约伯记 26 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

约伯记 26:1-14

约伯的回答

1约伯回答说:

2“你真是帮了软弱者的大忙!

救了臂膀无力的人!

3无智慧的人真多亏你的指教!

承蒙你的真知灼见!

4谁帮你想出这些点子?

谁的灵在借着你发言?

5“阴魂和水族在水底战抖,

6阴间在祂面前裸露,

冥府毫无遮掩。

7祂将北极铺在空中,

将地悬在虚无中;

8祂将水卷在密云中,

云负重却不裂开。

9祂遮盖自己的宝座26:9 宝座”或译“满月”。

把云彩铺在上面。

10祂在海面上画出地平线,

作为光明与黑暗的交界。

11祂的斥责使天柱震动惊骇,

12祂的能力使大海平静,

祂运用智慧击碎海怪。

13祂吹散天上的阴霾,

挥手刺穿逃跑的蛇。

14看啊,这不过是祂作为的一斑,

是我们听到的少许回音!

谁能领悟祂的雷霆万钧?”

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 26:1-14

Hotuba Ya Tisa Ya Ayubu

Ayubu Anajibu: Utukufu Wa Mungu Hauchunguziki

1Kisha Ayubu akajibu:

226:2 Ay 6:12; 4:3; Za 71:9; Mit 25:11“Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo!

Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!

326:3 Ay 34:35Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima?

Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!

426:4 1Fal 22:24Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo?

Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?

526:5 Za 88:10; Isa 14:9“Wafu wako katika maumivu makuu,

wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.

626:6 Za 139:8; Mit 15:11; Ebr 4:13; Amo 9:2Mauti26:6 Yaani Kuzimu; Kiebrania ni Sheol. iko wazi mbele za Mungu;

Uharibifu26:6 Kwa Kiebrania ni Abadon. haukufunikwa.

726:7 Ay 9:826:7 Ay 8:22; 31:35Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu;

naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.

826:8 Mit 30:4; Za 147:8Huyafungia maji kwenye mawingu yake,

hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.

926:9 2Sam 22:10; Za 97:2Huufunika uso wa mwezi mpevu,

akitandaza mawingu juu yake.

1026:10 Mit 8:27; Isa 40:22; Ay 28:3Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji,

ameweka mpaka wa nuru na giza.

1126:11 2Sam 22:8Nguzo za mbingu nazo zatetemeka,

zinatishika anapozikemea.

1226:12 Isa 51:15; Kut 14:21; Yer 31:35; Ay 12:13; Kut 14:21; Ay 12:13; 9:13Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari;

kwa hekima yake alimkata Rahabu26:12 Rahabu hapa ni fumbo la kumaanisha Lewiathani, mnyama mkubwa wa baharini mwenye magamba anayefanana na joka kubwa, mwenye umbo la kutisha, asiyeweza kuvuliwa. vipande vipande.

1326:13 Za 33:6; Isa 27:1Aliisafisha anga kwa pumzi yake;

kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.

1426:14 Ay 9:6; 36:29Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake;

tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu!

Ni nani basi awezaye kuelewa

ngurumo za nguvu zake?”