出埃及記 22 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

出埃及記 22:1-31

賠償條例

1「倘若有人偷了別人的牛羊,然後宰了或賣了,他要用五頭牛抵償一頭牛,四隻羊抵償一隻羊。 2倘若有人打死正入屋偷竊的賊,這人不算犯殺人罪。 3倘若事情發生在白天,家主就犯了殺人罪。倘若盜賊被擒,他就要賠償家主,若他一無所有,就要把他賣為奴隸作賠償。 4倘若他偷的牲畜如牛、羊或驢在他手上還活著,他要償還失主雙倍。

5「倘若有人在田野或葡萄園裡牧放牲畜,任由牲畜吃別人田裡的農作物或葡萄,他必須拿自己田裡最好的農作物或葡萄作賠償。 6倘若有人在自己的田間焚燒荊棘,不小心燒掉了別人的莊稼、禾捆或整個田園,那生火的人就要賠償一切損失。

7「倘若有人把金錢或物件交給鄰居保管,鄰居家遭盜,盜賊被緝拿歸案後要賠償雙倍; 8倘若沒捉到盜賊,鄰居就要到審判官那裡證明自己沒有偷拿。 9倘若二人之間有什麼糾紛,無論是為了牛、驢、羊、衣服或失物,爭執的雙方要把案件呈報審判官,審判官判誰敗訴,誰就要賠償雙倍。 10倘若有人把驢、牛、羊或別的牲畜交給鄰居看管,牲畜死傷或被人搶走,並且無人看見, 11看守的人就要在耶和華面前起誓沒有動鄰居的東西,這樣失主就應當作罷,看守的人不用賠償。 12但若牲畜是被人偷去的,受託人就要賠償失主。 13倘若牲畜被野獸咬死,受託人要把殘骸帶來當證據,無需賠償被咬死的牲畜。 14倘若有人向鄰居借牲畜,牲畜受傷或死掉,而當時物主不在場,借的人就要賠償。 15倘若物主當時在場,借的人就不用賠償。倘若牲畜是租來的,租的人只需付租金不用賠償。

社會條例

16「倘若有人誘姦了尚未許配的處女,他就要交出聘禮,娶她為妻; 17倘若女方家長反對婚事,男方要付出相當於聘禮的金錢給女方家長。

18「凡行邪術的女人,必須被處死。

19「與動物性交的人,必須被處死。

20「祭拜耶和華以外的其他任何神明的人,必須被處死。

21「不可欺壓在你們中間寄居的人,因為你們在埃及也做過寄居的人。

22「不可虧待寡婦和孤兒, 23倘若你們欺凌他們,他們向我呼求,我必聽他們的呼求, 24向你們發怒,用刀殺掉你們,使你們的妻子變為寡婦,兒女成為孤兒。

25「倘若有貧苦的同胞向你借錢,你不可像放債的一樣從中取利。 26倘若他把衣服給你作抵押,你要在日落之前把衣服還給他。 27因為他只有這件蔽體的衣服,若是沒有,他晚上如何睡覺?他若呼求我,我必定幫助他,因為我是仁慈的。 28不可褻瀆上帝,也不可咒詛百姓的官長。 29你們要向我獻上五穀和新酒,不可遲疑耽延。要把你們的長子獻給我。 30也要獻上頭生的牛羊,牠們生下來後可以留在母親身邊七天,第八天要獻給我。 31你們要做我聖潔的子民,不要吃田野間被野獸咬死的牲畜,要把牠丟給狗吃。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 22:1-31

Ulinzi Wa Mali

122:1 Law 6:1-7; 2Sam 12:6; Mit 6:31; Lk 19:8“Kama mtu akiiba maksai au kondoo na kumchinja au kumuuza, ni lazima alipe ngʼombe watano badala ya maksai mmoja na kondoo wanne badala ya kondoo mmoja.

