但以理書 5 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

但以理書 5:1-31

牆上寫字

1伯沙撒王盛宴款待一千大臣,與他們一同飲酒。 2王暢飲的時候,命人將先王尼布甲尼撒耶路撒冷聖殿中擄來的金銀器皿拿來,供他與大臣、王后和妃嬪用來飲酒。 3於是,他們把從耶路撒冷上帝殿中擄來的金器拿來,王與大臣、王后和妃嬪便用這些器皿飲酒。 4他們一邊飲酒,一邊頌讚金、銀、銅、鐵、木、石所造的神明。

5突然,有人手的指頭出現,在燈臺對面王宮的粉牆上寫字。王看見那隻手在寫字, 6臉色驟變,驚恐萬分,兩腿發軟,雙膝顫抖。 7他大聲傳令,召來巫師、占星家和占卜者,對這些巴比倫的智者說:「誰能讀牆上的字,把意思告訴我,他必身穿紫袍,頸戴金鏈,在國中位居第三。」 8王所有的智者進來後,竟無人能讀懂或把意思告訴王。 9伯沙撒王愈發恐懼,臉色蒼白,他的大臣都不知所措。

10太后聽到王和大臣的喊聲,便來到宴會廳,對王說:「願王萬歲!不要驚慌失色。 11你國中有一個人,他有聖潔神明的靈。先王在世時,曾發現他有神明一樣的灼見、悟性和智慧。先王尼布甲尼撒立他為術士、巫師、占星家和占卜者的首領。 12他有非凡的心智、知識和悟性,能解夢、釋謎、解惑。他叫但以理,先王給他取名叫伯提沙撒。現在可以把他召來,他必能解釋這些字的意思。」

13於是,但以理被帶到王面前。王問他:「你就是先王從猶大擄來的但以理嗎? 14我聽說你有神明的靈,有灼見、悟性和非凡的智慧。 15我召智者和巫師來讀這些字,為我解釋字的意思,但他們都不能解釋。 16我聽說你能釋夢、解惑。你若能讀出牆上的字,把意思告訴我,你必身穿紫袍、頸戴金鏈,在我的國中位居第三。」

17但以理回答說:「你的禮物自己留著,你的賞賜可以給別人,不過我會為你讀這些字,解釋意思。 18王啊,至高的上帝曾將國位、權力、尊榮、威嚴賜給你的先王尼布甲尼撒19因為他有上帝所賜的大權,各族、各邦、各語種的人都在他面前戰抖,充滿恐懼。他操生殺大權,可隨意擢升、罷黜。 20但他變得心高氣傲、剛愎自用、狂妄自大,因而被革除王位、剝去尊榮。 21他從人群中被趕走,他的心變成獸心,他與野驢同住,像牛一樣吃草,被天上的露水浸濕,直到他知道至高的上帝主宰世上萬國,祂要把國賜給誰就賜給誰。

22伯沙撒啊,你是他的後裔,你雖然知道這一切事,仍不謙卑, 23竟在天上的主面前自大,命人拿來祂殿裡的器皿,供你和大臣、王后、妃嬪用來飲酒,並頌讚不能看、不能聽、一無所知、用金、銀、銅、鐵、木、石所造的神明,卻不尊崇賜你生命氣息、掌管你一舉一動的上帝。

24「因此,上帝使指頭出現,寫下這些字, 25就是『彌尼,彌尼,提客勒,烏法珥新』。 26這些字的意思是這樣,彌尼——指上帝已經數算你國度的年日,使之到此為止; 27提客勒——指你已經被放在秤上稱了,發現分量不夠; 28烏法珥新5·28 烏法珥新」亞蘭文是「毗勒斯」,即「烏法珥新」的單數格式。——指你的國要分裂,歸給瑪代人和波斯人。」

29於是,伯沙撒下令給但以理穿上紫袍,戴上金項鏈,又宣告他在國中位居第三。 30當夜,迦勒底伯沙撒被殺。 31瑪代大流士六十二歲時奪取了王權。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Danieli 5:1-31

