罗马书 15 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

罗马书 15:1-33

我为人人

1我们坚强的人要扶助软弱的人,分担他们的重担,不该只顾自己的喜好。 2我们每个人都应该为他人着想,建造他人的生命。 3因为基督并没有专顾自己,正如圣经上说:“辱骂你之人的辱骂都落在我身上。” 4从前写在圣经上的话都是为了教导我们,使我们靠着忍耐和圣经的鼓励而有盼望。 5但愿赐忍耐和鼓励的上帝给你们合一的心去效法基督耶稣的榜样, 6使你们一起同声颂赞上帝——我们主耶稣基督的父。

7所以,你们应该像基督接纳你们一样彼此接纳,使上帝得荣耀。 8你们要知道,基督为了上帝的真理成为犹太15:8 犹太”希腊文是“受割礼之人”。的仆人,好实现上帝对犹太人祖先们的应许, 9使外族人也因祂的怜悯而将荣耀归给上帝。正如圣经上说:

“因此,我要在列邦中赞美你,

歌颂你的名。”

10又说:

“外族人啊,

你们当与主的子民一同欢乐。”

11又说:

“万邦啊,你们当赞美主!

万民啊,你们当颂赞祂!”

12以赛亚先知也说:

“将来耶西的根要兴起,

祂要统治外族,

外族人都要仰望祂。”

13愿使人有盼望的上帝,因为你们信祂,将诸般的喜乐和平安充满你们的心,使你们借着圣灵的能力充满盼望!

福音特使

14弟兄姊妹,我知道你们充满良善,知识全备,能彼此劝导。 15但我仍放胆写信提醒你们几件事,因为我蒙上帝赐恩, 16在外族人中做基督耶稣的仆人和上帝福音的祭司,好叫外族人借着圣灵得以圣洁,可以作上帝喜悦的祭物。 17因此,我在基督耶稣里以事奉上帝为荣。 18-19别的事我不敢提,只有一件是我津津乐道的,就是基督借着我的言语行为,用神迹奇事和圣灵的大能叫外族人顺服,使我把基督的福音从耶路撒冷一路传到了以利哩古。 20我立志只去从未听过基督之名的地方传福音,免得我建造在别人的根基上。 21正如圣经上说:“对祂毫无所闻的,将要看见;未曾听过的,将要明白。”

保罗计划去罗马

22因此,我一直受到拦阻,不能到你们那里。 23但如今福音传遍了这一带,况且我几年来一直盼望去你们那里, 24所以我想去西班牙的途中路过你们那里,稍作停留,享受与你们的相聚之乐,然后由你们资助我上路。 25但现在我要去耶路撒冷服侍当地的圣徒, 26因为马其顿亚该亚的教会欣然捐出了财物给耶路撒冷的穷困圣徒。 27这固然是他们慷慨解囊,但也可以说是他们该还的债。外族人既然分享了犹太圣徒属灵的福分,现在以物质报答他们也是应该的。 28等我办完这件事,将捐款交付他们之后,我就会途经你们那里去西班牙29我知道我去的时候,必会把基督丰盛的祝福带给你们。

30弟兄姊妹,我借着我们主耶稣基督和圣灵所赐的爱心,恳求你们与我一同竭力祷告,为我祈求上帝, 31使我脱离犹太地区不信之人的迫害,叫耶路撒冷的圣徒乐意接受我带去的捐款, 32并使我按照上帝的旨意欢然去与你们相聚,一同重新得力。

33愿赐平安的上帝常与你们同在。阿们!

