傳道書 11 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

傳道書 11:1-10

1當慷慨施捨11·1 當慷慨施捨」或譯「當把你的資財投入海外貿易」。

因為日後必有收穫。

2當把你的資財分給多人,

因為你不知道日後會有什麼災難臨到世上。

3雲中滿了水,就會下雨。

樹不論倒向南或倒向北,

倒在哪裡就躺在哪裡。

4你若等待完美的天氣,

必無法撒種,無法收割。

5正如你不知道風的路線,不知道骨骼在母胎中如何形成,你也無法瞭解創造萬物之上帝的作為。 6你要早晚不停地撒種,因為你不知道什麼時候撒的種子會發芽生長,或許所撒的都會帶來收穫。 7光真美好,能夠看見陽光真好! 8人一生不論活多久,都要活得快樂,但不要忘記死後有許多黑暗的日子。將來的一切都是虛空。 9年輕人啊,在年輕時要快樂,要在青春歲月裡使自己的心歡暢。心裡想做什麼就去做,眼睛想看什麼就去看。然而,要切記:上帝必照你所行的一切審判你。 10所以,你要拋開心中的煩惱和肉體的痛苦,因為青春年華轉瞬即逝。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mhubiri 11:1-10

Mkate Juu Ya Maji

111:1 Kum 15:10; 24:19; Hos 10:12; Mt 10:42; Isa 32:20; Mit 19:17Tupa mkate wako juu ya maji,

kwa maana baada ya siku nyingi

utaupata tena.

211:2 Mik 5:5; Efe 5:16; Za 112:9Wape sehemu watu saba, naam hata wanane,

kwa maana hujui ni baa gani

litakalokuwa juu ya nchi.

3Kama mawingu yamejaa maji,

hunyesha mvua juu ya nchi.

Kama mti ukianguka kuelekea kusini

au kuelekea kaskazini,

mahali ulipoangukia,

hapo ndipo utakapolala.

4Yeyote atazamaye upepo hatapanda,

yeyote aangaliaye mawingu hatavuna.

511:5 Za 139:14-16; Yn 3:8-10Kama vile usivyofahamu njia ya upepo,

au jinsi mwili uumbwavyo

ndani ya tumbo la mama,

vivyo hivyo huwezi kufahamu kazi ya Mungu,

Muumba wa vitu vyote.

611:6 Mhu 9:10Panda mbegu yako asubuhi,

nako jioni usiruhusu mikono yako ilegee,

kwa maana hujui ni ipi itakayofanikiwa,

kwamba ni hii au ni ile,

au kwamba zote zitafanikiwa sawasawa.

Mkumbuke Muumba Wako Ukiwa Bado Kijana

711:7 Mhu 7:11Nuru ni tamu,

tena inafurahisha macho kuona jua.

8Hata kama mtu ataishi miaka mingi kiasi gani,

na aifurahie yote.

Lakini na akumbuke siku za giza,

kwa maana zitakuwa nyingi.

Kila kitu kitakachokuja ni ubatili.

911:9 Ay 19:29; Kum 29:19; Mdo 14:16; Rum 14:10; Mhu 2:24; 3:17Furahi ewe kijana, wakati ungali kijana,

moyo wako na ukupe furaha

katika siku za ujana wako.

Fuata njia za moyo wako

na chochote macho yako yaonayo,

lakini ujue kwamba kwa ajili ya haya yote

Mungu atakuleta hukumuni.

1011:10 2Kor 7:1; Za 94:19; Mhu 2:24Kwa hiyo basi, ondoa wasiwasi moyoni mwako

na utupilie mbali masumbufu ya mwili wako,

kwa kuwa ujana na nguvu ni ubatili.