以賽亞書 19 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以賽亞書 19:1-25

關於埃及的預言

1以下是關於埃及的預言:

看啊,耶和華駕著疾馳的雲來到埃及

埃及的偶像在祂面前顫抖,

埃及人膽戰心驚。

2「我必使埃及人彼此為敵——手足相殘,

鄰居互鬥,城邑相爭,

邦國互攻。

3埃及人必灰心喪志,

我必破壞他們的計謀。

他們必求問偶像、巫師、靈媒和術士。

4我必將埃及人交給一位殘忍的主人,

一位暴君必統治他們。」

這是主——萬軍之耶和華說的。

5尼羅河必枯竭,

河床必乾涸。

6河流必發臭,

埃及的河流逐漸枯竭。

蘆荻和燈心草必枯死,

7尼羅河兩岸青草枯黃,

田地龜裂,莊稼被風吹去,

蕩然無存。

8所有在尼羅河下鉤的漁夫都哀哭悲傷,

在河上撒網的人都傷痛。

9紡紗織布的人一籌莫展,

感到絕望。

10埃及的顯貴都沒落,

靠工錢維生的人都憂心忡忡。

11埃及王聰明的謀士——瑣安的首領們變得愚不可及。

他們怎敢在埃及王面前自稱是古聖先賢的子孫呢?

12埃及王啊,你的智者在哪裡呢?

讓他們把萬軍之耶和華對付埃及的計劃告訴你吧!

13瑣安的首領愚昧,

挪弗的首領糊塗。

他們是埃及的房角石,

卻把埃及人引入歧途。

14耶和華使錯謬的靈進入他們當中,

使他們像又嘔又吐、東倒西歪的醉漢,

做什麼都錯誤百出。

15埃及從首領到平民,

從權貴到草根必一籌莫展。

16到那日,當萬軍之耶和華揮拳懲罰的時候,埃及人必恐懼戰抖,如柔弱的女子。 17他們必對猶大充滿恐懼,一聽見猶大的名字就害怕,因為萬軍之耶和華定下計劃要對付他們。 18到那日,埃及必有五座城的人講迦南的語言,並信奉萬軍之耶和華,其中有一座必叫滅亡城19·18 滅亡城」有些抄本作「太陽城」。

19到那日,埃及的中央必有一座為耶和華築的祭壇,邊境必有一根為耶和華立的石柱。 20這是萬軍之耶和華在埃及的記號和憑據。埃及人因受到欺壓就呼求耶和華,祂必差遣一位救主保護、拯救他們。 21耶和華必向埃及人彰顯自己。到那日,埃及人必認識祂,帶著祭物和供品來敬拜祂,向祂許願還願。 22耶和華必擊打他們,也必醫治他們。他們必歸向耶和華,祂必應允他們的禱告,醫治他們。

23到那日,必有一條大道連接埃及亞述,兩國人民可以互相往來,一同敬拜耶和華。 24到那日,以色列必與埃及亞述一同成為世人的祝福。 25萬軍之耶和華必賜福給他們,說:「我的子民埃及、我手中的傑作亞述、我的產業以色列都有福了!」

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 19:1-25

Unabii Kuhusu Misri

119:1 Yer 43:12; Yoe 3:19; Kut 12:12; 2Sam 22:10; Yos 2:11; Isa 20:3; Kum 10:14; Isa 13:1Neno kuhusu Misri:

Tazama, Bwana amepanda juu ya wingu liendalo kwa haraka

naye anakuja Misri.

Sanamu za Misri zinatetemeka mbele yake,

nayo mioyo ya Wamisri inayeyuka ndani yao.

219:2 Amu 7:22; 12:4; Mk 13:8; Mt 10:21, 36; 24:7; 2Nya 15:6; Lk 21:10“Nitamchochea Mmisri dhidi ya Mmisri,

ndugu atapigana dhidi ya ndugu,

jirani dhidi ya jirani,

mji dhidi ya mji,

ufalme dhidi ya ufalme.

319:3 Law 19:31; Dan 2:2, 10; Za 18:45; Ay 5:12; 2Nya 10:13; Isa 47:13Wamisri watakufa moyo,

na nitaibatilisha mipango yao.

Watatafuta ushauri kwa sanamu na kwa roho za waliokufa,

kwa waaguzi na kwa wale waongeao na mizimu.

419:4 Yer 46:26; Eze 32:11; 29:19; Isa 20:4Nitawatia Wamisri

mikononi mwa bwana mkatili

na mfalme mkali atatawala juu yao,”

asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote.

519:5 Isa 44:27; Yer 50:38; 2Sam 14:14Maji ya mito yatakauka,

chini ya mto kutakauka kwa jua.

619:6 Kut 7:18; Eze 30:12; Isa 37:25; 15:6; Mwa 41:2; Ay 8:11Mifereji itanuka;

vijito vya Misri vitapungua

na kukauka.

Mafunjo na nyasi vitanyauka,

719:7 Kum 29:23; Isa 23:3; Zek 10:11; Hes 11:5pia mimea iliyoko kando ya Mto Naili,

pale mto unapomwaga maji baharini.

Kila shamba lililopandwa kando ya Mto Naili litakauka,

litapeperushwa na kutoweka kabisa.

819:8 Hes 11:5; Amo 4:2; Hab 1:15; Eze 47:10Wavuvi watalia na kuomboleza,

wale wote watupao ndoano katika Mto Naili,

watadhoofika kwa majonzi.

