以斯拉記 6 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以斯拉記 6:1-22

發現塞魯士王的諭旨

1於是,大流士王下令查閱保存在巴比倫庫房裡的典籍。 2瑪代亞馬他城的宮內找到一卷書,書中記載如下:

3塞魯士王元年,塞魯士王就耶路撒冷的上帝之殿降下諭旨,要重建這殿作獻祭之處,要奠立殿的地基。殿要高二十七米、寬二十七米, 4每三層巨石加鋪一層木料,經費由國庫支付。 5尼布甲尼撒耶路撒冷上帝的殿裡擄到巴比倫的金銀器皿,都要歸還到耶路撒冷上帝的殿裡,放回原處。」

6於是,大流士王降旨:

「河西總督達乃示他·波斯乃,以及你們的同僚——河西的官員,要遠離那殿! 7不要干涉上帝殿的建造,要讓猶太人的省長和長老在原址上重建這座上帝的殿。 8另外,我降旨命你們幫助猶太人的長老建造上帝的殿,要立刻從河西的王室稅收中撥出款項作建殿之用,以免耽誤工程。 9他們向天上的上帝獻燔祭時所需的公牛犢、公綿羊、綿羊羔、小麥、鹽、酒和油,都要照耶路撒冷祭司的話天天供給他們,不得有誤, 10好讓他們向天上的上帝獻上蒙悅納的祭物,並為王和眾王子求壽。 11我再降旨,若有人更改這諭旨,必從他的房屋抽掉一根大樑,把他釘在樑上掛起來,他的房屋也要淪為糞堆。 12無論君王還是百姓,若有人擅自更改這命令或毀壞耶路撒冷的這殿,願揀選這殿作其居所的上帝毀滅他!我大流士降此諭旨,務要速速遵行。」

建殿工程竣工

13於是,河西總督達乃示他·波斯乃及其同僚都認真執行大流士王的諭旨。 14哈該先知和易多的子孫撒迦利亞的勸勉下,猶太人的長老建造這殿,進展順利。他們遵照上帝的命令和波斯塞魯士大流士亞達薛西的諭旨,完成了建殿工程。 15大流士王第六年亞達月6·15 亞達月」即希伯來曆的十二月,陽曆是二月中旬到三月中旬。三日,建殿工程竣工。

舉行獻殿禮

16以色列人、祭司、利未人,以及其餘流亡歸來的人都滿心歡喜地為上帝的殿舉行奉獻禮。 17他們為此獻上一百頭公牛犢,二百隻公綿羊和四百隻綿羊羔,又照以色列十二支派的數目獻上十二隻公山羊,作全體以色列人的贖罪祭。 18他們依照摩西律法書的規定,派祭司和利未人按班次在耶路撒冷事奉上帝。

守逾越節

19一月十四日,流亡歸來的人守逾越節。 20祭司和利未人一起自潔,成為潔淨的人,並為所有流亡歸來的人、其他祭司同胞以及他們自己宰殺逾越節的羔羊。 21從流亡之地歸回的以色列人,連同所有棄絕當地民族的污穢行為、尋求以色列的上帝耶和華的人,一起吃這羔羊。 22他們歡歡喜喜地守除酵節七天,因為耶和華使亞述王對他們心存善意,幫助他們重建以色列上帝的殿。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezra 6:1-22

Amri Ya Dario

16:1 Ezr 4:15; 5:17Kisha Mfalme Dario alitoa amri, nao wakafanya uchunguzi katika kumbukumbu zilizohifadhiwa katika hazina huko Babeli. 2Karatasi moja ndefu ya maandishi ilipatikana huko Ekbatana katika jimbo la Umedi. Haya ndiyo yaliyokuwa yameandikwa humo:

Kumbukumbu:

36:3 Ezr 3:10; Hag 2:3Katika mwaka wa kwanza wa kutawala Mfalme Koreshi, mfalme alitoa amri kuhusu Hekalu la Mungu katika Yerusalemu:

Hekalu na lijengwe tena mahali palepale Wayahudi walipokuwa wakitoa dhabihu, kwenye msingi ule ule. Iwe na kimo cha mikono sitini,6:3 Mikono 60 ni sawa na mita 27. upana wa mikono sitini, 46:4 1Fal 6:36; Ezr 7:20; Isa 60:6; Za 68:29kuta zijengwe kwa safu tatu za mawe makubwa kisha ifuate safu moja ya mbao. Gharama zitalipwa kutoka hazina ya mfalme. 56:5 1Nya 29:2; Yer 27:18-22; Ezr 5:14Pia, vyombo vya dhahabu na vya fedha vya nyumba ya Mungu, ambavyo Nebukadneza alivichukua kutoka kwenye Hekalu huko Yerusalemu akavileta Babeli, yapasa virudishwe mahali pake ndani ya Hekalu huko Yerusalemu, yapasa viwekwe ndani ya nyumba ya Mungu.

66:6 Ezr 5:3Sasa basi, Tatenai, mtawala wa Ngʼambo ya Mto Frati na Shethar-Bozenai pamoja na ninyi, maafisa wenzao wa jimbo hilo kaeni mbali na mahali hapo. 7Msiingilie kazi ya Hekalu hili la Mungu. Mwacheni mtawala wa Wayahudi na viongozi Wayahudi wajenge upya nyumba hii ya Mungu mahali pake.