Maandishi Ukutani

15:1 1Fal 3:15; Mk 6:21; Es 3:1; Yer 50:35; Dan 7:1; 8:1Mfalme Belshaza alifanya karamu kubwa kwa ajili ya maelfu ya wakuu wake na akanywa mvinyo pamoja nao. 25:2 2Nya 36:10; Yer 52:19; Es 1:7; Mit 20:1; Isa 21:5; 2Fal 24:13; Es 2:14; Dan 1:2Wakati Belshaza alipokuwa akinywa mvinyo wake, aliamuru viletwe vile vikombe vya dhahabu na fedha ambavyo Nebukadneza baba yake alikuwa amevichukua kutoka hekaluni huko Yerusalemu, ili mfalme na wakuu wake, wake zake na masuria wake waweze kuvinywea. 3Kwa hiyo wakavileta vile vikombe vya dhahabu ambavyo vilikuwa vimechukuliwa kutoka Hekalu la Mungu huko Yerusalemu, naye mfalme na wakuu wake, wake zake na masuria wake wakavinywea. 45:4 Es 1:10; Ufu 9:20; Za 115:4-8; Amu 16:24; Hag 2:19; Za 135:15-18Walipokuwa wakinywa mvinyo, wakaisifu miungu ya dhahabu na fedha, ya shaba, chuma, miti na mawe.

5Ghafula vidole vya mkono wa mwanadamu vilitokea na kuandika juu ya ukuta, karibu na kinara cha taa ndani ya jumba la mfalme. Mfalme akatazama kitanga kilivyokuwa kikiandika. 65:6 Dan 4:5; Za 22:14; Nah 2:10; Ay 4:15; Isa 7:2; Eze 7:17Uso wa mfalme ukageuka rangi, naye akaogopa sana, kiasi kwamba magoti yake yaligongana na miguu yake ikalegea.

75:7 Isa 44:25; 47:13; Dan 4:6-7; Mwa 41:42; Dan 2:5-6, 48; 6:2-3; Mwa 41:8; Isa 19:3; 44:25; Yer 50:35; Es 10:3Mfalme akawaita wasihiri, wanajimu na waganga waletwe, naye akawaambia hawa wenye hekima wa Babeli, “Yeyote asomaye maandishi haya na kuniambia maana yake atavikwa nguo za zambarau, na kuvikwa mkufu wa dhahabu shingoni mwake, naye atafanywa mtawala wa cheo cha tatu katika ufalme.”

85:8 Dan 2:10, 27; 4:18; Mwa 41:8; 41:8; Kut 8:18Ndipo watu wote wa mfalme wenye hekima wakaingia, lakini hawakuweza kusoma yale maandishi wala kumwambia mfalme maana yake. 95:9 Za 48:5; Isa 21:4Basi Mfalme Belshaza akazidi kujawa na hofu, na uso wake ukageuka rangi zaidi. Wakuu wake wakapigwa na bumbuazi.

105:10 Neh 2:3; Dan 3:9Malkia5:10 Au: Mama yake mfalme. aliposikia sauti za mfalme na wakuu wake, alikuja katika ukumbi wa karamu. Akasema, “Ee mfalme, uishi milele! Usishtuke! Usibadilike rangi kiasi hicho! 115:11 Mwa 41:38; Dan 4:8-9; 1:17; 2:47-48; 2:22; Mwa 41:38; Dan 2:22Yuko mtu katika ufalme wako ambaye ana roho ya miungu mitakatifu ndani yake. Wakati wa baba yako, mtu huyo alionekana kuwa na ufahamu, akili na hekima kama ile ya miungu. Mfalme Nebukadneza baba yako, yaani nasema mfalme baba yako, alimweka kuwa mkuu wa waganga, wasihiri, wanajimu na waaguzi. 125:12 Dan 1:7; 6:3; Hes 12:8; Eze 28:3Mtu huyu Danieli, ambaye mfalme alimwita Belteshaza, alionekana kuwa na akili nyepesi, maarifa na ufahamu, pia uwezo wa kufasiri ndoto, kueleza mafumbo na kutatua matatizo magumu. Mwite Danieli, naye atakuambia maana ya haya maandishi.”

135:13 Es 2:5-6; Dan 6:13Hivyo Danieli akaletwa mbele ya mfalme, naye mfalme akamuuliza, “Je, wewe ndiwe Danieli, mmoja wa watu wa uhamisho walioletwa na mfalme baba yangu kutoka Yuda? 14Nimesikia kwamba roho ya miungu iko ndani yako, na kwamba una ufahamu, akili na hekima ya pekee. 155:15 Dan 4:18Watu wenye hekima na wasihiri waliletwa mbele yangu ili kusoma maandishi haya na kuniambia maana yake, lakini hawakuweza kunifafanulia. 165:16 Mwa 41:15; 42; Es 5:3; Dan 2:6; Mwa 41:15, 42Basi nimesikia kwamba unaweza kutoa tafsiri na kutatua matatizo magumu. Ikiwa unaweza kusoma maandishi haya na kuniambia maana yake, utavikwa nguo za zambarau na mkufu wa dhahabu shingoni mwako, nawe utafanywa mtawala wa tatu katika ufalme.”