222:2 Ay 24:16; Yer 2:34; Hos 7:1; Mt 6:19-20; 24:43; Hes 35:27; Kut 20:15; Law 19:11; Kum 5:19; Lk 18:20; Rum 13:9; Efe 4:28; 1Pet 4:15“Kama mwizi akishikwa anavunja nyumba akapigwa hata akafa, aliyemuua hana hatia ya kumwaga damu; 322:3 Kut 21:2; Mt 18:25lakini jambo hilo likitokea wakati jua limechomoza, huyo mtu atakuwa na hatia ya kumwaga damu.

“Mwizi huyo sharti alipe, lakini kama hana kitu, lazima auzwe ili alipe kwa ajili ya wizi wake.

422:4 1Sam 12:5; Mwa 43:12; Kut 21:16; Mit 6:31“Kama mnyama aliyeibwa akikutwa hai mikononi mwake, ikiwa ni maksai au punda au kondoo, lazima alipe mara mbili.

5“Kama mtu akichunga mifugo yake katika shamba au shamba la mizabibu, na akawaachia wajilishe katika shamba la mtu mwingine, ni lazima alipe vitu bora kutoka kwenye shamba lake mwenyewe au kutoka shamba lake la mizabibu.

622:6 Amu 15:5“Kama moto ukiwaka na kuenea kwenye vichaka vya miiba na kuteketeza miganda ya nafaka au nafaka ambayo haijavunwa, au kuteketeza shamba lote, mtu yule aliyewasha moto lazima alipe.

722:7 Law 6:2; Mwa 43:12“Kama mtu akimpa jirani yake fedha au mali nyingine amtunzie, na kama vikiibwa kutoka nyumba ya huyo jirani, kama mwizi atashikwa, lazima alipe mara mbili. 822:8 Kut 21:6; Kum 17:8-9Lakini mwizi asipopatikana, mwenye nyumba atafika mbele ya waamuzi ili kuthibitisha kuwa hakuchukua mali ya mwenzake. 922:9 Kum 25:1Pakiwepo jambo lolote la mali isiyo halali, ikiwa ni maksai, punda, kondoo, mavazi, ama mali yoyote iliyopotea ambayo fulani atasema, ‘Hii ni mali yangu,’ pande zote mbili wataleta mashauri yao mbele ya waamuzi. Yule ambaye waamuzi watamwona kuwa na hatia atamlipa jirani yake mara mbili.

10“Kama mtu akimpa jirani yake punda, ngʼombe, kondoo au mnyama mwingine yeyote amtunzie, akifa au akijeruhiwa au akichukuliwa wakati haonekani na mtu yeyote, 1122:11 Law 6:3; 1Fal 8:31; 2Nya 6:22; Ebr 6:16jambo hili kati yao wawili litaamuliwa kwa kuapa kiapo mbele za Bwana, kwamba huyo jirani hakuhusika na wizi wa mali ya jirani yake. Mwenye mali itampasa akubali jambo hili, na hakuna malipo yatakayohitajika. 12Lakini kama mnyama aliibwa kwa jirani, itampasa amlipe mwenye mnyama. 1322:13 Mwa 31:39Kama ameraruliwa na mnyama pori, ataleta mabaki ya mnyama kama ushahidi, naye hatadaiwa kulipa mnyama aliyeraruliwa.

14“Kama mtu akimwazima mnyama kutoka kwa jirani yake, na kama akiumia au akafa na mwenye mnyama hayupo, lazima amlipe huyo mnyama. 1522:15 Law 19:13; Ay 17:5Lakini mwenye mnyama akiwa angalipo na mnyama wake, mwazimaji hatalazimika kumlipa. Kama mnyama alikuwa amekodishwa, fedha iliyolipwa kwa kukodisha inatosha kwa kufidia hasara.

Uwajibikaji Wa Kijamii

1622:16 Kum 22:28; Mwa 34:12“Kama mtu akimshawishi bikira ambaye hajaposwa na akilala naye, lazima alipe mahari, kisha atamwoa msichana huyo. 17Baba wa msichana akikataa katakata kumpa huyo mtu huyo msichana wake, bado ni lazima huyo mtu atalipa mahari kama inavyostahili malipo ya ubikira.

