雅各书 4 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

雅各书 4:1-17

不要与世俗为友

1你们彼此冲突、互相斗殴的起因是什么呢?不就是你们身体中不断交战的欲望吗? 2你们贪心,得不到就去杀人。你们嫉妒,得不到就争吵、打斗。你们得不到是因为你们不向上帝祈求。 3你们求也得不到是因为你们动机不纯,只求享乐和满足自己的欲望。 4你们这些对主不忠的人啊,难道还不明白与世俗为友就是与上帝为敌吗?所以,凡是与世俗为友的,都是上帝的敌人。 5圣经上说:“上帝所赐、住在我们心里的圣灵深愿我们完全属于祂。”你们以为这是空谈吗? 6但上帝赐给我们更大的恩典,所以圣经上说:“上帝阻挡骄傲的人,恩待谦卑的人。”

7因此,你们要服从上帝,抵挡魔鬼,魔鬼必逃离你们。 8你们亲近上帝,上帝就必亲近你们。有罪的人啊,洗净你们的手吧!三心二意的人啊,洁净你们的心吧! 9你们要悲伤、忧愁、痛哭,转欢笑为悲哀,变欢乐为愁苦。 10你们要在主面前谦卑,祂必擢升你们。

不要论断

11弟兄姊妹,不要彼此批评。批评、论断弟兄姊妹就等于是批评、论断律法。如果你论断律法,你就不是遵行律法的人,而是以审判者自居。 12设立律法和审判人的只有一位,就是能拯救人也能毁灭人的上帝。你是谁,竟然论断别人呢?

警戒自夸

13你们有些人说:“今天或是明天,我们要往某某城去,在那里逗留一年半载,做生意赚钱。” 14其实你们根本不知道明天会发生什么事。你们的生命是什么呢?你们只不过像一阵雾气,出现片刻,就无影无踪了。 15你们只当说:“如果主许可,我们就可以活着,可以做这事或做那事。” 16现在,你们竟敢傲慢自夸,这实属邪恶。 17所以人若知道善而不去行,就是犯罪。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yakobo 4:1-17

Jinyenyekezeni Kwa Mungu

14:1 Tit 3:9; Rum 7:23Ni kitu gani kinachosababisha mapigano na ugomvi miongoni mwenu? Je, haya hayatokani na tamaa zenu zinazoshindana ndani yenu? 24:2 Mt 5:21, 22; Yak 5:6; 1Yn 3:15Mnatamani lakini hampati, kwa hiyo mwaua. Mwatamani kupata lakini hampati vile mnavyotaka, kwa hiyo mnajitia katika magomvi na mapigano. Mmepungukiwa kwa sababu hammwombi Mungu. 34:3 Mt 7:7; Za 66:18; 1Yn 5:14Mnapoomba hampati kwa sababu mnaomba kwa nia mbaya, ili mpate kuvitumia hivyo mtakavyopata kwa tamaa zenu.

44:4 Yak 1:27; Rum 8:7; Yn 15:19Ninyi wanaume na wanawake wazinzi, hamjui ya kwamba urafiki na dunia ni uadui na Mungu? Kwa hiyo mtu yeyote anayetaka kuwa rafiki wa dunia hufanyika adui wa Mungu. 54:5 1Kor 6:19; Mwa 6:5; 8:21; Hes 11:29; Mit 21:10Au mwadhani kwamba Andiko lasema bure kuwa huyo Roho ambaye Mungu amemweka ndani yetu hututamani kiasi cha kuona wivu? 64:6 Za 138:6; Mt 23:12Lakini yeye hutupatia neema zaidi. Hii ndiyo sababu Andiko husema:

“Mungu huwapinga wenye kiburi,

lakini huwapa wanyenyekevu neema.”

74:7 Efe 6:11; 1Pet 5:6-9Basi mtiini Mungu. Mpingeni ibilisi, naye atawakimbia. 84:8 Ebr 7:19; Isa 1:16; Za 119:113Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu ninyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu ninyi wenye nia mbili. 94:9 Lk 6:25; Mt 5:4Huzunikeni, ombolezeni na kulia. Kicheko chenu na kigeuzwe kuwa kuomboleza, na furaha yenu kuwa huzuni. 104:10 Ay 22:29; Mt 23:12; Lk 14:11; 1Pet 5:6Jinyenyekezeni mbele za Bwana, naye atawainua.

Onyo Kuhusu Kuhukumu Wengine

114:11 Rum 1:30; 2Kor 12:20; Mt 7:1; Yak 1:22Ndugu, msineneane mabaya ninyi kwa ninyi. Mtu yeyote anayesema mabaya dhidi ya ndugu yake au kumhukumu anasema dhidi ya sheria na kuihukumu. Unapoihukumu sheria, basi huishiki sheria bali umekuwa hakimu wa kuihukumu hiyo sheria. 124:12 Mt 10:28; 7:1Yuko Mtoa sheria mmoja tu na yeye peke yake ndiye Hakimu, ndiye awezaye kuokoa au kuangamiza. Lakini wewe ni nani hata umhukumu jirani yako?

Kujivuna Kwa Ajili Ya Kesho

134:13 Lk 12:18-20Basi sikilizeni ninyi msemao, “Leo au kesho tutakwenda katika mji huu ama ule tukae humo mwaka mmoja, tufanye biashara na kupata faida.” 144:14 Za 39:5; Isa 2:22Lakini hamjui hata litakalotukia kesho. Maisha yenu ni nini? Ninyi ni ukungu ambao huonekana kwa kitambo kidogo kisha hutoweka. 154:15 Mdo 18:21Badala yake, inawapasa kusema, “Kama Bwana akipenda, tutaishi na kufanya hili ama lile.” 164:16 1Kor 5:6Kama ilivyo sasa, mnajisifu na kujigamba. Kujisifu kwa namna hiyo ni uovu. 174:17 Lk 12:47; Yn 9:41Basi mtu yeyote anayejua jema limpasalo kutenda, lakini asilitende, mtu huyo anatenda dhambi.