子; 16燔祭壇、祭壇的銅網、抬祭壇的橫杠、祭壇用的一切器具、洗濯盆和盆座; 17院子的帷幔、懸掛幔子的柱子和底座、遮擋院子入口的門簾; 18聖幕和院子用的橛子和繩索; 19在聖所供職時穿的精製禮服、亞倫祭司的聖衣及其眾子供祭司之職時穿的衣服。」

20摩西說完後,以色列全體會眾便從他面前退去。 21凡心裡有感動又甘願奉獻的,都把禮物拿來獻給耶和華,作會幕、會幕中的一切器具及聖衣之用。 22凡甘心奉獻的,不論男女,都把別針、耳環、戒指、項鏈等各樣金飾拿來獻給耶和華。 23凡有細麻線,山羊毛,藍色、紫色和朱紅色的線,染成紅色的公羊皮,海狗皮的,都把它們拿來了。 24凡奉獻銀器和銅器的,都拿來獻給耶和華。凡有皂莢木的,只要用得上,都拿來奉獻。 25凡懂得紡線的婦女,都把親手紡成的細麻線和藍色、紫色、朱紅色的線拿來奉獻。 26凡心裡受感動又懂得紡織的婦女都來紡山羊毛。 27眾首領奉獻了紅瑪瑙和其他寶石,用來鑲嵌在以弗得和胸牌上。 28他們又獻出香料和油,用來做香、點燈、做膏油。 29以色列人,不論男女、凡是甘心樂意奉獻的,都把禮物帶來獻給耶和華,好完成耶和華藉摩西吩咐他們的一切工作。

30摩西以色列人說:「看啊,耶和華已經親自選出猶大支派中戶珥的孫子、烏利的兒子比撒列31上帝的靈已經充滿他,使他有聰明智慧,精於各種技能和手藝, 32懂得用金、銀和銅製造各式各樣精巧的器具, 33又能雕刻和鑲嵌寶石,精通木工和各種手藝。 34耶和華又使他與支派亞希撒抹的兒子亞何利亞伯有能力教授別人。 35耶和華使他們成為能工巧匠,精通各樣技藝,包括雕刻、圖案設計、紡織以及用細麻線和藍色、紫色、朱紅色的線刺繡。」

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 35:1-35

Masharti Ya Sabato

135:1 Kut 34:32Mose akakusanya jumuiya yote ya Waisraeli na kuwaambia, “Haya ndiyo mambo ambayo Bwana amewaamuru ninyi mfanye: 235:2 Law 23:3; Mwa 2:3; Kut 34:21; Kum 5:13-14; Kut 31:14, 15; Hes 15:32; Lk 13:14Kwa siku sita, mtafanya kazi, lakini siku ya saba itakuwa takatifu kwenu, Sabato ya kupumzika kwa Bwana. Yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo ni lazima auawe. 335:3 Kut 16:23Msiwashe moto mahali popote katika makazi yenu siku ya Sabato.”

Vifaa Kwa Ajili Ya Maskani Ya Mungu

(Kutoka 25:1-9)

435:4 Kut 25:1, 2Mose akaiambia jumuiya yote ya Waisraeli, “Hili ndilo Bwana aliloamuru: 535:5 Kut 25:2; 2Kor 9:7Toeni sadaka kwa Bwana kutoka mali mliyo nayo. Kila mmoja aliye na moyo wa kupenda atamletea Bwana sadaka ya dhahabu, fedha na shaba; 6nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi; singa za mbuzi; 7ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo;35:7 Pomboo hapa ina maana ya mnyama mwenye ngozi laini aishiye kwenye milima yenye misitu, au pengine nguva au sili. mbao za mshita; 835:8 Kut 25:6mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri; 9vito vya shohamu, na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.