175:17 2Fal 5:16Ndipo Danieli akamjibu mfalme, “Waweza kubaki na zawadi zako mwenyewe na kumpa mtu mwingine zawadi zako. Hata hivyo, nitasoma maandishi kwa mfalme na kumwambia maana yake.

185:18 Yer 27:7; Dan 4:36; Yer 28:14; Dan 2:37-38“Ee mfalme, Mungu Aliye Juu Sana alimpa baba yako Nebukadneza utawala, ukuu, utukufu na fahari. 195:19 Dan 2:12-13; 3:6; Yer 25:9; Dan 4:22Kwa sababu ya nafasi ya juu aliyompa baba yako, kabila zote za watu, mataifa na watu wa kila lugha walimhofu na kumwogopa. Wale ambao mfalme alitaka kuwaua, aliwaua; wale aliotaka kuwaacha hai, aliwaacha hai; wale aliotaka kuwapandisha cheo, aliwapandisha; aliotaka kuwashusha, aliwashusha. 205:20 Dan 4:30; Yer 13:18; Ay 40:12; Eze 31:10-11; Isa 14:12; Yer 43:10; Dan 8:8Lakini moyo wake ulipokuwa na majivuno na kuwa mgumu kwa kiburi, aliondolewa kutoka kwa kiti chake cha ufalme na kuvuliwa utukufu wake. 215:21 Eze 17:24; Kut 9:14-16; Dan 4:16-17Akafukuzwa mbali na wanadamu na kupewa akili ya mnyama, akaishi pamoja na punda-mwitu, akala majani kama ngʼombe, nao mwili wake ukaloweshwa kwa umande wa mbingu, mpaka alipotambua kwamba Mungu Aliye Juu Sana ndiye mtawala juu ya falme za wanadamu na kwamba humtawaza juu yao yeyote amtakaye.

225:22 Kut 10:3; 2Nya 33:23“Lakini wewe mwanawe, ee Belshaza, hukujinyenyekeza, ingawa ulifahamu haya yote. 235:23 Ufu 13:6; Isa 14:13; Hes 2:19; Yer 50:29; Ufu 9:20; Ay 12:10; Mdo 17:28; Yer 44:9; Ay 31:4; Za 115:4-8; Hab 2:19; Isa 13:11; Yer 10:23; 48:26Badala yake, umejiinua dhidi ya Bwana wa mbingu. Uliletewa vikombe vya Hekalu lake, nawe na wakuu wako, wake zako na masuria wako mlivitumia kwa kunywea mvinyo. Ukaisifu miungu ya fedha na dhahabu, ya shaba, chuma, miti na mawe, miungu ambayo haiwezi kuona, au kusikia wala kufahamu. Lakini hukumheshimu Mungu ambaye anaushikilia uhai wako na njia zako zote mkononi mwake. 24Kwa hiyo ameutuma mkono ule ulioandika maneno.

25“Haya ndiyo maneno yaliyoandikwa:

mene, mene, tekeli na peresi

265:26 Yer 27:7; Isa 13:9“Hii ndiyo maana ya maneno haya:

Mene: Mungu amezihesabu siku za utawala wako na kuukomesha.

275:27 Za 62:9; Yer 6:30; Ay 6:2Tekeli: Wewe umepimwa katika mizani na umeonekana umepungua.

285:28 Isa 13:17; Yer 50:41-43; Dan 6:28; Yer 7:27Peresi: Ufalme wako umegawanywa na kupewa Wamedi na Waajemi.”

295:29 Mwa 41:42; Dan 2:6Ndipo kwa amri ya Belshaza, Danieli akavikwa nguo za zambarau na mkufu wa dhahabu shingoni, tena akatangazwa kuwa mtawala wa tatu katika ufalme.

305:30 Isa 21:9; Yer 51:31; 50:35Usiku ule ule, Belshaza mfalme wa Wakaldayo akauawa, 315:31 Yer 50:41; Dan 11:1; Isa 13:3naye Dario Mmedi akashika ufalme akiwa na miaka sitini na miwili.