使徒行傳 28 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

使徒行傳 28:1-31

在馬爾他島

1我們安全上岸後,才知道那個島的名字叫馬爾他2島上的居民對我們非常友善。因為下雨,天氣又冷,他們就生火接待我們。 3保羅拿起一捆柴放進火堆裡,不料有一條毒蛇經不住熱鑽了出來,咬住了他的手。 4那裡的居民看見毒蛇吊在保羅手上,就交頭接耳地說:「這人一定是個兇手,雖然僥倖沒有淹死,天理卻不容他活下去。」 5可是保羅把蛇甩進火裡,並沒有受傷。 6他們以為保羅的手一定會腫起來或者他會突然倒斃,但是等了很久,見他還是安然無恙,就改變了態度,說他是個神明。

7那個島的首領名叫部百流,他的田產就在附近。他接待我們,熱情款待了我們三天。 8當時,部百流的父親患痢疾,正發熱躺在床上。保羅去為他禱告,把手按在他身上治好了他。 9這事以後,島上其他的病人都來了,他們都得了醫治。 10他們處處尊敬我們,在我們啟航的時候,又贈送我們途中所需用的物品。

保羅抵達羅馬

11三個月後,我們搭乘一艘停在該島過冬的船離開。這船叫「雙神號」,來自亞歷山大12我們先到敘拉古港,在那裡停泊三天, 13然後繼續前行,到達利基翁。第二天,起了南風,第三天我們抵達部丟利14在那裡遇見幾位弟兄姊妹,應邀和他們同住了七天,然後前往羅馬15那裡的弟兄姊妹聽說我們來了,便到亞比烏三館迎接我們。保羅見到他們後,就感謝上帝,心中受到鼓勵。 16進了羅馬城後,保羅獲准在衛兵的看守下自己一個人住。

繼續傳道

17三天後,保羅請來當地猶太人的首領,對他們說:「弟兄們,雖然我沒有做過任何對不起同胞或違背祖先規矩的事,卻在耶路撒冷遭囚禁,又被交到羅馬人的手裡。 18羅馬官員審訊了我,發現我沒有什麼該死的罪,想釋放我, 19猶太人卻反對,我不得已只好上訴凱撒。我並非有什麼事要控告自己的同胞。 20為此,我才請你們來當面談,我受捆綁是為了以色列人所盼望的那位。」

21他們說:「猶太境內的同胞沒有給我們寫信提及你的事,也沒有弟兄到這裡說你的壞話。 22不過,我們倒很想聽聽你的觀點,因為我們知道你們這一派的人到處受人抨擊。」

23於是,他們和保羅約定了會面的日期。那一天,很多人來到保羅住的地方。從早到晚,保羅向他們傳揚上帝國的道,引用摩西律法和先知書勸他們相信有關耶穌的事。 24有些人聽後相信了他的話,有些人不相信, 25他們彼此意見不一。在他們散去之前,保羅說了一句話:「聖靈藉以賽亞先知對你們祖先所說的話真是一點不錯, 26祂說,

『你去告訴百姓,

你們聽了又聽,卻不明白;

看了又看,卻不領悟。

27因為這百姓心靈麻木,

耳朵發背,眼睛昏花,

以致眼睛看不見,

耳朵聽不見,心裡不明白,無法回心轉意,

得不到我的醫治。』

28所以你們當知道,上帝的救恩已經傳給了外族人,他們也必聽。」

29聽完保羅的話後,那些猶太人就回去了,他們中間起了激烈的爭論。28·29 有古卷無「聽完保羅的話後,那些猶太人就回去了,他們中間起了激烈的爭論。」

30後來,保羅租了一間房子,在那裡住了整整兩年,接待所有到訪的人。 31他勇敢地傳講上帝的國,教導有關主耶穌基督的事,沒有受到任何攔阻。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Matendo 28:1-31

Paulo Kisiwani Malta

128:1 Mdo 16:10; 27:26, 39Baada ya kufika nchi kavu salama, ndipo tukafahamu kwamba jina la kile kisiwa ni Malta. 228:2 Mdo 27:3; 2Kor 11:27Wenyeji wa kile kisiwa wakatufanyia ukarimu usio wa kawaida. Waliwasha moto na kutukaribisha sisi sote kwa sababu mvua ilikuwa inanyesha na kulikuwa na baridi. 3Paulo alikuwa amekusanya mzigo wa kuni na alipokuwa anaweka kwenye moto kwa ajili ya joto, nyoka mwenye sumu akatoka humo na kujisokotea mkononi mwake. 428:4 Mk 16:18; Lk 13:2, 4Wale wenyeji wa kile kisiwa walipomwona yule nyoka akiningʼinia mkononi mwa Paulo, wakaambiana, “Huyu mtu lazima awe ni muuaji, ingawa ameokoka kutoka baharini, haki haijamwacha aishi.” 528:5 Lk 10:19Lakini Paulo akamkungʼutia yule nyoka ndani ya moto wala yeye hakupata madhara yoyote. 628:6 Mdo 14:11Watu walikuwa wanangoja avimbe au aanguke ghafula na kufa. Lakini baada ya kungoja kwa muda mrefu na kuona kwamba hakuna chochote kisicho cha kawaida kilichomtokea, wakabadili mawazo yao na kuanza kusema kwamba yeye ni mungu.

