诗篇 17 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

诗篇 17:1-15

第 17 篇

无辜者的祈祷

大卫的祈祷。

1耶和华啊,

求你听我祈求公义的声音,

侧耳听我的呼求,

垂听我真诚的祷告。

2愿你宣判我无罪,

愿你明察是非。

3你试验过我的心思,

夜间鉴察过我,磨炼过我,

找不出任何过犯;

我立志口不犯罪。

4我遵守你的教导,洁身自守,

不与残暴之徒同流。

5我坚定地走你的道路,

从未偏离。

6上帝啊!我向你祈祷,

因为你必应允我。

求你垂听我的祷告。

7求你彰显你奇妙的慈爱,

用右手拯救投靠你的人脱离仇敌。

8求你保护我,像保护眼中的瞳仁,

用你的翅膀荫庇我,

9救我脱离恶人的攻击,

脱离四围杀气腾腾的仇敌。

10他们良心丧尽,口出狂言。

11他们穷追围堵,

伺机把我打倒在地。

12他们像急于撕碎猎物的饿狮,

又像蹲伏在暗处的猛狮。

13耶和华啊,

求你起来迎头击倒他们,

求你持刀救我脱离恶人。

14耶和华啊,

求你伸手救我脱离这些人,

脱离这些只在今生有福分的世人。

你使他们财宝无数。

他们儿女众多,

还把财富留给子孙。

15但我因持守公义必见你的面;

我醒来见到你就心满意足了。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 17:1-15

Zaburi 17

Sala Ya Mtu Asiye Na Hatia

Sala ya Daudi.

117:1 Za 30:10; 64:1; 80:1; 140:6; 5:1, 2; 39:12; 142:6; 143:1; Isa 29:13Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki,

sikiliza kilio changu.

Tega sikio kwa ombi langu,

halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.

217:2 Za 24:5; 26:1; 99:4; Isa 46:13; 50:8-9; 54:17Hukumu yangu na itoke kwako,

macho yako na yaone yale yaliyo haki.

317:3 Za 139:1; Yak 3:2; Ay 7:18; 23:10; Yer 12:3; 50:20Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku,

ingawa umenijaribu, hutaona chochote.

Nimeamua kwamba kinywa changu

hakitatenda dhambi.

417:4 Rum 12:2Kuhusu matendo ya wanadamu:

kwa neno la midomo yako,

nimejiepusha

na njia za wenye jeuri.

517:5 Ay 23:11; Za 44:18; 73:2; 121:3; Kum 32:35Hatua zangu zimeshikamana na njia zako;

nyayo zangu hazikuteleza.

617:6 Za 84:7; 116:2; 4:1Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu,

nitegee sikio lako na usikie ombi langu.

717:7 Za 31:21; 69:13; 106:45; 107:43; 117:2; 10:12; 2:12Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu,

wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume

wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.

817:8 Hes 6:24; Isa 34:15; Kum 32:10; Mit 7:2; Za 27:5; 31:20; 32:7; 36:7; 63:7; Rum 2:12Nilinde kama mboni ya jicho lako,

unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako

917:9 Za 109:3kutokana na waovu wanaonishambulia,

kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.

1017:10 Za 73:7; 119:70; Isa 6:10; 2:3Huifunga mioyo yao iliyo migumu,

vinywa vyao hunena kwa majivuno.

1117:11 Za 88:17; 1Sam 23:26Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira,

wakiwa macho, waniangushe chini.

1217:12 Za 7:2; Yer 5:6; 12:8; Mao 3:10; Mwa 49:9Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye,

kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.

1317:13 Za 35:8; 55:23; 73:18; Hes 10:3Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe,

niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.

1417:14 Za 49:17; Lk 16:8, 25; Isa 2:7; 57:17Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii,

kutokana na watu wa ulimwengu huu

ambao fungu lao liko katika maisha haya.

Na wapate adhabu ya kuwatosha.

Watoto wao na wapate zaidi ya hayo,

hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.

1517:15 Za 3:5; Hes 12:2; Mt 5:8; 1Yn 3:2Na mimi katika haki nitauona uso wako,

niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.