以賽亞書 52 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以賽亞書 52:1-15

錫安必獲救

1錫安啊,醒來吧,醒來吧,展示你的能力!

聖城耶路撒冷啊,

穿上你華美的衣服!

從今以後,

未受割禮和不潔淨的人必不得進入你的城門。

2耶路撒冷啊,抖掉身上的灰塵,

起來坐到寶座上!

被擄的錫安城啊,

卸去你頸上的鎖鏈!

3耶和華說:「你們被賣未得分文,你們被贖回也不需分文。」 4主耶和華說:「起先我的子民到埃及寄居,後來亞述人無緣無故地欺壓他們。」 5耶和華說:「我這裡還有什麼呢?我的子民白白地被擄去,轄制他們的人咆哮大叫,我的名整天被褻瀆。 6然而,我的子民終會認識我的名。到那日,他們就會知道是我對他們說,『我在這裡。』」

7那穿山越嶺之人的腳蹤是何等佳美!

他帶來佳音,報告平安,

傳遞喜訊,宣佈救恩,

錫安說:「你的上帝做王了。」

8聽啊,你的守望者都一同高聲歡呼,

因為耶和華回到錫安的時候,

他們必親眼看見。

9耶路撒冷的荒場啊,

你們要一同歡呼歌唱,

因為耶和華安慰了祂的子民,

救贖了耶路撒冷

10耶和華要向萬國展現祂神聖的大能,

普天下將看見我們上帝的救恩。

11離開吧,離開吧,

離開巴比倫吧!

不要碰不潔淨的東西。

你們抬耶和華器具的人啊,

要從那裡出來,要潔淨自己。

12你們不必匆忙離開,

也不用奔逃,

因為耶和華必走在你們前面,

以色列的上帝必作你們的後盾。

13看啊,我的僕人必成功,

受到擁戴、仰慕和尊崇。

14許多人看見祂就詫異,

祂的面容被毀、身體被殘害得不成人樣。

15祂必洗淨許多國家,

君王必因祂而閉口無言。

因為他們將看見未曾聽過的事,

明白聞所未聞的事。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 52:1-15

152:1 Isa 51:9; Es 6:8; Ufu 21:2; Yoe 3:17; Zek 3:4; Isa 49:18; Kut 28:2, 40; Neh 1:1Amka, amka, ee Sayuni,

jivike nguvu.

Vaa mavazi yako ya fahari,

ee Yerusalemu, mji mtakatifu.

Asiyetahiriwa na aliye najisi

hataingia kwako tena.

252:2 Zek 2:7; Isa 29:4; 10:27; Za 81:9; 9:14Jikungʼute mavumbi yako,

inuka, uketi kwenye kiti cha enzi, ee Yerusalemu.

Jifungue minyororo iliyo shingoni mwako,

ee Binti Sayuni uliye mateka.

352:3 Za 44:12; Isa 45:13; 1:27; 1Pet 1:18Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana:

“Mliuzwa pasipo malipo,

nanyi mtakombolewa bila fedha.”

452:4 Mwa 46:6; Isa 10:24Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi:

“Hapo kwanza watu wangu walishuka Misri kuishi,

hatimaye, Ashuru wakawaonea.

552:5 Eze 36:20; Rum 2:24; Isa 37:23“Basi sasa nina nini hapa?” asema Bwana.

“Kwa kuwa watu wangu wamechukuliwa pasipo malipo,

nao wale wanaowatawala wanawadhihaki,”

asema Bwana.

“Mchana kutwa

jina langu limetukanwa bila kikomo.

652:6 Isa 49:23; Kut 6:3; Isa 41:26; 10:20Kwa hiyo watu wangu watalijua Jina langu;

kwa hiyo katika siku ile watajua

kwamba ndimi niliyetangulia kulisema.

Naam, ni mimi.”

752:7 2Sam 18:26; Rum 10:15; 1Kor 15:24-25; Lk 2:14; Isa 42:11; 40:9; Efe 6:15Tazama jinsi miguu ya wale waletao habari njema

ilivyo mizuri juu ya milima,

wale wanaotangaza amani,

wanaoleta habari njema,

wanaotangaza wokovu,

wauambiao Sayuni,

“Mungu wako anatawala!”

852:8 Sef 3:9; Eze 3:17; 1Sam 14:16; Isa 56:10; Yer 6:17; Hes 10:36; Zek 8:3Sikiliza! Walinzi wako wanapaza sauti zao,

pamoja wanapaza sauti zao kwa furaha.

Wakati Bwana atakaporejea Sayuni,

wataliona kwa macho yao wenyewe.

952:9 Za 98:4; Isa 35:2; Za 74:3; Isa 48:20; Ezr 9:9; Lk 2:25; Isa 51:3Pazeni sauti ya nyimbo za furaha pamoja,

enyi magofu ya Yerusalemu,

kwa maana Bwana amewafariji watu wake,

ameikomboa Yerusalemu.

1052:10 Lk 2:30; Za 67:2; Isa 66:18; 2Nya 32:8; Za 44:3; Isa 30:30; Yos 4:24Mkono mtakatifu wa Bwana umefunuliwa

machoni pa mataifa yote,

nayo miisho yote ya dunia itaona

wokovu wa Mungu wetu.

1152:11 Yer 50:8; 2Kor 6:17; Hes 8:6; 2Tim 2:9; Isa 1:16; 2Nya 36:10; Isa 48:20Ondokeni, ondokeni, tokeni huko!

Msiguse kitu chochote kilicho najisi!

Tokeni kati yake mwe safi,

ninyi mchukuao vyombo vya Bwana.

1252:12 Kut 14:19; 12:11; Mik 2:13; Yn 10:4Lakini hamtaondoka kwa haraka,

wala hamtakwenda kwa kukimbia;

kwa maana Bwana atatangulia mbele yenu,

Mungu wa Israeli atakuwa mlinzi nyuma yenu.

Mateso Na Utukufu Wa Mtumishi

1352:13 Isa 53:3; Mdo 3:13; Yos 1:8; Isa 20:3; 57:15; Flp 2:9Tazama, mtumishi wangu atatenda kwa hekima;

atatukuzwa, na kuinuliwa juu, na kukwezwa sana.

1452:14 Law 26:32; Ay 2:12; 16:16; 18:20; 2Sam 10:4Kama walivyokuwa wengi

walioshangazwa naye,

kwani uso wake ulikuwa umeharibiwa sana

zaidi ya mtu yeyote

na umbo lake kuharibiwa

zaidi ya mfano wa mwanadamu:

1552:15 Ebr 9:13; Rum 15:21; Efe 3:4-5; Za 107:42; Amu 18:19; Law 14:7; 16:14-15hivyo atayashangaza mataifa mengi,

nao wafalme watafunga vinywa vyao kwa sababu yake.

Kwa kuwa yale ambayo hawakuambiwa, watayaona,

nayo yale wasiyoyasikia, watayafahamu.