马可福音 5 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

马可福音 5:1-43

治好被鬼附身的人

1他们来到湖对岸的格拉森地区。 2耶稣刚下船,就遇见一个被污鬼附身的人从坟场迎面而来。 3那人以坟场为家,从来没有人能把他捆住,就算用铁链也锁不住他。 4尽管有人多次用铁链和脚镣锁住他,但他挣断了铁链,砸碎了脚镣。没有人能制服他。 5他昼夜在坟场和山野间大喊大叫,又用石头砍自己。

6他远远看见耶稣,就跑过去跪下来拜祂,喊着说: 7“至高上帝的儿子耶稣啊,我和你有什么关系?看在上帝的份上,求你不要折磨我!” 8原来,耶稣已经对他身上的鬼说:“污鬼,从这人身上出来!”

9耶稣问:“你叫什么名字?”

他说:“我的名字叫‘群’,因为我们是一大群。”

10接着污鬼再三哀求耶稣,不要把它们逐出那个地区。 11当时有一大群猪在附近山坡上觅食。 12污鬼就哀求耶稣说:“让我们到猪群里去,附在它们身上吧!”

13耶稣允许了,污鬼就离开那人,进入猪群。那群猪就一路奔下陡坡,冲进湖里淹死了,约有两千头。

14放猪的人都吓跑了。他们把这消息传遍了城里乡间,于是人人都跑来看个究竟。 15他们到了耶稣那里,看见那一度被群鬼附身的人神智清醒、衣着整齐地坐在那里,都很害怕。 16目睹这件事的人向他们讲述整个经过。 17他们请耶稣离开他们的地方。

18耶稣上了船准备离开的时候,那被鬼附过的人恳求耶稣让他随行。 19耶稣没有答应,只对他说:“回去见你的家人,将主为你所做的事和祂怜悯你的经过告诉他们吧!”

20这人就回到低加坡里一带宣扬耶稣为他所行的奇事,大家都很惊奇。

耶稣医治有信心的人

21耶稣再坐船回到对岸,立刻有一大群人在岸边围着祂。 22人群中有一位会堂的主管名叫雅鲁,他一见到耶稣便俯伏在祂脚前, 23恳求说:“我小女儿快要死了,求你去把手按在她身上,医治她,救她一命。”

24耶稣和他同去,一大群人跟着祂,拥挤着祂。

25有一个妇人患血漏病已经十二年, 26经过许多医生的诊治,受尽痛苦,耗尽钱财,病情仍没有好转,反而更加严重。 27她听见耶稣的事,就夹在人群中挤到耶稣背后摸祂的衣服, 28心想:“只要摸到祂的衣服,我就痊愈了!”

29她的血漏立刻停止了,她感到自己痊愈了。 30耶稣马上知道有能力从自己身上发出,便在人群中转过身来问:“谁摸了我的衣服?”

31门徒对祂说:“你看,这么多人在你周围挤来挤去,你怎么问谁摸你呢?”

32耶稣环视四周,要找出摸祂的人。 33那妇人害怕得发抖,她知道在自己身上发生了什么事,于是上前俯伏在耶稣面前,将实情说了出来。

34耶稣说:“女儿,你的信心救了你。安心地回去吧!你的病好了。”

35耶稣还在说话的时候,有人从雅鲁家中赶来,对雅鲁说:“你的女儿已经死了,何必麻烦老师呢?”

36耶稣听了,便对雅鲁说:“不要怕,只要信。” 37于是,祂带着彼得雅各雅各的弟弟约翰雅鲁家,不准其他人跟着。 38他们到了那里,只见在场的人嚎啕大哭,场面混乱。 39耶稣进去问道:“你们为什么大哭大嚷呢?这孩子并没有死,只是睡着了。”

40这些人听了,都讥笑祂。耶稣让他们全部出去,然后带着孩子的父母和三个门徒进了房间。 41祂拉着孩子的手说:“大利大,古米!”意思是:“小女孩,我吩咐你起来!”

