使徒行傳 3 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

使徒行傳 3:1-26

彼得醫治瘸腿的乞丐

1一天,在下午三點禱告的時間,彼得約翰去聖殿。 2有一個生來瘸腿的人天天被人抬到聖殿美門的外面,向進殿的人乞討。 3他看見彼得約翰要進殿,就求他們施捨。 4二人定睛看他,彼得說:「看著我們!」 5那人就緊盯著他們,期盼能有所收穫。

6彼得說:「金子、銀子我都沒有,但是我把我有的給你。我奉拿撒勒人耶穌基督的名,命令你起來行走!」

7彼得拉著他的右手扶他起來,那人的腳和踝骨立刻變得強健有力。 8他跳了起來,站穩後開始行走,跟著彼得約翰進入聖殿,走著跳著讚美上帝。 9大家看見他一邊走一邊讚美上帝, 10認出他就是那個在美門外面的乞丐,都為發生在他身上的事而感到驚奇、詫異。 11那乞丐緊緊拉著彼得約翰的手走到所羅門廊,眾人都跑過來,嘖嘖稱奇。

彼得傳揚基督

12彼得看見這情形,就對大家說:「以色列人啊,何必驚奇呢?為什麼一直盯著我們呢?你們以為我們是憑自己的能力和虔誠叫這人行走嗎? 13亞伯拉罕以撒雅各的上帝,就是我們祖先的上帝,已經使祂的僕人耶穌得了榮耀。你們把耶穌交給彼拉多,儘管彼拉多想釋放祂,你們卻在彼拉多面前棄絕祂! 14你們棄絕了那聖潔公義者,竟然要求彼拉多釋放一個兇手。 15你們殺了生命之主,上帝卻使祂從死裡復活了。我們都是這事的見證人。 16你們認識的這個乞丐因為相信耶穌的名,得到了醫治。你們都看見了,他能痊癒是因為他信耶穌。

17「弟兄們,我知道你們的所作所為是出於無知,你們的官長也是一樣。 18但是上帝早已藉眾先知預言基督要受害,這事果然應驗了。 19所以你們要悔改,歸向上帝,祂將除去你們一切的罪惡, 20賜給你們煥然一新的日子,也將差遣祂預先為你們選立的基督耶穌降臨。 21基督必須留在天上,直到萬物更新的時候,這是上帝自古以來藉聖先知的口說的。 22摩西曾經說,『主——你們的上帝將要在你們中間興起一位像我一樣的先知。你們要留心聽祂的話, 23凡不聽的,必將他從民中剷除。』

24「從撒母耳到後來的所有先知都宣告過這些日子。 25你們是先知的子孫,也承受了上帝和你們祖先所立的約。上帝曾對亞伯拉罕說,『天下萬族必因你的後裔而蒙福。』 26上帝興起祂的僕人,首先差遣祂到你們中間賜福給你們,使你們脫離罪惡。」

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Matendo 3:1-26

Petro Amponya Mlemavu Kwa Jina La Yesu

13:1 Lk 22:8; Mdo 2:46; Za 55:17; Mdo 10:30Siku moja Petro na Yohana walikuwa wanapanda kwenda Hekaluni kusali yapata saa tisa alasiri. 23:2 Mdo 14:8; Lk 16:20; Yn 9:8Basi palikuwa na mtu mmoja aliyekuwa kiwete tangu kuzaliwa. Alichukuliwa na kuwekwa kwenye lango la Hekalu liitwalo Zuri, kila siku ili aombe msaada kwa watu wanaoingia Hekaluni. 3Huyu mtu alipowaona Petro na Yohana wakikaribia kuingia Hekaluni, akawaomba wampe sadaka. 43:4 Mdo 14:9Wakamkazia macho, kisha Petro akamwambia, “Tutazame sisi.” 5Hivyo yule mtu akawatazama, akitazamia kupata kitu kutoka kwao.

63:6 Mk 1:24; Mdo 14:10Ndipo Petro akamwambia, “Sina fedha wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, tembea!” 7Petro akamshika yule mtu kwa mkono wa kuume akamwinua, mara nyayo zake na vifundo vya miguu yake vikapata nguvu. 83:8 Isa 35:6; Mdo 14:10Akaruka juu na kusimama, akaanza kutembea. Kisha akaingia Hekaluni pamoja na Petro na Yohana, huku akitembea na kurukaruka na kumsifu Mungu. 93:9 Mdo 4:16, 21Watu wote walipomwona akitembea na kumsifu Mungu, 103:10 Mdo 3:2; Yn 9:8wakamtambua kuwa ni yule mtu aliyekuwa akiketi nje ya Hekalu penye lango liitwalo Zuri akiomba msaada, nao wakajawa na mshangao, wakastaajabu juu ya yale yaliyomtukia.

