以賽亞書 25 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以賽亞書 25:1-12

讚美之歌

1耶和華啊!你是我的上帝,我要尊崇你,讚美你的名。你信實無比,

按你古時定下的計劃行了奇妙的事。

2你使城邑淪為廢墟,

使堅壘淪為荒場。

外族人的宮殿不復存在,

永遠不能重建。

3因此,強盛的國家必頌揚你,

殘暴的民族必敬畏你。

4你是貧窮人的避難所,

是困苦之人患難中的避難所,

你是避風港,

是酷暑中的陰涼處。

殘暴之徒的氣息好像吹襲牆垣的暴風,

5又像沙漠中的熱氣。

但你平息外族人的喧嘩,

止息殘暴之徒的歌聲,

好像雲朵消去酷熱。

6錫安山上,萬軍之耶和華必為天下萬民擺設豐盛的宴席,有陳年佳釀和精選的美食。 7在這山上,祂必除去遮蔽萬民的面紗和籠罩萬國的幔子。 8祂必永遠吞滅死亡。主耶和華必擦去各人臉上的眼淚,從世上除掉祂子民的羞辱。這是耶和華說的。 9到那日,人們必說:「看啊,這是我們的上帝,我們信靠祂,祂拯救了我們。這是耶和華,我們信靠祂,我們要因祂的拯救而歡喜快樂。」 10耶和華必伸手保護這山,但摩押人必被踐踏,像乾草被踐踏在糞池中。 11他們必在裡面張開手臂,好像張開手臂游泳的人一樣。耶和華必摧毀他們的驕傲,挫敗他們手中的詭計。 12祂必拆毀他們高大堅固的城牆,將其夷為平地、化為塵土。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 25:1-12

Msifuni Bwana

125:1 Hes 23:19; Za 40:5; Yoe 2:21-26; Isa 7:13; 14:24; 37:26; Efe 1:11Ee Bwana, wewe ni Mungu wangu,

nitakutukuza na kulisifu jina lako,

kwa maana katika ukamilifu wa uaminifu

umetenda mambo ya ajabu,

mambo yaliyokusudiwa tangu zamani.

225:2 Isa 37:26; Yer 51:37; Isa 17:3; 13:22; Kum 13:16; Ay 12:14Umeufanya mji kuwa lundo la kifusi,

mji wenye ngome kuwa magofu,

ngome imara ya wageni kuwa si mji tena,

wala hautajengwa tena kamwe.

325:3 Kut 6:2; Za 22:23; Isa 11:14; 13:11; Ufu 11:13Kwa hiyo mataifa yenye nguvu yatakuheshimu,

miji ya mataifa katili itakuheshimu wewe.

425:4 Yoe 3:16; Isa 33:16; Za 46:1-11; Isa 49:25; 2Sam 22:3; Za 118:8; Isa 3:14Umekuwa kimbilio la watu maskini,

kimbilio la mhitaji katika taabu yake,

hifadhi wakati wa dhoruba

na kivuli wakati wa hari.

Kwa maana pumzi ya wakatili

ni kama dhoruba ipigayo ukuta

525:5 Yer 51:25; Za 18:44; Isa 13:11na kama joto la jangwani.

Wewe wanyamazisha makelele ya wageni;

kama vile hari ipunguzwavyo na kivuli cha wingu,

ndivyo wimbo wa wakatili unyamazishwavyo.

625:6 Mt 22:4; Mit 9:2; Dan 7:14; Mwa 29:22; Za 36:8Juu ya mlima huu Bwana Mwenye Nguvu Zote ataandaa

karamu ya vinono kwa mataifa yote,

karamu ya mvinyo wa zamani,

nyama nzuri sana na divai zilizo bora sana.

725:7 2Kor 3:15-16; Efe 4:8; 1:17; Ay 4:9Juu ya mlima huu ataharibu

sitara ihifadhiyo mataifa yote,

kile kifuniko kifunikacho mataifa yote,

825:8 Hos 13:14; 1Kor 15:54-55; Yer 31:16; Ufu 7:14-17; Ebr 2:14; Isa 26:19yeye atameza mauti milele.

Bwana Mwenyezi atafuta machozi katika nyuso zote;

ataondoa aibu ya watu wake duniani kote.

Bwana amesema hili.

925:9 Isa 40:9; Yer 14:8; Za 20:5; Kum 32:43; Isa 2:11; 49:25-26; Za 145:19Katika siku ile watasema,

“Hakika huyu ndiye Mungu wetu;

tulimtumaini, naye akatuokoa.

Huyu ndiye Bwana, tuliyemtumaini;

sisi tushangilie na kufurahia katika wokovu wake.”

1025:10 Mwa 19:37; Hes 21:29; Kum 23:6; Isa 11:14; Amo 2:1-2Mkono wa Bwana utatulia juu ya mlima huu,

bali Moabu atakanyagwa chini

kama majani makavu yakanyagwavyo kwenye shimo la mbolea.

1125:11 Isa 5:25; 14:26; Law 26:19; Ay 40:12; Isa 2:10-17; 16:14Watakunjua mikono yao katikati yake,

kama vile mwogeleaji akunjuavyo mikono yake ili aogelee.

Mungu atashusha kiburi chao

licha ya ujanja wa mikono yao.

1225:12 Ay 40:11; Isa 26:5; Yer 51:44; Isa 2:15Atabomoa kuta ndefu za maboma yako

na kuziangusha chini,

atazishusha chini ardhini,

mpaka mavumbini kabisa.