42小女孩应声而起,并且可以走动,那时她十二岁。在场的人都惊奇不已。 43耶稣郑重叮嘱他们不要把这事张扬出去,又吩咐他们给女孩东西吃。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Marko 5:1-43

Yesu Amponya Mtu Mwenye Pepo

(Mathayo 8:28-34; Luka 8:26-39)

15:1 Mt 8:28; Mk 8:26Wakafika upande wa pili wa ziwa wakaingia katika nchi ya Wagerasi. 25:2 Mk 4:1; 1:23Yesu alipotoka kwenye mashua, mara mtu mmoja mwenye pepo mchafu akatoka makaburini akakutana naye. 3Mtu huyu aliishi makaburini, wala hakuna aliyeweza kumzuia hata kwa kumfunga minyororo. 4Kwa kuwa mara kwa mara alikuwa amefungwa minyororo mikononi na miguuni, lakini akaikata hiyo minyororo na kuzivunja zile pingu miguuni mwake. Hapakuwa na mtu yeyote aliyekuwa na nguvu za kumzuia. 5Usiku na mchana alikuwa makaburini na milimani, akipiga kelele na kujikatakata kwa mawe.

6Alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia, akapiga magoti mbele yake. 75:7 Mt 8:29; Mdo 16:17; Ebr 7:1Akapiga kelele kwa nguvu akisema, “Una nini nami, Yesu, Mwana wa Mungu Aliye Juu Sana? Ninakusihi kwa jina la Mungu, usinitese!” 8Kwa kuwa Yesu alikuwa amemwambia, “Mtoke mtu huyu, wewe pepo mchafu!”

9Yesu akamuuliza, “Jina lako ni nani?”

Akamjibu, “Jina langu ni Legioni,5:9 Legioni maana yake ni Jeshi. kwa kuwa tuko wengi.” 10Akamsihi Yesu sana asiwapeleke nje ya nchi ile.

11Palikuwa na kundi kubwa la nguruwe lililokuwa likilisha karibu kando ya kilima. 12Wale pepo wachafu wakamsihi Yesu wakisema, “Tuamuru twende kwenye wale nguruwe. Turuhusu tuwaingie.” 13Basi Yesu akawaruhusu, nao wale pepo wachafu wakatoka, wakawaingia hao nguruwe. Lile kundi lilikuwa na nguruwe wapatao 2,000, nao wote wakateremkia gengeni kwa kasi, nao wakatumbukia ziwani na kuzama.

14Wale watu waliokuwa wakichunga hao nguruwe wakakimbilia mjini na vijijini kueleza yaliyotukia. Watu wakatoka kwenda kuona hayo yaliyokuwa yametukia. 155:15 Mk 5:9; 5:18-19; 4:24Walipofika kwa Yesu, wakamwona yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu legioni akiwa ameketi hapo, amevaa nguo na mwenye akili timamu. Wakaogopa. 16Wale walioyaona mambo hayo wakawaeleza watu wengine yaliyomtokea yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu, na habari za lile kundi la nguruwe pia. 175:17 Mt 8:34; Mdo 16:39Basi watu wakaanza kumwomba Yesu aondoke katika nchi yao.

185:18 Lk 8:38Yesu alipokuwa anaingia kwenye mashua, yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu akamsihi Yesu waende pamoja. 195:19 Mt 8:4Yesu hakumruhusu, bali alimwambia, “Nenda nyumbani kwa jamaa yako ukawaeleze mambo makuu aliyokutendea Bwana, na jinsi alivyokuhurumia.” 205:20 Mt 4:25; Mk 7:31Yule mtu akaenda zake, akaanza kutangaza katika Dekapoli mambo makuu Yesu aliyomtendea. Nao watu wote wakastaajabu.