Petro Anashuhudia Kuwa Yesu Anaponya

113:11 Lk 22:8; Yn 10:23; Mdo 5:12Aliyeponywa alipokuwa akiambatana na Petro na Yohana, watu wote walishangaa mno, wakaja wakiwakimbilia pale ukumbi wa Solomoni. 12Petro alipoona watu wamekusanyika akawaambia, “Enyi Waisraeli, kwa nini mnastaajabu kuhusu jambo hili? Mbona mnatukazia macho kwa mshangao kana kwamba ni kwa uwezo wetu au utakatifu wetu tumemfanya mtu huyu kutembea? 133:13 Mdo 7:32; 22:14; Mt 27; 2; Lk 23:4Mungu wa Abrahamu na Isaki na Yakobo, Mungu wa baba zetu amemtukuza Mwanawe Yesu, ambaye ninyi mlimtoa ahukumiwe kifo na mkamkana mbele ya Pilato, ingawa yeye alikuwa ameamua kumwachia aende zake. 143:14 Mdo 4:27; 7:52; Mk 15:11; Lk 23:18-25Ninyi mlimkataa huyo Mtakatifu na Mwenye Haki mkaomba mpewe yule muuaji. 153:15 Mdo 2:24; 2:32Hivyo mkamuua aliye chanzo cha uzima, lakini Mungu akamfufua kutoka kwa wafu. Sisi tu mashahidi wa mambo haya. 163:16 Mt 9:22; Mdo 4:10; 14:9Kwa imani katika jina la Yesu, huyu mtu mnayemwona na kumfahamu ametiwa nguvu. Ni kwa jina la Yesu na imani itokayo kwake ambayo imemponya kabisa huyu mtu, kama ninyi wote mnavyoona.

173:17 Lk 23:34; Mdo 13:27“Sasa ndugu zangu, najua ya kuwa ninyi mlitenda bila kujua, kama walivyofanya viongozi wenu. 183:18 Mdo 17:2-3; Lk 24:27; Mdo 26:22-27Lakini kwa njia hii Mungu alitimiza kile ambacho alikuwa ametabiri kwa vinywa vya manabii wake wote, kwamba Kristo3:18 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. atateswa. 193:19 Za 5:11; Mdo 2:38Tubuni basi mkamgeukie Mungu, dhambi zenu zifutwe, ili zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwepo kwake Bwana, 203:20 Lk 2:11naye apate kumtuma Kristo, ambaye ameteuliwa kwa ajili yenu, yaani Yesu. 213:21 Mdo 1:11; Mt 17:11; Lk 1:70Ilimpasa mbingu zimpokee mpaka wakati wa kufanywa upya kila kitu, kama Mungu alivyoahidi zamani kupitia kwa vinywa vya manabii wake watakatifu. 223:22 Kum 18:15-18; Mdo 7:37Kwa maana Mose alisema, ‘Bwana Mungu wenu atawainulia nabii kama mimi kutoka miongoni mwa ndugu zenu. Itawapasa kumtii huyo kwa kila jambo atakalowaambia. 233:23 Kum 18:19; Law 23:29Mtu yeyote ambaye hatamsikiliza huyo nabii, atatupiliwa mbali kabisa na watu wake.’

243:24 Lk 24:27“Naam, manabii wote tangu Samweli na waliokuja baada yake, wote walitabiri kuhusu siku hizi. 253:25 Mdo 2:39; Rum 9:4-5; Mwa 22:18; 28:14Ninyi ndio wana wa manabii na wa Agano ambalo Mungu alifanya na baba zenu, akimwambia Abrahamu, ‘Kupitia kwa uzao wako, watu wote wa ulimwengu watabarikiwa.’ 263:26 Mdo 2:24; 13:46; Rum 1:16Mungu alipomfufua Yesu Mwanawe, alimtuma kwenu kwanza, ili awabariki kwa kumgeuza kila mmoja wenu kutoka njia yake mbaya.”