出埃及記 31 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

出埃及記 31:1-18

會幕的工匠

1耶和華對摩西說: 2「看啊,在猶大支派中我已經親自選出戶珥的孫子、烏利的兒子比撒列3用我的靈充滿他,使他有聰明智慧,精於各種技能和手藝, 4懂得用金、銀和銅製造各式各樣精巧的器具, 5又能雕刻和鑲嵌寶石,精通木工和各種手藝。 6我委派支派亞希撒抹的兒子亞何利亞伯做他的助手。至於其他能工巧匠,我已賜給他們智慧,好照我對你的吩咐製造一切器具, 7即會幕、約櫃和約櫃上面的施恩座、會幕裡面所有的器具、 8桌子和桌上的器具、純金的燈臺和燈臺的一切器具、香壇、 9燔祭壇和壇上的一切器具、洗濯盆和盆座, 10還有精工製作的禮服,即亞倫祭司的聖衣及其眾子供祭司之職時穿的禮服, 11以及膏油和聖所使用的芬芳的香。他們要照我對你的吩咐去做。」

安息日

12耶和華對摩西說: 13「你要吩咐以色列百姓務必守我的安息日,因為這是我與你們之間世世代代的記號,叫你們知道使你們聖潔的是我耶和華。 14你們要守安息日,以它為聖日。凡不守這誡命的,必被處死。凡在這天工作的,必從民中被剷除。 15一週要工作六天,第七天是莊嚴的安息日,是耶和華的聖日。凡在安息日做工的,必被處死。 16因此,以色列人世世代代都要守安息日,作為永久的約, 17這是我和以色列人之間永久的記號。耶和華用六天的時間創造天地萬物,在第七天停工休息。」 18耶和華在西奈山對摩西說完這些話以後,就把自己用指頭刻上誡命的兩塊石版交給摩西

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 31:1-18

Bezaleli Na Oholiabu

(Kutoka 35:30–36:1)

1Ndipo Bwana akamwambia Mose, 231:2 Kut 36:1-2; 37:1; 38:22; 1Nya 21:20; 2Nya 1:5; Kut 17:10“Tazama, nimemchagua Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda, 331:3 Kut 28:3; 1Fal 7:14; 1Kor 12:4; Kut 35:31; Isa 28:26nami nimemjaza Roho wa Mungu, pamoja na ustadi, uwezo na ujuzi katika aina zote za ufundi, 4ili kubuni michoro ya kupendeza katika ufundi wa dhahabu, fedha na shaba, 5kuchonga vito na kuvitia mahali, kufanya ufundi kwa mbao, na kujishughulisha na aina zote za ufundi. 631:6 Kut 36:1-2; 38:23; 1Fal 7:14; 2Nya 2:14Tena nimemteua Oholiabu mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, ili kumsaidia. Pia mafundi wote nimewapa ustadi wa kutengeneza kila kitu nilichokuamuru wewe: 731:7 Kut 36:8-38; 37:1-6; 40:20Hema la Kukutania, Sanduku la Ushuhuda pamoja na kiti cha rehema juu yake, pia na vifaa vyote vya kwenye hema, 831:8 Kut 37:10-24; Law 24:4; Kut 37:25-28meza na vifaa vyake, kinara cha taa cha dhahabu safi na vifaa vyake vyote, madhabahu ya kufukizia uvumba, 931:9 Kut 38:3; Hes 4:14; Kut 30:18madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake vyote, sinia na kinara chake, 1031:10 Kut 28:2; 39:1, 41pamoja na mavazi matakatifu yaliyofumwa ya kuhani Aroni, na mavazi kwa ajili ya wanawe wakati wanahudumu katika kazi ya ukuhani, 1131:11 Kut 30:22-32; 37:29; 25:6-9pia mafuta ya upako na uvumba wenye harufu nzuri kwa ajili ya Mahali Patakatifu. Watavitengeneza sawasawa kama vile nilivyokuagiza wewe.”

Sabato

12Kisha Bwana akamwambia Mose, 1331:13 Kut 20:8; Isa 56:4; Eze 20:12, 20; Kut 29:42; Law 11:44; 20:8; Eze 37:28“Waambie Waisraeli, ‘Ninyi ni lazima mzishike Sabato zangu. Hii itakuwa ni ishara kati yangu na ninyi kwa ajili ya vizazi vijavyo, ili mpate kujua kwamba Mimi Ndimi Bwana, niwafanyaye ninyi watakatifu.

1431:14 Kut 35:2; Hes 15:32-36“ ‘Mtaishika Sabato, kwa sababu ni takatifu kwenu. Yeyote atakayeinajisi lazima auawe, yeyote atakayefanya kazi siku hiyo lazima akafie mbali na watu wake. 1531:15 Kut 20:8-11; 35:2; Law 16:29; 23:3; Hes 29:7; Mwa 2:3Kwa siku sita, mtafanya kazi, lakini siku ya saba ni Sabato ya kupumzika, takatifu kwa Bwana. Yeyote afanyaye kazi yoyote siku ya Sabato ni lazima auawe. 1631:16 Kut 20:8Waisraeli wataishika Sabato, kuiadhimisha kwa vizazi vijavyo kuwa Agano la milele. 1731:17 Mwa 2:2-3; Kut 20:9; Isa 56:2; 58:13; 66:23; Yer 17:21-22; Eze 20:12, 20Itakuwa ishara kati yangu na Waisraeli milele, kwa kuwa kwa muda wa siku sita Bwana aliumba mbingu na dunia, na siku ya saba akaacha kufanya kazi, akapumzika.’ ”

1831:18 Kut 19:11; 24:12; 2Kor 3:3; Ebr 9:4; Kut 32:15-16; 34:1; 28; Kum 4:30; 9:10Bwana alipomaliza kusema na Mose juu ya Mlima Sinai, Mungu akampa vile vibao viwili vya Ushuhuda, vibao vya mawe vilivyoandikwa kwa kidole cha Mungu.