Mwanamke Aponywa

(Mathayo 9:18-26; Luka 8:40-56)

215:21 Mt 9:1; Mk 4:1Yesu alipokwisha kuvuka tena na kufika ngʼambo, umati mkubwa wa watu ukamzunguka yeye akiwa hapo kando ya bahari. 225:22 Lk 13:14; Mdo 13:15Kisha mmoja wa viongozi wa sinagogi aliyeitwa Yairo akafika pale. Naye alipomwona Yesu, akapiga magoti miguuni pake, 235:23 Mt 19:13akamsihi akisema, “Binti yangu mdogo ni mgonjwa mahututi. Tafadhali nakusihi, njoo uweke mikono yako juu yake ili apate kupona, naye atakuwa hai.” 24Hivyo Yesu akaenda pamoja naye.

Umati mkubwa wa watu ukamfuata, nao watu wakawa wanamsonga. 255:25 Law 15:25-30Hapo palikuwa na mwanamke aliyekuwa amesumbuliwa na tatizo la kutokwa damu kwa miaka kumi na miwili. 26Mwanamke huyu alikuwa ameteseka sana kwa mikono ya matabibu wengi, na kutumia kila kitu alichokuwa nacho. Lakini badala ya kupona, hali yake ilizidi kuwa mbaya. 27Alikuwa amesikia habari za Yesu, naye akaja kwa nyuma yake kwenye umati wa watu, akaligusa vazi lake, 285:28 Mt 5:20kwa maana alisema moyoni mwake, “Kama nikiweza kuligusa vazi lake tu, nitaponywa.” 295:29 Mk 5:34Mara kutoka damu kwake kukakoma, naye akajisikia mwilini mwake amepona kabisa.

305:30 Lk 5:17; 6:19Ghafula Yesu akatambua kuwa nguvu zimemtoka. Akaugeukia ule umati wa watu na kuuliza, “Ni nani aliyegusa mavazi yangu?”

31Wanafunzi wake wakamjibu, “Unaona jinsi umati wa watu unavyokusonga. Wawezaje kuuliza, ‘Ni nani aliyenigusa?’ ”

32Lakini Yesu akaangalia pande zote ili aone ni nani aliyemgusa. 33Yule mwanamke, akijua kilichomtokea, akaja, akaanguka miguuni pake akitetemeka kwa hofu, akamweleza ukweli wote. 345:34 Mt 9:22; Mdo 15:33Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako.”

Yesu Amfufua Binti Yairo

355:35 Mk 5:22Alipokuwa bado anaongea, watu wakafika kutoka nyumbani kwa Yairo. Wakamwambia, “Binti yako amekufa. Kwa nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?”

36Aliposikia hayo waliyosema, Yesu akamwambia huyo kiongozi wa sinagogi, “Usiogope. Amini tu.”

375:37 Mt 4:21Hakumruhusu mtu mwingine yeyote amfuate isipokuwa Petro, Yakobo na Yohana, nduguye Yakobo. 385:38 Mt 5:22Walipofika nyumbani kwa yule kiongozi wa sinagogi, Yesu akaona ghasia, watu wakilia na kuomboleza kwa sauti kubwa. 395:39 Mt 9:24Alipokwisha kuingia ndani, akawaambia, “Kwa nini mnafanya ghasia na kulia? Mtoto hajafa, bali amelala tu.” 405:40 Mdo 9:40Wale watu wakamcheka kwa dharau.

Lakini yeye akawatoa wote nje, akawachukua baba na mama wa yule mtoto, pamoja na wale wanafunzi aliokuwa nao. Wakaingia ndani mpaka pale alipokuwa yule mtoto. 415:41 Mk 1:31; Lk 7:14; Mdo 9:40Akamshika mtoto mkono, akamwambia, “Talitha koum!” 5:41 Talitha koum ni lugha ya Kiaramu. (maana yake ni, “Msichana, nakuambia: amka!”) 42Mara yule msichana akasimama, akaanza kutembea (alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili). Walipoona haya, wakastaajabu sana. 435:43 Mt 8:4Yesu akawaagiza kwa ukali wasimweleze mtu yeyote jambo hilo, naye akawaambia wampe yule msichana chakula.