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Warumi 15:1-33

Usijipendeze Mwenyewe, Bali Wapendeze Wengine

115:1 Rum 14:1; 1The 5:14Sisi tulio na nguvu, hatuna budi kuchukuliana na kushindwa kwa wale walio dhaifu wala si kujipendeza nafsi zetu wenyewe. 215:2 1Kor 10:33Kila mmoja wetu inampasa kumpendeza jirani yake kwa mambo mema, ili kumjenga katika imani. 315:3 2Kor 8:9; Za 69:9Kwa maana hata Kristo hakujipendeza mwenyewe, bali kama ilivyoandikwa: “Matukano yao wale wanaokutukana wewe yalinipata mimi.” 415:4 Rum 4:23, 24; 1Kor 10:11; 9:9, 10; 10:11; 2Tim 3:16, 17Kwa maana kila kitu kilichoandikwa zamani, kiliandikwa kutufundisha, ili kwamba kwa saburi na faraja tunayopata katika Maandiko tuwe na tumaini.

515:5 2Kor 13:11; Efe 4:3Mungu atoaye saburi na faraja, awajalie ninyi roho ya umoja miongoni mwenu mnapomfuata Kristo Yesu, 615:6 Ufu 1; 6; Za 34:3; Mdo 4:24, 32ili kwa moyo mmoja mpate kumtukuza Mungu aliye Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo.

Injili Sawa Kwa Wayahudi Na Kwa Watu Wa Mataifa

715:7 Rum 14:1; 5:2Karibishaneni ninyi kwa ninyi kama Kristo alivyowakaribisha ninyi ili kumletea Mungu utukufu. 815:8 Mt 15:24; Mdo 3:25, 26; 2Kor 1:20Kwa maana nawaambia kwamba, Kristo amekuwa mtumishi kwa wale waliotahiriwa ili kuonyesha kweli ya Mungu na kuthibitisha zile ahadi walizopewa baba zetu wa zamani, 915:9 Rum 3:29; Mt 9:8; 2Sam 22:50; Za 18:49pia ili watu wa Mataifa wamtukuze Mungu kwa rehema zake. Kama ilivyoandikwa:

“Kwa hiyo nitakutukuza katikati ya watu wa Mataifa;

nitaliimbia sifa jina lako.”

1015:10 Kum 32:43Tena yasema,

“Enyi watu wa Mataifa, furahini

pamoja na watu wa Mungu.”

1115:11 Za 117:1Tena,

“Msifuni Bwana, ninyi watu wa Mataifa wote,

na kumwimbia sifa, enyi watu wote.”

1215:12 Ufu 5:5; Isa 11:10; Mt 12:21Tena Isaya anasema,

“Shina la Yese litachipuka,

yeye atakayeinuka ili kutawala juu ya mataifa.

Watu wa Mataifa watamtumaini.”

1315:13 Rum 14:17; 1Kor 4:20Mungu wa tumaini awajaze ninyi furaha yote na amani katika kumwamini, ili mpate kujawa na tumaini tele kwa nguvu ya Roho Mtakatifu.

Paulo Mhudumu Wa Watu Wa Mataifa

1415:14 Efe 5:9; 2Pet 1:12Ndugu zangu, mimi mwenyewe ninasadiki kwamba mmejaa wema na ufahamu wote, tena mnaweza kufundishana ninyi kwa ninyi. 1515:15 Rum 12:3; 1:5; 12:3; Gal 1:15; Efe 3:7, 8Nimewaandikia kwa ujasiri vipengele kadha wa kadha katika waraka huu kama kuwakumbusha tena kwa habari ya ile neema Mungu aliyonipa, 1615:16 Mdo 9:5; Rum 11:13; 1:1; Isa 66:20ili kuwa mhudumu wa Kristo Yesu kwa watu wa Mataifa nikiwa na huduma ya kikuhani ya kutangaza Injili ya Mungu, ili watu wa Mataifa wapate kuwa dhabihu inayokubaliwa na Mungu, iliyotakaswa na Roho Mtakatifu.

