出埃及記 13 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

出埃及記 13:1-22

奉獻頭胎

1耶和華對摩西說: 2以色列人中的長子和頭生的牲畜都屬於我,因此要把他們分別出來,使他們聖潔,歸給我。」

3摩西對百姓說:「你們要記住離開埃及的這一天,因為耶和華用大能的手把你們從受奴役的地方解救出來。不可吃帶酵的食物。 4你們是在亞筆月13·4 亞筆月是猶太曆的第一個月,約在陽曆三月中旬到四月中旬,相當於中國的春分時節。的這一天從埃及出來的, 5將來耶和華帶領你們進入迦南以後,你們每逢此月都要為祂守節期。那裡現在住著迦南人、人、亞摩利人、希未人和耶布斯人。耶和華已經向你們祖先起誓,應許賜給你們那奶蜜之鄉。 6在節期的七天之內,你們只可以吃無酵餅,到了第七天,你們要為耶和華守節期。 7七天之內要吃無酵餅,你們境內不得有酵或是帶酵的東西。 8那時,要告訴你們的子孫,『這節期是紀念我們離開埃及時耶和華為我們所做的一切。』 9這節期就好像在你們手上或額上作的記號,叫你們記得耶和華的律法,祂曾經用大能的手把你們帶出埃及10因此,每一年你們都要按時守這節期。

11「將來耶和華成就祂起誓給你們祖先的應許,領你們進入迦南人的土地,把那裡賜給你們以後, 12你們要把所有長子和頭生的公畜歸給祂。 13所有頭生的公驢必須用羊羔贖回,不然就要打斷牠的脖子。要贖回你們所有的長子。 14將來你們的子孫問起這件事的意義,你們就回答,『耶和華曾經用大能的手把我們從受奴役之地——埃及領出來。 15當時法老硬著心不肯放我們走,所以耶和華就把埃及人的長子和頭生的牲畜全都殺了。因此,我們把所有頭生的公畜當作祭牲獻給耶和華,只把長子贖回來。』 16這事就像在你們手上作記號,額上作標記,以牢記耶和華曾用大能的手領我們離開埃及。」

雲柱和火柱

17法老讓以色列人離開埃及後,上帝沒有帶領他們穿越非利士地區,雖然那是條捷徑。因為上帝說:「如果他們遇上戰爭,就會改變主意,返回埃及。」 18所以,上帝領他們繞道而行,走曠野的路,前往紅海13·18 紅海」或譯「蘆葦湖」,確切地點約在今紅海北端蘇伊士運河附近。以色列人離開埃及時都帶著兵器。 19摩西約瑟的骸骨一起帶走,因為約瑟曾叫以色列人鄭重發誓,對他們說:「上帝必眷顧你們,把你們帶出埃及,那時你們要把我的骸骨也一起帶走。」 20以色列人從疏割啟程,來到曠野邊緣的以倘安營。 21耶和華走在他們前面,白天用雲柱為他們指示道路,晚上用火柱照亮他們,這樣他們可以日夜趕路。 22白天的雲柱和晚上的火柱從不離開他們。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 13:1-22

Kuwekwa Wakfu Kwa Wazaliwa Wa Kwanza

1Bwana akamwambia Mose, 213:2 Kut 22:29; 34:20; Law 27:26; Hes 3:13; 8:17; 18:15; Kum 15:19; Neh 10:34; Lk 2:23“Niwekeeni wakfu kila mzaliwa wa kwanza wa kiume. Kila mtoto wa kwanza aliye kifungua tumbo miongoni mwa Waisraeli ni mali yangu, akiwa wa mwanadamu au wa mnyama.”

313:3 Kut 7:4; Law 26:13; Hes 22:5; 26:4; Kum 4:45; 5:6; Za 81:10; 114:1; Kut 3:20; 12:8Ndipo Mose akawaambia watu, “Ikumbukeni siku hii, siku ambayo mlitoka katika nchi ya Misri, katika nchi ya utumwa, kwa sababu Bwana aliwatoa humo kwa mkono wenye nguvu. Msile chochote kilichotiwa chachu. 413:4 Kut 12:2Leo, katika mwezi wa Abibu,13:4 Abibu ni jina la mwezi wa kwanza kwa Wayahudi, ambao ni mwezi wa nne katika kalenda yetu. mnatoka. 513:5 Kut 3:8; 12:25-26Bwana atakapokuleta katika nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Wahivi na Wayebusi, nchi aliyowaapia baba zako kukupa, nchi itiririkayo maziwa na asali, utaiadhimisha sikukuu hii katika mwezi huu: 613:6 Kut 12:15-20Kwa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu na katika siku ya saba utamfanyia Bwana sikukuu. 7Kwa muda wa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu, pasionekane kitu chochote kilicho na chachu miongoni mwako, wala chachu yoyote isionekane popote ndani ya mipaka yako. 813:8 Kut 10:2; Za 78:5-6Siku ile utamwambia mwanao, ‘Nafanya hivi kwa sababu ya jambo ambalo Bwana alinitendea nilipotoka katika nchi ya Misri.’ 913:9 Isa 44:5; Kum 6:8; 11:18; Mit 3:3; Mt 23:5; Kut 3:20Adhimisho hili, litakuwa kama alama kwenye mkono wako na ukumbusho katika paji lako la uso, kwamba sheria ya Bwana inapaswa iwe kinywani mwako. Kwa kuwa Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu. 1013:10 Kut 12:14; Za 75:2; 102:13Ni lazima uishike amri hii kwa wakati uliopangwa mwaka baada ya mwaka.