86:8 1Sam 9:10Zaidi ya hayo, hapa natoa amri kuhusu mtakalofanya kwa ajili ya wazee wa Wayahudi katika ujenzi wa nyumba hii ya Mungu:

Gharama za watu hawa zitalipwa kikamilifu kutoka hazina ya mfalme, kutoka kwenye mapato ya Ngʼambo ya Mto Frati, ili ujenzi usisimame. 9Chochote kinachohitajika kama mafahali wachanga, kondoo dume, wana-kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa Mungu wa mbinguni, ngano, chumvi, divai na mafuta kama vitakavyohitajika na makuhani huko Yerusalemu, lazima wapewe kila siku pasipo kukosa, 106:10 Ezr 7:23; Yer 29:7; Law 1:9; Mwa 8:21; 1Tim 2:1-2ili waweze kutoa dhabihu inayompendeza Mungu wa mbinguni na kumwombea mfalme na wanawe hali njema.

116:11 Kum 21:22-23; Es 2:23; Ezr 7:26; Dan 2:5Zaidi ya hayo, ninaamuru kwamba mtu yeyote atakayebadilisha amri hii, boriti itangʼolewa kutoka nyumba yake, ichongwe upande mmoja na atumbuliwe nayo. Kwa ajili ya kosa hili nyumba yake ifanywe lundo la taka. 126:12 Kut 20:24; Kum 12:11; 1Fal 9:3; 2Nya 7:16; Za 132:13Naye Mungu, aliyeliweka Jina lake huko, amwangushe mfalme yeyote au watu watakaoinua mikono kubadili amri hii au kuharibu Hekalu hili lililoko Yerusalemu.

Mimi Dario nimetoa amri hii. Nayo itekelezwe kwa bidii na kwa makini.

Jengo Linakamilika Na Kuwekwa Wakfu

136:13 Ay 5:12; Ezr 4:9; Za 9:16; 1Kor 3:19Kwa sababu ya amri aliyotoa Mfalme Dario, Tatenai mtawala wa Ngʼambo ya Mto Frati na Shethar-Bozenai na wenzao wakaitekeleza kwa bidii na kwa makini. 146:14 Ezr 5:1; 7:1; Neh 2:1; Ezr 4:24Hivyo wazee wa Wayahudi waliendelea kujenga na kustawi kutokana na mahubiri ya manabii Hagai na Zekaria, mwana wa Ido. Wakakamilisha ujenzi wa Hekalu kulingana na agizo la Mungu wa Israeli na amri ya Koreshi, Dario na Artashasta wafalme wa Uajemi. 156:15 Zek 4:9Hekalu lilikamilika siku ya kumi na mbili ya mwezi wa Adari, ndio mwezi wa tatu, katika mwaka wa sita wa utawala wa Mfalme Dario.

166:16 1Fal 8:63; 2Nya 7:15; Yn 10:22Kisha watu wa Israeli: makuhani, Walawi na wengine wote waliohamishwa, wakaadhimisha kule kuwekwa wakfu nyumba ya Mungu kwa shangwe. 176:17 2Sam 6:13; 1Nya 16:1-3; 2Nya 29:21; Hes 7:2-3; Ezr 8:25Kwa ajili ya kuwekwa wakfu nyumba hii ya Mungu walitoa mafahali mia moja, kondoo dume mia mbili, wana-kondoo mia nne, sadaka kwa ajili ya dhambi ya Israeli yote walitoa mbuzi dume kumi na wawili, mmoja kwa ajili ya kila kabila la Israeli. 186:18 1Nya 24:1; 23:6; Hes 3:6-9; 8:9-11Wakawaweka makuhani katika nafasi zao na Walawi wakawekwa katika makundi yao ya huduma kwa Mungu huko Yerusalemu, kulingana na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Mose.

Pasaka

196:19 Kut 12:11; Hes 28:16Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, waliorudi kutoka uhamishoni wakaadhimisha Pasaka. 206:20 2Nya 30:15-17; 35:11; Kut 12:25; 2Nya 29:34Makuhani na Walawi walikuwa wamekwisha kujitakasa nao wamekuwa safi kwa kufuata kawaida za ibada. Walawi wakachinja kondoo wa Pasaka kwa ajili ya wana wa waliorudi kutoka utumwani uhamishoni, kwa ajili ya ndugu zao makuhani na wao wenyewe. 216:21 Kut 12:48; Za 93:5Hivyo Waisraeli waliokuwa wamerudi kutoka utumwani uhamishoni wakaila Pasaka, pamoja na wale waliokuwa wamejitenga na matendo ya unajisi wa Mataifa ya jirani ili kumtafuta Bwana, Mungu wa Israeli. 226:22 Kut 12:17; Mit 21:1; Ezr 1:1Kwa muda wa siku saba waliiadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa furaha, kwa sababu Bwana alikuwa amewajaza furaha kwa kubadilisha nia ya mfalme wa Ashuru kwamba awasaidie ujenzi wa nyumba ya Mungu, Mungu wa Israeli.