1715:17 Flp 3:3; Ebr 2:17Kwa hiyo ninajisifu katika Kristo Yesu, kwenye utumishi wangu kwa Mungu. 1815:18 Mdo 15:12; Rum 1:15; 16:26Kwa maana sitathubutu kusema kitu chochote zaidi ya kile ambacho Kristo amefanya kwa kunitumia mimi katika kuwaongoza watu wa Mataifa wamtii Mungu kwa yale niliyosema na kufanya, 1915:19 Yn 4:48; Mdo 19:11; 22:17-21kwa nguvu za ishara na miujiza, kwa uweza wa Roho wa Mungu, hivyo kuanzia Yerusalemu hadi maeneo yote ya kandokando yake mpaka Iliriko, nimekwisha kuihubiri Injili ya Kristo kwa ukamilifu. 2015:20 2Kor 10:15, 16Hivyo ni nia yangu kuhubiri Habari Njema, si pale ambapo Kristo amekwisha kujulikana, ili nisije nikajenga juu ya msingi wa mtu mwingine. 2115:21 Isa 52:15Lakini kama ilivyoandikwa:

“Wale ambao hawajahubiriwa habari zake wataona,

nao wale ambao hawajazisikia watafahamu.”

2215:22 Rum 1:13Hii ndiyo sababu nimezuiliwa mara nyingi nisiweze kuja kwenu.

Paulo Apanga Kwenda Rumi

2315:23 Mdo 19:21; 24:17Lakini sasa kwa kuwa hakuna nafasi zaidi kwa ajili yangu katika sehemu hii, ninatamani kuja kwenu kama ambavyo nimekuwa na shauku kwa miaka mingi. 2415:24 Rum 15:28; 1Kor 16:6; Tit 3:1Nimekusudia kufanya hivyo nitakapokuwa njiani kwenda Hispania. Natarajia kuwaona katika safari yangu na kusafirishwa nanyi mpaka huko, baada ya kufurahia ushirika wenu kwa kitambo kidogo. 2515:25 Mdo 19:21; 24:17Sasa, niko njiani kuelekea Yerusalemu kwa ajili ya kuwahudumia watakatifu huko. 2615:26 Rum 16:9; 2Kor 1:11; Kol 4:12Kwa kuwa imewapendeza watu wa Makedonia na Akaya kufanya changizo kwa ajili ya maskini walioko miongoni mwa watakatifu huko Yerusalemu. 2715:27 1Kor 9:11; Rum 9:4; 11:17; Gal 6:6Imewapendeza kufanya hivyo, naam, kwani ni wadeni wao. Kwa maana ikiwa watu wa Mataifa wameshiriki baraka za rohoni za Wayahudi, wao ni wadeni wa Wayahudi, ili Wayahudi nao washiriki baraka zao za mambo ya mwilini. 2815:28 Flp 4:17; Rum 15:24Kwa hiyo baada ya kukamilisha kazi hii na kuhakikisha kuwa wamepokea kila kitu kilichokusanywa, nitapitia kwenu nikiwa njiani kwenda Hispania. 2915:29 Rum 1:10; 1:11Ninajua kwamba nitakapokuja kwenu, nitakuja na wingi wa baraka za Kristo.

3015:30 Gal 5:22; 2Kor 1:11; Kol 4:12Basi, ndugu zangu, nawasihi kwa Jina la Bwana wetu Yesu Kristo na kwa upendo wa Roho Mtakatifu, kujiunga nami katika taabu zangu mkiniombea kwa Mungu. 3115:31 2Kor 1:10; 2Tim 3:11Ombeni ili nipate kuokolewa mikononi mwa wale wasioamini walioko Uyahudi, na kwamba utumishi wangu upate kukubaliwa na watakatifu wa huko Yerusalemu, 3215:32 Mdo 18:21; Rum 1:10, 13; 1Kor 16:18ili kwa mapenzi ya Mungu niweze kuja kwenu kwa furaha, nami niburudishwe pamoja nanyi. 3315:33 2The 3:16Mungu wa amani na awe pamoja nanyi nyote. Amen.