以西結書 24 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以西結書 24:1-27

鏽鍋的比喻

1第九年十月十日,耶和華對我說: 2「人子啊,今天是巴比倫王圍攻耶路撒冷的日子,你要記下這日子。 3你要向叛逆的以色列人說比喻,告訴他們,主耶和華這樣說,

『把鍋放在火上,

裡面倒進水,

4把羊腿、羊肩等上好的肉塊放進鍋裡,

讓鍋裡盛滿精選的骨頭。

5要從羊群中選一頭上好的羊,

把柴堆在鍋下,

燒開鍋煮裡面的骨頭。』」

6主耶和華說:「這像鏽鍋一樣充滿血腥的城有禍了!要把肉從這鏽跡斑斑的鍋中一塊塊地取出來。 7這城沾滿血腥,任憑受害者的血流在光禿禿的磐石上,而不是流在地上用土掩蓋。 8我任憑這城把受害者的血灑在磐石上,不加掩蓋,好激起我的烈怒,使她受報應。 9所以主耶和華說,『血腥的城啊,你有禍了!我要預備大堆木柴, 10添在火上,燃起旺火,把肉煮爛,加入香料,燒焦骨頭。 11然後,把倒空的鍋放在炭火上燒熱,把銅燒紅,好熔化它的雜質,除淨鏽垢, 12卻徒勞無功,因為鏽垢太厚,就是用火也不能清除。 13耶路撒冷啊,淫蕩使你污穢不堪,我要潔淨你,你卻不願被潔淨。所以,除非我向你傾盡一切憤怒,否則你的污穢將不能清除。 14我耶和華言出必行,決不寬容,也不留情,我必照你的所作所為來審判你。』這是主耶和華說的。」

15耶和華對我說: 16「人子啊,我要突然奪去你心愛的人,你不可悲傷,也不可流淚哭泣。 17你要默然哀歎,不可為死人辦喪事,仍要纏著頭巾,穿著鞋,不可蒙著臉,也不可吃喪家吃的飯。」 18早晨我把這事告訴百姓,晚上我的妻子便死了。次日早晨,我便遵照耶和華的吩咐行。

19百姓問我:「你可以告訴我們,你這樣做跟我們有什麼關係嗎?」 20我告訴他們:「耶和華對我說, 21『你告訴以色列人,我要使我的聖所,就是你們引以為傲、眼中所愛、心裡所慕的受到褻瀆。你們留下的兒女必死於刀下。 22那時,你們將像我的僕人一樣不蒙臉,不吃喪家吃的飯。 23你們仍將裹著頭巾,穿著鞋,不哭泣,也不悲傷。你們必因自己的罪惡而默然歎息,逐漸滅亡。 24以西結做的事都是你們的預兆,你們也將做他做的。當這事發生時,你們就知道我是主耶和華了。』

25「人子啊,有一天我要奪去他們所喜悅、所誇耀、眼中所愛、心裡所慕的堡壘,也要奪去他們的兒女。 26那日,倖存的人必來告訴你這個消息。 27那時,你必開口向那人說話,不再沉默。你必成為他們的預兆,他們就知道我是耶和華。」

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 24:1-27

Chungu Cha Kupikia

124:1 Eze 8:1; 26:1; 29:17Katika mwaka wa tisa, mwezi wa kumi, siku ya kumi, neno la Bwana likanijia kusema: 224:2 2Fal 25:1; Yer 52:4; Isa 30:8; Hab 2:2; Yer 39:1“Mwanadamu, weka kumbukumbu ya tarehe hii, tarehe hii hasa, kwa kuwa mfalme wa Babeli ameuzingira mji wa Yerusalemu kwa jeshi siku hii ya leo. 324:3 Za 78:2; Eze 17:2; 11:3-6; 11:3Iambie nyumba hii ya kuasi fumbo, na uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Teleka sufuria jikoni; iteleke

na umimine maji ndani yake,

424:4 Eze 11:7Weka vipande vya nyama ndani yake,

vipande vyote vizuri,

vya paja na vya bega.

Ijaze hiyo sufuria kwa mifupa hii mizuri;

524:5 Isa 34:12; Yer 52:10, 24-27; Mik 3:2-3chagua yule aliye bora wa kundi la kondoo.

Panga kuni chini ya sufuria kwa ajili ya mifupa;

chochea mpaka ichemke

na uitokose hiyo mifupa ndani yake.

624:6 Eze 22:2; Ay 6:27; Nah 3:10; Oba 1:11; Eze 16:23; Yoe 3:3; Eze 11:11“ ‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Ole wa mji umwagao damu,

ole wa sufuria ambayo sasa

ina ukoko ndani yake,

ambayo ukoko wake hautoki.

Kipakue kipande baada ya kipande,

bila kuvipigia kura.

724:7 Law 17:13; Kum 12:16“ ‘Kwa kuwa damu aliyoimwaga ipo katikati yake:

huyo mwanamke aliimwaga

juu ya mwamba ulio wazi;

hakuimwaga kwenye ardhi,

ambako vumbi lingeifunika.