7Basi karibu na sehemu ile, palikuwa na shamba kubwa la mtu mmoja kiongozi wa kile kisiwa, aliyeitwa Publio. Alitupokea na akatuhudumia kwa ukarimu mkubwa kwa muda wa siku tatu. 828:8 Yak 5:14, 15; Mdo 9:40Baba yake Publio alikuwa mgonjwa kitandani, akiwa anaumwa homa na kuhara damu. Paulo akaingia ndani ili kumwona na baada ya maombi, akaweka mikono juu yake na kumponya. 9Jambo hili lilipotukia, watu wote wa kisiwa kile waliokuwa wagonjwa wakaja, nao wakaponywa. 1028:10 Mt 15:6; 1Tim 5:17; Za 15:4Wakatupa heshima nyingi, nasi tulipokuwa tayari kusafiri kwa njia ya bahari, wakapakia melini vitu vyote tulivyokuwa tunavihitaji.

Paulo Awasili Rumi

1128:11 Mdo 27:6Miezi mitatu baadaye tukaanza safari kwa meli iliyokuwa imetia nanga kwenye kisiwa hicho kwa ajili ya majira ya baridi. Hii ilikuwa meli ya Iskanderia yenye alama ya miungu pacha waitwao Kasta na Poluksi. 12Kituo chetu cha kwanza kilikuwa Sirakusa na tukakaa huko siku tatu. 13Kisha tukangʼoa nanga, tukafika Regio. Siku iliyofuata, upepo mkali wa kusi ukavuma, na siku ya pili yake tukafika Puteoli. 1428:14 Mdo 1:16Huko tukawakuta ndugu, nasi tukakaribishwa tukae nao kwa siku saba. Hivyo tukaendelea na safari mpaka Rumi. 1528:15 Mdo 1:16Ndugu wa huko Rumi waliposikia habari zetu, walikuja mpaka Soko la Apio na mahali paitwapo Mikahawa Mitatu kutulaki. Paulo alipowaona, alimshukuru Mungu akatiwa moyo. 1628:16 Mdo 24:23; 27:3Tulipofika Rumi, Paulo aliruhusiwa kuishi peke yake akiwa na askari wa kumlinda.

Paulo Ahubiri Rumi Chini Ya Ulinzi

1728:17 Mdo 25:2; 22:5; 25:8; 6:14Siku tatu baadaye Paulo akawaita pamoja viongozi wa Kiyahudi. Walipokwisha kukusanyika akawaambia, “Ndugu zangu, ingawa sikufanya jambo lolote dhidi ya watu wetu au dhidi ya desturi za baba zetu, lakini nilikamatwa huko Yerusalemu nikakabidhiwa kwa Warumi. 1828:18 Mdo 22:24; 26:31, 32; 23:9Wao walipokwisha kunihoji, wakataka kuniachia huru kwa sababu hawakuona kosa lolote nililolifanya linalostahili adhabu ya kifo. 1928:19 Mdo 25:11; 26:32Lakini Wayahudi walipopinga uamuzi huo, nililazimika kukata rufaa kwa Kaisari, ingawa sikuwa na lalamiko lolote juu ya taifa langu. 2028:20 Mdo 26:6, 7; 21:33Basi hii ndiyo sababu nimewatumania, ili niseme nanyi. Kwa kuwa ni kwa ajili ya tumaini la Israeli nimefungwa kwa minyororo.”

2128:21 Mdo 22:5Wakamjibu, “Hatujapokea barua zozote kutoka Uyahudi zinazokuhusu, wala hapana ndugu yeyote aliyekuja hapa ambaye ametoa taarifa au kuzungumza jambo lolote baya juu yako. 2228:22 Mdo 24:5, 14Lakini tungependa kusikia kutoka kwako unalofikiri kwa sababu tunajua kwamba kila mahali watu wanazungumza mabaya kuhusu jamii hii.”

2328:23 Mt 3:2; Mdo 19:8; 17:3; 8:35Baada ya kupanga siku ya kuonana naye, watu wengi wakaja kuanzia asubuhi hadi jioni akawaeleza na kutangaza kuhusu Ufalme wa Mungu akijaribu kuwahadithia juu ya Yesu kutoka Sheria ya Mose na kutoka Manabii. 2428:24 Mdo 14:4Baadhi wakasadiki yale aliyosema, lakini wengine hawakuamini. 25Hivyo hawakukubaliana, nao walipokuwa wanaondoka, Paulo akatoa kauli moja zaidi: “Roho Mtakatifu alinena kweli na baba zenu aliposema mambo yale yaliyomhusu Bwana Yesu kwa kinywa cha nabii Isaya kwamba:

2628:26 Isa 6:9; Yer 5:21; Eze 12:2; Mt 13:14, 15; Mk 4:12; Lk 8:10; Yn 12:40; Rum 11:8“ ‘Nenda kwa watu hawa na useme,

“Hakika mtasikiliza lakini hamtaelewa;

na pia mtatazama, lakini hamtaona.”

2728:27 Za 119:70; Isa 6:9, 10Kwa kuwa mioyo ya watu hawa imekuwa migumu;

hawasikii kwa masikio yao,

na wamefumba macho yao.

Wasije wakaona kwa macho yao,

na wakasikiliza kwa masikio yao,

wakaelewa kwa mioyo yao,

na kugeuka nami nikawaponya.’

2828:28 Lk 2:30; Mdo 13:46“Basi na ijulikane kwenu kwamba, huu wokovu wa Mungu umepelekwa kwa watu wa Mataifa, nao watasikiliza.” [ 29Naye akiisha kusema maneno haya, Wayahudi wakaondoka wakiwa na hoja nyingi miongoni mwao.]

30Kwa miaka miwili mizima Paulo alikaa huko kwa nyumba aliyokuwa amepanga. Akawakaribisha wote waliokwenda kumwona. 3128:31 Mdo 4:29; Mt 4:23; Mdo 4:29; 28:23; Mt 4:23; Mdo 4:23; 4:23; 4:31; Efe 6:19Akahubiri Ufalme wa Mungu na kufundisha mambo yale yaliyomhusu Bwana Yesu Kristo, kwa ujasiri wote na bila kizuizi chochote.