1035:10 Kut 31:6; 39:43; 1Fal 7:14; Isa 28:26“Wote wenye ujuzi miongoni mwenu inawapasa kuja na kutengeneza kila kitu Bwana alichoamuru: 1135:11 Kut 26:1-37; 36:8-38; Mdo 7:44, 45; Ebr 8:2, 5; 9:2-11; Ufu 21:3Maskani pamoja na hema lake na kifuniko chake, vibanio, mihimili, mataruma, nguzo na vitako; 1235:12 Kut 25:10-22; 37:1-9; 26:33Sanduku la Agano pamoja na mipiko yake, kifuniko cha kiti cha rehema na pazia linalokizuia; 1335:13 Kut 25:23-30; 37:10-16meza na mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, mikate ya Wonyesho; 1435:14 Kut 25:31kinara cha taa kwa ajili ya mwanga pamoja na vifaa vyake vyote, taa na mafuta kwa ajili ya mwanga; 1535:15 Kut 30:1-6; 37:26-28; 30:34-38; 26:36; 1Sam 2:28; 1Nya 23:13; 2Nya 29:11; Lk 1:9madhabahu ya kufukiza uvumba pamoja na mipiko yake, mafuta ya upako na uvumba wenye harufu nzuri; pazia la mlangoni mahali pa kuingilia ndani ya maskani; 1635:16 Kut 27:1-8; 38:1-7; 30:18madhabahu ya sadaka za kuteketeza pamoja na wavu wake wa shaba, mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote; sinia la shaba pamoja na tako lake; 1735:17 Kut 27:9; 38:9-20pazia la eneo la ua pamoja na nguzo zake na vitako vyake, pazia la ingilio la kwenye ua; 1835:18 Kut 27:19; 38:20vigingi vya hema kwa ajili ya maskani pamoja na ua na kamba zake; 1935:19 Kut 28:2; 31:10; 39:1mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu kwa ajili ya kuhani Aroni, na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.”

20Ndipo jumuiya yote ya Waisraeli ilipoondoka mbele ya Mose, 2135:21 Kut 25:2; 36:2; 1Nya 28:2, 9; 29:9; Ezr 7:27; 2Kor 8:12; 9:7na kila mmoja aliyependa na ambaye moyo wake ulimsukuma alikuja na kuleta sadaka kwa Bwana, kwa ajili ya kazi katika Hema la Kukutania, kwa ajili ya huduma yake yote na kwa ajili ya mavazi matakatifu. 22Wote waliokuwa na utayari, wanaume kwa wanawake, wakaja wakaleta vito vya dhahabu vya kila aina: vipini, vipuli, pete na mapambo. Wote wakatoa dhahabu zao kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana. 2335:23 Kut 39:1; 1Nya 29:8Kila mmoja aliyekuwa na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi, au singa za mbuzi, ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, au ngozi za pomboo, wakavileta. 24Wale waliotoa sadaka ya fedha au shaba wakavileta kama sadaka kwa Bwana, na kila aliyekuwa na mti wa mshita kwa ajili ya kazi yoyote ile akauleta. 2535:25 Kut 28:3; 31:6; 36:1; 2Fal 23:7; Mit 31:19-24Kila mwanamke aliyekuwa na ujuzi alisokota kwa mikono yake na alileta kile alichosokota, iwe ni nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi. 2635:26 Kut 25:2; 1Nya 29:6-8Wanawake wote waliopenda na waliokuwa na ujuzi wakasokota singa za mbuzi. 27Viongozi wakaleta vito vya shohamu pamoja na vito vingine vya thamani kwa ajili ya kuweka kwenye kisibau na kwenye kifuko cha kifuani. 2835:28 Kut 25:6Wakaleta pia vikolezi na mafuta ya zeituni kwa ajili ya mwanga, kwa ajili ya mafuta ya upako na kwa ajili ya uvumba wenye harufu nzuri. 2935:29 Kut 25:2-7; 36:3; 2Fal 12:4Waisraeli wote waume kwa wake waliokuwa wanapenda wakaleta mbele za Bwana kwa hiari yao wenyewe sadaka kwa ajili ya kazi yote ya Bwana aliyokuwa amewaagiza kuifanya kupitia kwa Mose.

Bezaleli Na Oholiabu

(Kutoka 31:1-11)

30Kisha Mose akawaambia Waisraeli, “Tazameni, Bwana amemchagua Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda, 3135:31 2Nya 2:7, 14naye amemjaza Roho wa Mungu, pamoja na ustadi, na uwezo na ujuzi katika aina zote za ufundi, 32ili kubuni michoro ya kupendeza katika ufundi wa dhahabu, fedha na shaba, 33kuchonga vito na kuvitia mahali, kufanya ufundi kwa mbao, na kujishughulisha na aina zote za ufundi wa kupendeza. 3435:34 Kut 31:6; 2Nya 2:14Tena amempa yeye pamoja na Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, uwezo wa kufundisha wengine. 3535:35 Kut 31:3, 6; 36:1, 2; 1Fal 7:14; 1Nya 2:14; Isa 28:26; Yak 1:5Amewajaza ustadi wa kufanya kazi za aina zote zifanywazo na mafundi, na wenye kubuni michoro, pia na watarizi kwa rangi za buluu, zambarau, nyekundu na kitani safi, na wafumaji: wote wakiwa mafundi na wabunifu hodari.