以斯帖記 4 – CCBT & NEN

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以斯帖記 4:1-17

末底改求以斯帖幫忙

1末底改得知這事,就撕裂衣服,披上麻衣,頭蒙灰塵,在城中行走,放聲痛哭, 2一直走到宮門前才停住,因為穿麻衣的不可進宮門。 3王的命令和諭旨傳到各省,各地的猶太人極其悲傷,他們禁食、哭泣、哀號,許多人身披麻衣躺在灰中。

4以斯帖王后的宮女和太監把這事稟告她,她非常難過,便為末底改送去衣服,讓他換下麻衣,他卻不肯接受。 5於是,以斯帖把王派來服侍她的一個名叫哈他革的太監召來,叫他去見末底改,查明事情的原委。 6哈他革就到宮門前的廣場見末底改7末底改便將自己的遭遇及哈曼為滅絕猶太人而捐入國庫的銀子數目都告訴了他。 8末底改還把一份在書珊城頒佈的要消滅猶太人的諭旨抄本交給哈他革,讓他給以斯帖看,並囑咐她去見王,為自己的同胞向王求情。 9哈他革回去把末底改的話告訴以斯帖10以斯帖便吩咐哈他革回覆末底改說: 11「王的所有臣僕和各省人民都知道有一條法令,不論男女,未蒙宣召擅入內院去見王的必被處死,除非王向他伸出金杖,他才能活命。現在我已有三十天未蒙王召見了。」

12末底改聽到以斯帖捎來的話後, 13便回覆她說:「你別以為在宮裡就比其他猶太人安全。 14如果此時你閉口不語,猶太人必從別處得解脫,蒙拯救,但你和你父親一家必滅亡。誰知道你得了王后之位不是為了今日之時呢?」

15以斯帖派人回覆末底改說: 16「你去召集書珊城所有的猶太人為我禁食,三天三夜不吃不喝,我和我的宮女也要這樣禁食。然後,我要違例去見王,我若死就死吧。」

17於是,末底改便去照以斯帖的一切吩咐行事。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Esta 4:1-17

Mordekai Amshawishi Esta Kusaidia

14:1 Eze 27:30-31; Za 30:11Mordekai alipojua yote yaliyokwisha kufanyika, alirarua mavazi yake na kuvaa nguo za magunia na kujipaka majivu, akaenda mjini, akiomboleza kwa sauti na kwa uchungu. 2Alikwenda akasimama nje ya lango la mfalme, kwa sababu hakuna yeyote aliyeruhusiwa kuingia akiwa amevaa nguo za magunia. 3Katika kila jimbo ambapo amri na agizo la mfalme lilifika, kulikuwa na maombolezo makuu miongoni mwa Wayahudi pamoja na kufunga, kulia na kuomboleza. Watu wengi wakalala juu ya nguo za magunia na majivu.

4Wajakazi wa Esta na matowashi walipokuja na kumwambia kuhusu Mordekai, alipatwa na huzuni kuu. Alimtumia nguo avae badala ya nguo za magunia, lakini Mordekai hakuzikubali. 5Ndipo Esta akamwita Hathaki, mmojawapo wa matowashi wa mfalme ambaye alikuwa amewekwa kumhudumia Esta, akamwagiza kutafuta ni nini kilikuwa kikimtaabisha Mordekai na ni kwa nini.

6Basi Hathaki alitoka nje kumwendea Mordekai kwenye uwanja ulio wazi wa mji mbele ya lango la mfalme. 74:7 Es 7:4Mordekai akamwambia kila kitu ambacho kimempata, pamoja na hesabu kamili ya fedha ambazo Hamani aliahidi kulipa katika hazina ya mfalme kwa ajili ya maangamizi ya Wayahudi. 8Akampa nakala ya andiko la amri kwa ajili ya maangamizi yao, lililokuwa limechapishwa huko Shushani, kumwonyesha Esta na kumwelezea. Mordekai akamwambia towashi amshawishi Esta kwenda mbele ya mfalme kuomba rehema na kumsihi kwa ajili ya watu wake.

9Hathaki akarudi kwa Esta na kumwarifu alilolisema Mordekai. 10Kisha Esta akamwamuru Hathaki amweleze Mordekai, 114:11 Dan 2:9; Za 125:3“Maafisa wote wa mfalme na watu wa majimbo ya ufalme wanajua kuwa mwanaume au mwanamke yeyote ambaye ataingia kumwona mfalme katika ua wa ndani bila kuitwa, mfalme ana sheria moja tu: Atauawa. Njia pekee kinyume na hili ni mfalme kumnyooshea fimbo ya dhahabu ili aishi. Lakini siku thelathini zimepita tangu nilipoitwa kwenda kwa mfalme.”

12Wakati Mordekai aliarifiwa maneno ya Esta, 13Mordekai alirudisha jibu hili: “Usifikiri kwamba kwa sababu uko katika nyumba ya mfalme wewe pekee katika Wayahudi wote utapona. 144:14 Ay 34:29; Mhu 3:7; Amo 5:13Kwa kuwa kama utakaa kimya wakati huu, msaada na ukombozi kwa Wayahudi utatoka mahali pengine, lakini wewe na jamaa ya baba yako mtaangamia. Nani ajuaye kwamba hukuja kwenye nafasi ya mamlaka kwa ajili ya wakati kama huu?”

15Kisha Esta alituma jibu hili kwa Mordekai: 164:16 2Nya 20:3; Mwa 43:14“Nenda, kusanya pamoja Wayahudi wote walioko Shushani, nanyi mfunge kwa ajili yangu. Msile wala kunywa kwa siku tatu, usiku na mchana. Mimi na wajakazi wangu tutafunga kama mnavyofanya. Baada ya kufanyika hili, nitakwenda kwa mfalme, hata ingawa ni kinyume cha sheria. Ikiwa ni kuangamia na niangamie.”

17Kwa hiyo Mordekai alikwenda zake na kutekeleza maagizo yote ya Esta.