824:8 Mt 7:2Kuchochea ghadhabu na kulipiza kisasi,

nimemwaga damu yake

juu ya mwamba ulio wazi,

ili isifunikwe.

924:9 Eze 24:6; Nah 3:1; Hab 2:12“ ‘Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Ole wa mji umwagao damu!

Mimi nami nitalundikia kuni nyingi.

10Kwa hiyo lundika kuni

na uwashe moto.

Pika hiyo nyama vizuri,

changanya viungo ndani yake,

na uiache mifupa iungue kwenye moto.

1124:11 Yer 21:10; Eze 22:15Kisha teleka sufuria tupu kwenye makaa

mpaka iwe na moto sana na shaba yake ingʼae,

ili uchafu wake upate kuyeyuka

na ukoko wake upate kuungua na kuondoka.

12Imezuia juhudi zote,

ukoko wake mwingi haujaondoka,

hata ikiwa ni kwa moto.

1324:13 Mao 1:9; Zek 6:8; Eze 5:13; 8:18; Isa 22:14; Yer 6:28-30; Eze 16:18“ ‘Sasa uchafu wako ni uasherati wako. Kwa sababu nilijaribu kukutakasa lakini haikuwezekana kutakaswa kutoka kwenye huo uchafu wako, hutatakasika tena mpaka ghadhabu yangu dhidi yako iwe imepungua.

1424:14 Zek 8:14; Hes 23:19; Isa 3:11; Eze 18:30; Isa 22:14; Hes 11:23; Ay 27:22“ ‘Mimi Bwana nimesema, wakati umewadia wa mimi kutenda. Mimi sitazuia, mimi sitaona huruma wala sitapunguza hasira yangu, Utahukumiwa sawasawa na mwenendo na matendo yako, asema Bwana Mwenyezi.’ ”

Kifo Cha Mke Wa Ezekieli

15Neno la Bwana likanijia kusema: 1624:16 Yer 13:17; 16:5; Za 39:10; 84:1; Mao 2:4; Yer 22:10“Mwanadamu, kwa pigo moja nakaribia kukuondolea kile kilicho furaha ya macho yako. Lakini usiomboleze au kulia wala kudondosha machozi yoyote. 1724:17 Yer 16:7; Hes 20:29; Isa 3:20; 20:2; 20:2; Law 13:45Lia kwa uchungu kimya kimya usimwombolezee mtu aliyekufa. Jifunge kilemba chako na uvae viatu vyako miguuni mwako, usifunike sehemu ya chini ya uso wako, wala usile vyakula vya kawaida vya wakati wa matanga.”

1824:18 Eze 12:7Hivyo nikanena na watu asubuhi na jioni mke wangu akafa. Asubuhi yake nilifanya kama nilivyoamriwa.

1924:19 Eze 12:9; 37:18Ndipo watu wakaniuliza, “Je, jambo hili unalofanya linamaanisha nini kwetu?”

20Kwa hiyo nikawaambia, “Neno la Bwana lilinijia kusema: 2124:21 Za 27:4; Yer 7:14; Eze 23:25; Hos 9:12-16; Mal 2:12; Law 26:19, 31‘Sema na nyumba ya Israeli. Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninakaribia kupatia unajisi mahali pangu patakatifu, ngome ambayo ndani yake mnaona fahari, furaha ya macho yenu, kitu mnachokipenda. Wana wenu na binti zenu mliowaacha nyuma wataanguka kwa upanga. 2224:22 Yer 16:7; Law 13:45Nanyi mtafanya kama nilivyofanya. Hamtafunika sehemu ya chini ya nyuso zenu wala hamtakula vyakula vya kawaida vya waombolezaji. 2324:23 Kut 33:4; Ay 27:15; Za 78:64; Kut 28:39; Isa 3:20Mtajifunga vilemba vichwani mwenu na kuvaa viatu vyenu miguuni mwenu. Hamtaomboleza au kulia, lakini mtadhoofika kwa sababu ya dhambi zenu na kulia kwa uchungu kila mtu na mwenzake. 2424:24 Isa 20:3; Eze 4:3; Yn 13:19; Eze 12:11Ezekieli atakuwa ishara kwenu, mtafanya kama yeye alivyofanya. Wakati jambo hili litakapotokea, mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.’

2524:25 Kum 28:32; Yer 11:22; Za 20:4; Mao 2:4“Nawe, mwanadamu, siku ile nitakapoondoa ngome yao iliyo furaha yao na utukufu wao, kitu cha kupendeza macho yao, kile kilicho shauku ya mioyo yao, wana wao na binti zao vilevile, 2624:26 1Sam 4:12; Ay 1:15-19siku hiyo atakayetoroka atakuja kuwapasha habari. 2724:27 Eze 3:26; 33:22; Dan 10:15Katika siku ile kinywa chako kitamfumbukia yeye aliyenusurika, nawe utaongea wala hutanyamaza tena. Hivyo wewe utakuwa ishara kwao, nao watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.”