1822:18 Kut 7:11; Law 19:26, 31; 20:27; Kum 18:17; 1Sam 28:3; 2Nya 33:6; Isa 57:3“Usiruhusu mwanamke mchawi aishi.

1922:19 Law 18:23; 20:15; Kum 27:21“Mtu yeyote aziniye na mnyama lazima auawe.

2022:20 Kut 20:23; 22:21“Mtu awaye yote anayemtolea mungu mwingine dhabihu isipokuwa Bwana, lazima aangamizwe.

21“Usimtendee mgeni vibaya au kumwonea, kwa kuwa nanyi mlikuwa wageni huko Misri.

2222:22 Kum 10:18; 24:6, 10-17; Ay 22:6-9; 24:3; 21; Za 68:5; 146:9; Mit 23:10; Isa 1:17; Yer 7:5-6; 21:12; 22:3; Eze 18:5-12; Zek 7:9-10; Mal 3:5; Yak 1:27“Usimdhulumu mjane wala yatima. 2322:23 Lk 18:7; Kum 10:18; 15:9; 24:15; Ay 34:28; 35:9; Za 10:14-17; 12:5; 18:6; Yak 5:4Kama ukifanya hivyo nao wakinililia, hakika nitasikia kilio chao. 2422:24 Za 10:9; 69:24; Mao 5:3Hasira yangu itawaka, nami nitawaua kwa upanga, wake zenu watakuwa wajane na watoto wenu watakuwa yatima.

2522:25 Law 25:35-37; Kum 15:7-11; 23:20; Neh 5:7-10; Za 15:5; Eze 18:8“Kama ukimkopesha mmojawapo wa watu wangu fedha ambaye ni mhitaji, usiwe kama mtu mkopesha fedha; usimtoze riba. 2622:26 Mit 20:16; Eze 33:15; Amo 2:8Kama ukichukua vazi la jirani kama rehani, ulirudishe kwake kabla jua kuzama, 2722:27 Kum 24:13, 17; Ay 22:6; 24:7; 29:11; 31:19-20; Eze 18:12, 16; Kut 34:6; Kum 4:31; 2Nya 30:9; Neh 9:17; Za 99:8; 103:8; 116:5; 145:8; Yoe 2:13; Yon 4:2kwa kuwa vazi lake ndilo pekee alilo nalo la kumfunika mwili wake. Ni nini kingine atajifunika nacho? Atakaponililia, nitasikia, kwa kuwa nina huruma.

2822:28 Kut 20:7; 2Sam 16:5, 9; 1Sam 19:21; 1Fal 21:10; 2Fal 2:23; Za 102; 8; Mhu 10:20; Mdo 23:5“Usimkufuru Mungu au kumlaani mtawala wa watu wako.

2922:29 Kut 23:15-19; 34:20-26; Law 19:24; 23:10; Hes 18:13; 28:26; Kum 18:4; 26:2, 10; 1Sam 6:3; Neh 10:35; Mit 3:9; Mal 3:10; Kut 13:2; Hes 8:16-17; Lk 2:23“Usiache kutoa sadaka kutoka ghala lako au mapipa yako.

“Lazima unipe mzaliwa wa kwanza wa wana wako. 3022:30 Kut 34:19; Kum 15:19; Law 12:3; 22:27; Mwa 17:12Ufanye vivyo hivyo kwa ngʼombe wako na kwa kondoo wako. Waache wakae na mama zao kwa siku saba, lakini siku ya nane unipe.

3122:31 Kut 19:6; Law 19:2; 22:31; Ezr 9:2; Law 7:24; 17:15; 22:8; Kum 14:21; Eze 4:14; 44:31“Ninyi mtakuwa watu wangu watakatifu. Kwa hiyo msile nyama ya mnyama aliyeraruliwa na wanyama pori; mtupieni mbwa.