919:9 Mit 7:16; Eze 16:10; 27:7; Yos 2:10Wale watu wafanyao kazi ya kitani kilichochambuliwa watakata tamaa,

wafumaji wa kitani safi watavunjika moyo.

10Wafanyao kazi ya kufuma nguo watahuzunishwa,

nao vibarua wataugua moyoni.

1119:11 Hes 13:22; 1Fal 4:30; Mdo 7:22; Mwa 41:37Maafisa wa Soani ni wapumbavu kabisa,

washauri wa Farao wenye busara wanatoa ushauri wa kijinga.

Unawezaje kumwambia Farao,

“Mimi ni mmojawapo wa watu wenye hekima,

mwanafunzi wa wafalme wa zamani”?

1219:12 1Kor 1:20; Isa 41:22-23; Rum 9:17; Isa 14:24Wako wapi sasa watu wako wenye hekima?

Wao wakuonyeshe na kukufahamisha

ni nini Bwana Mwenye Nguvu Zote

amepanga dhidi ya Misri.

1319:13 Yer 2:16; Hos 9:6; Hes 13:22; Yer 46:14-19; Eze 30:13-16; Za 118:22Maafisa wa Soani wamekuwa wapumbavu,

viongozi wa Memfisi19:13 Memfisi kwa Kiebrania ni Nofu. wamedanganyika,

walio mawe ya pembe ya taifa lake

wameipotosha Misri.

1419:14 Mit 12:8; Mt 17:17; Za 107:27Bwana amewamwagia

roho ya kizunguzungu;

wanaifanya Misri iyumbayumbe

katika yale yote inayoyafanya,

kama vile mlevi ayumbayumbavyo

katika kutapika kwake.

1519:15 Isa 9:14Misri haiwezi kufanya kitu chochote,

cha kichwa wala cha mkia,

cha tawi la mtende wala cha tete.

1619:16 Isa 2:17; 11:10; Nah 3:13; Kum 2:25Katika siku ile Wamisri watakuwa kama wanawake. Watatetemeka kwa hofu mbele ya mkono wa Bwana Mwenye Nguvu Zote anaoinua dhidi yao. 1719:17 Mwa 35:5; Isa 14:24Nayo nchi ya Yuda itawatia hofu Wamisri, kila mmoja atakayetajiwa Yuda ataingiwa na hofu, kwa sababu ya kile ambacho Bwana Mwenye Nguvu Zote anapanga dhidi yao.

1819:18 Za 22:27; Yer 4:2; 43:13; Isa 10:20; 24:12; 32:19; Sef 3:9; Yer 44:1; Isa 48:1Katika siku hiyo miji mitano ya Misri, itazungumza lugha ya Kanaani, na kuapa kumtii Bwana Mwenye Nguvu Zote. Mji mmojawapo utaitwa Mji wa Uharibifu.19:18 Yaani Heliopoli (Mji wa Jua).

1919:19 Yos 22:10; Kut 24:4; Za 68:18; Mwa 12:7; 28:18; Isa 10:20; Za 68:31Katika siku hiyo patakuwepo madhabahu ya Bwana katikati ya Misri na mnara wa kumbukumbu kwa Bwana kwenye mpaka wa Misri. 2019:20 Isa 25:9; 49:24-26; Yos 4:20; Mwa 21:30; Amu 2:18; Kum 28:29Itakuwa alama na ushahidi kwa ajili ya Bwana Mwenye Nguvu Zote katika nchi ya Misri. Watakapomlilia Bwana kwa sababu ya watesi wao, Mungu atawapelekea mwokozi na mtetezi, naye atawaokoa. 2119:21 Isa 11:9; 43:10; 56:7; Mwa 27:29; Za 86:9; Hes 30:2; Kum 23:21Hivyo Bwana atajijulisha mwenyewe kwa Wamisri, nao katika siku hiyo watamkubali Bwana. Wataabudu kwa kumtolea dhabihu na sadaka za nafaka, watamwekea Bwana nadhiri na kuzitimiza. 2219:22 Kut 12:23; 11:10; Ebr 12:11; Eze 33:11; Yoe 2:13; Kum 32:39; Isa 45:14; Hos 10:2Bwana ataipiga Misri kwa tauni; atawapiga na kuwaponya. Watamgeukia Bwana, naye atayasikia maombi yao na kuwaponya.

2319:23 Isa 11:15-16; 20:6; 27:13; 66:23; Mik 7:12; Mwa 27:29Katika siku hiyo kutakuwepo na njia kuu kutoka Misri hadi Ashuru. Waashuru watakwenda Misri, na Wamisri watakwenda Ashuru. Wamisri na Waashuru wataabudu pamoja. 2419:24 Isa 11:11; Mwa 12:2Katika siku hiyo Israeli itakuwa ya tatu, pamoja na Misri na Ashuru, nao watakuwa baraka kwa dunia. 2519:25 Za 87:4; 100:3; Efe 2:10; Kut 34:9; Yer 30:22; Hos 2:23; Mwa 12:3; Isa 29:23; 43:7Bwana Mwenye Nguvu Zote atawabariki, akisema, “Baraka iwe kwa Misri watu wangu, kwa Ashuru kazi ya mikono yangu, na kwa Israeli urithi wangu.”