以賽亞書 16 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以賽亞書 16:1-14

1摩押人從西拉穿過曠野,來到錫安城的山,

把羊羔獻給那裡的掌權者。

2亞嫩河渡口,

摩押16·2 摩押人」希伯來文是「摩押的女子」。如同被趕離巢穴的飛鳥。

3他們對猶大人說:「給我們出個主意,伸張正義吧!

請讓你們的影子在正午如黑夜,

遮蓋逃難的人,

不要出賣逃亡者。

4讓我們這些逃難的摩押人留在你們那裡,

好躲避毀滅者。」

欺壓和毀滅之事終必停止,

入侵者終必從地上消失。

5那時,必有一個寶座在愛中堅立,

大衛家的人必坐在上面以信實治國,

秉公審判,速行公義。

6我們聽說摩押人心驕氣傲、狂妄自大,

然而他們所誇耀的都是虛假的。

7他們必為摩押哀哭,

人人都必哀哭,

為不再有吉珥·哈列設的美味葡萄餅而哀歎、悲傷。

8因為希實本的農田荒廢,

西比瑪的葡萄樹枯萎。

各國的君王都來踐踏這些上好的葡萄樹。

它們的枝子曾經伸展到雅謝和曠野,

嫩枝一直蔓延到海。

9因此,我像雅謝人一樣為西比瑪的葡萄樹哀哭。

希實本以利亞利啊,

我用眼淚來澆灌你們,

因為再無人為你們的果品和莊稼而歡呼了。

10肥美的田園裡聽不到快樂的聲音,

葡萄園裡也無人歌唱歡呼,

榨酒池裡無人榨酒。

我已經使歡呼聲止息。

11我的內心為摩押

吉珥·哈列設哀鳴,

好像淒涼的琴聲。

12摩押人上邱壇祭拜,

卻落得精疲力盡;

在廟宇裡禱告,

卻毫無用處。

13以上是耶和華所說有關摩押的預言。 14現在,耶和華說:「正如一個雇工的工作年限是三年,摩押的榮耀也必在三年之內消失,那裡的人民必遭藐視,殘存的人必寥寥無幾、軟弱無力。」

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 16:1-14

Hali Ya Kukata Tamaa Ya Moabu

116:1 Isa 10:32; Amu 1:36; 2Fal 14:7; 2Nya 32:23; 2Fal 3:4; Oba 1:3Pelekeni wana-kondoo kama ushuru

kwa mtawala wa nchi,

Kutoka Sela, kupitia jangwani,

hadi mlima wa Binti Sayuni.

216:2 Mit 27:8; Hes 21:13-14; Yer 48:40; Hes 21:29Kama ndege wanaopapatika

waliofukuzwa kutoka kwenye kiota,

ndivyo walivyo wanawake wa Moabu

kwenye vivuko vya Arnoni.

316:3 1Fal 18:4“Tupeni shauri,

toeni uamuzi.

Wakati wa adhuhuri,

fanyeni kivuli chenu kama usiku.

Waficheni watoro,

msisaliti wakimbizi.

416:4 Isa 55:7; 9:4; 2:2-4Waacheni watoro wa Moabu wakae pamoja nanyi;

kuweni mahali pao pa salama ili kuepuka mharabu.”

Mtesi atafikia mwisho na maangamizi yatakoma,

aletaye vita atatoweka kutoka nchi.

516:5 1Sam 13:14; Mik 4:7; Isa 7:2; Dan 7:14; Mit 20:28; Isa 9:7; Lk 1:32Kwa upendo kiti cha enzi kitaimarishwa,

kwa uaminifu mtu ataketi juu yake,

yeye atokaye nyumba ya Daudi:

yeye ambaye katika kuhukumu hutafuta haki,

na huhimiza njia ya haki.

616:6 Eze 25:8; Yer 25:21; Law 26:19; Ay 20:6; Sef 2:8; Yer 49:16; Amo 2:1Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu:

kiburi chake cha kujivuna na udanganyifu,

kiburi chake na ufidhuli wake,

lakini majivuno yake si kitu.

716:7 1Nya 16:3; 2Fal 3:25; Yer 48:20; 49:3; Isa 13:6Kwa hiyo Wamoabu wanaomboleza,

wanaiombolezea Moabu kwa pamoja.

Wanaomboleza na kuhuzunika

kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.

816:8 Ay 8:16; Hes 21:32; 21:25; Isa 15:6; 5:2; Ay 8:16; Za 80:11Mashamba ya Heshboni yananyauka,

pia na mizabibu ya Sibma.

Watawala wa mataifa

wamekanyaga mizabibu iliyo mizuri sana,

ambayo ilipata kufika Yazeri

na kuenea kuelekea jangwani.

Machipukizi yake yalienea

yakafika hadi baharini.

916:9 Isa 15:3; Eze 27:31; Yer 40:12; Ay 7:3; Hes 32:3; Ezr 3:13Hivyo ninalia kama Yazeri aliavyo,

kwa ajili ya mizabibu ya Sibma.

Ee Heshboni, ee Eleale,

ninakulowesha kwa machozi!

Kelele za furaha kwa ajili ya tunda lako lililoiva

na kwa ajili ya mavuno zimekomeshwa.

1016:10 Isa 24:7-8; Amu 9:27; Ay 24:11; Yer 25:30; Isa 5:2Furaha na shangwe zimeondolewa

kutoka mashamba ya matunda;

hakuna yeyote aimbaye wala apazaye sauti

katika mashamba ya mizabibu;

hakuna yeyote akanyagaye zabibu shinikizoni,

kwa kuwa nimekomesha makelele.

1116:11 Isa 15:5; Hos 11:8; Flp 2:1; Ay 30:31; Isa 63:15Moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama kinubi,

nafsi yangu yote kwa ajili ya Kir-Haresethi.

1216:12 Za 115:4-7; 1Kor 8:4; Hes 22:4; Isa 15:2; 1Fal 11:7; 18:29Wakati Moabu anapojitokeza mahali pake pa juu,

anajichosha mwenyewe tu;

anapokwenda mahali pake pa kuabudia miungu ili kuomba,

haitamfaidi lolote.

13Hili ndilo neno ambalo Bwana ameshasema kuhusu Moabu. 1416:14 Isa 25:10; Yer 48:42; Kum 15:18; 13:16; Isa 20:3; 37:30; Law 19:13Lakini sasa Bwana anasema: “Katika miaka mitatu, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, fahari ya Moabu na watu wake wengi watadharauliwa, nao walionusurika watakuwa wachache sana, tena wanyonge.”