1113:11 Mwa 22:16; Kum 1:8; Mwa 12:7; 17:19; Za 105:42-45“Baada ya Bwana kukuingiza katika nchi ya Wakanaani na kukupa nchi hiyo, kama alivyokuahidi kwa kiapo na kwa baba zako, 1213:12 Mwa 4:4; Law 27:26; Hes 3:13; 18:15-17; Lk 2:23inakupasa kumtolea Bwana mzaliwa wa kwanza wa kila tumbo. Wazaliwa wote wa kwanza wa kiume wa mifugo yako ni mali ya Bwana. 1313:13 Law 27:11; Kut 34:20; Isa 66:3; Hes 3:46-47; 18:15Kila mzaliwa wa kwanza wa punda utamkomboa kwa mwana-kondoo, lakini kama hukumkomboa, utamvunja shingo yake. Kila mzaliwa wa kwanza mwanaume miongoni mwa wana wenu utamkomboa.

1413:14 Kut 10:2; 20:2; Kum 7:8; 6:20; 28:68“Katika siku zijazo, mwanao akikuuliza, ‘Hii ina maana gani?’ Mwambie, ‘Kwa mkono wenye nguvu Bwana alitutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa. 15Farao alipokataa kwa ukaidi kuturuhusu kuondoka, Bwana aliua kila mzaliwa wa kwanza wa Wamisri, mwanadamu na wa mnyama. Hii ndiyo sababu ninatoa dhabihu kwa Bwana mzaliwa wa kwanza wa kiume, wa kila tumbo na kumkomboa kila mzaliwa wa kwanza wa wana wangu.’ 16Jambo hili litakuwa kama ishara kwenye mkono wako na kama alama kwenye paji la uso wako, kwamba Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu.”

Nguzo Ya Wingu Na Moto

1713:17 Kut 14:11; Hes 14:1-4; Kum 17:16; Hos 11:5Farao alipowaachia watu waende, Mungu hakuwaongoza kufuata njia ipitiayo katika nchi ya Wafilisti, ingawa njia hiyo ilikuwa fupi zaidi. Kwa maana Mungu alisema, “Wakikabiliana na vita, wanaweza kubadili mawazo yao na kurudi Misri.” 1813:18 Kut 15:22; Za 136:16; Eze 20:10; Yos 4:13Kwa hiyo Mungu akawaongoza watu kupitia njia ya kuzunguka kupitia jangwani, kuelekea Bahari ya Shamu. Waisraeli walipanda kutoka nchi ya Misri wakiwa wamejiandaa kwa vita.

1913:19 Yos 24:32; Mdo 7:16; Ebr 11:22; Mwa 47:29-30Mose akachukua mifupa ya Yosefu kwa sababu Yosefu alikuwa amewaapisha wana wa Israeli. Alikuwa amewaambia, “Hakika Mungu atakuja kuwasaidia, nanyi ni lazima mwiichukue mifupa yangu mwende nayo kutoka mahali hapa.”

2013:20 Kut 12:37; Hes 33:6Baada ya Waisraeli kuondoka Sukothi wakapiga kambi huko Ethamu pembeni mwa jangwa. 2113:21 Kut 32:1; 33:14; Kum 2:7; 31:8; Amu 4:14; 5:4; Za 68:7; 72:20; Yer 2:2; Hab 3:13; Kut 14:19, 24; 24:16; 33:9-10; 34:5; 40:38; Hes 9:16; 12:5; 14:14; Kum 1:33; Neh 9:12, 19; Za 78:14; 99:7; 105:39; Isa 4:5; 1Kor 10:1Wakati wa mchana Bwana aliwatangulia kwa nguzo ya wingu kuwaongoza katika njia yao, na wakati wa usiku aliwatangulia kwa nguzo ya moto kuwaangazia, ili waweze kusafiri mchana au usiku. 2213:22 Neh 9:19; Hes 33:7; Yer 44:1; Eze 29:10Ile nguzo ya wingu wakati wa mchana au ile nguzo ya moto wakati wa usiku haikuondoka mahali pake mbele ya watu.