以賽亞書 50 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以賽亞書 50:1-11

以色列的罪惡

1耶和華說:

「我休你們母親的休書在哪裡呢?

我把你們賣給了我哪一個債主呢?

你們被賣是因為你們的罪惡,

你們母親被休是因為你們的過犯。

2為什麼我來的時候一個人也不在?

為什麼我呼喚的時候沒有人回答?

是我的臂膀太短不能救贖你們嗎?

是我沒有能力拯救你們嗎?

看啊,我斥責一聲,海就乾了;

我使江河變為曠野,

魚類因無水而乾死,發出腥臭。

3我使黑暗遮蔽穹蒼,

用麻布掩蓋天空。」

主僕的順服

4主耶和華賜我教導的能力,

使我知道用什麼話幫助疲乏的人。

每天早晨,主喚醒我,

叫我像受教者那樣側耳聆聽。

5主耶和華開了我的耳朵,

我沒有悖逆,也沒有退縮。

6人打我的背,我任他打;

人拔我的鬍子,我任他拔;

人侮辱我,朝我吐唾沬,

我也不掩面。

7我並不覺得羞愧,

因為主耶和華幫助我。

我心如堅石,

知道自己必不會蒙羞。

8為我伸張正義的來了,

誰要控告我呢?

讓我們來理論吧!

誰是我的控告者呢?

讓他到我這裡來吧!

9看啊,有主耶和華幫助我,

誰能定我有罪呢?

看啊,他們都要像衣服一樣漸漸破舊,

被蛀蟲吃掉。

信靠上帝

10你們中間誰敬畏耶和華,

聽從祂僕人的話?

行在黑暗中、

沒有光的人要信靠耶和華的名,

仰賴自己的上帝。

11然而,你們自己生火、自備火把的人啊,

靠自己點燃的火光行走吧!

你們必落入悲慘的境地,

這是耶和華親手所定的。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 50:1-11

Dhambi Ya Israeli Na Utii Wa Mtumishi

150:1 Kum 24:1; Mk 10:4; Mt 18:25; Amu 3:8; Hos 2:2; Mt 19:7; Neh 5:5; Isa 1:25Hili ndilo asemalo Bwana:

“Iko wapi hati ya talaka ya mama yako

ambayo kwayo niliachana naye?

Au nimewauza ninyi kwa nani

miongoni mwa watu wanaonidai?

Kwa ajili ya dhambi zenu mliuzwa,

kwa sababu ya makosa, mama yenu aliachwa.

250:2 Mwa 18:14; Kut 14:22; Hes 11:23; 1Sam 8:19; Isa 41:28; Za 68:35; Yer 14:9Nilipokuja, kwa nini hakuwepo hata mmoja?

Nilipoita, kwa nini hakuwepo hata mmoja wa kujibu?

Je, mkono wangu ni mfupi mno hata nisiweze kuwakomboa?

Je, mimi sina nguvu za kukuokoa?

Kwa kukemea tu naikausha bahari,

naigeuza mito ya maji kuwa jangwa;

samaki wake wanaoza kwa kukosa maji

na kufa kwa ajili ya kiu.

350:3 Isa 5:30; Ufu 6:12; Kut 10:21Ninalivika anga weusi na kufanya nguo ya gunia

kuwa kifuniko chake.”

450:4 Kut 4:11-12; Za 88:13; Mt 7:29; Isa 40:29; Mt 11:28Bwana Mwenyezi amenipa ulimi uliofundishwa,

ili kujua neno limtegemezalo aliyechoka.

Huniamsha asubuhi kwa asubuhi,

huamsha sikio langu lisikie kama mtu afundishwaye.

550:5 Isa 35:5; Eze 2:8; Ebr 10:5; Isa 48:16; Eze 24:3; Mdo 26:19; Mt 26:39Bwana Mwenyezi amezibua masikio yangu,

nami sikuwa mwasi,

wala sikurudi nyuma.

650:6 Mt 27:30; Isa 53:5; Mao 3:30; Hes 12:14; Mt 26:67; Mk 14:65Niliwapa mgongo wangu wale wanipigao,

mashavu yangu wale wangʼoao ndevu zangu;

sikuuficha uso wangu kutokana na fedheha

na kutemewa mate.

750:7 Isa 41:10; Rum 8:31; Eze 3:8-9; Isa 48:16; 28:16; 29:22Kwa sababu Bwana Mwenyezi ananisaidia,

sitatahayarika.

Kwa hiyo nimekaza uso wangu kama jiwe la gumegume,

nami ninajua sitaaibika.

850:8 Ay 13:19; Rum 8:32-34; 1Kor 4:4; Isa 26:2; 49:4Yeye anipatiaye haki yangu yu karibu.

Ni nani basi atakayeleta mashtaka dhidi yangu?

Tukabiliane uso kwa uso!

Mshtaki wangu ni nani?

Ni nani aliye mshtaki wangu?

950:9 Ay 13:28; Isa 41:10; Ebr 1:11-12; Rum 8:1, 34; Isa 51:8Ni Bwana Mwenyezi anisaidiaye mimi.

Ni nani huyo atakayenihukumu?

Wote watachakaa kama vazi,

nondo watawala wawamalize.

1050:10 2Nya 20:20; Isa 49:3; 26:4; 1:19; Hag 1:12; Mdo 26:18; Isa 10:20Ni nani miongoni mwenu amchaye Bwana,

na kulitii neno la mtumishi wake?

Yeye atembeaye gizani,

yeye asiye na nuru,

na alitumainie jina la Bwana,

na amtegemee Mungu wake.

1150:11 Mit 26:18; Yak 3:6; Ay 15:20; Isa 65:13-15; Kum 21:22-23Lakini sasa, ninyi nyote mnaowasha mioto,

na kupeana mienge iwakayo ninyi kwa ninyi,

nendeni, tembeeni katika nuru ya moto wenu

na ya mienge mliyoiwasha.

Hili ndilo mtakalolipokea kutoka mkononi mwangu:

Mtalala chini kwa mateso makali.