箴言 26 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

箴言 26:1-28

1愚人得尊荣本不合宜,

如夏天降雪、收割时下雨。

2麻雀翻飞,燕子翱翔,

咒诅不会无端降临。

3鞭子打马,缰绳勒驴,

棍棒责打愚人的背。

4别照愚人的愚昧回答他,

免得你像他一样。

5要照愚人的愚昧回答他,

免得他自以为有智慧。

6靠愚人传信,

如同砍断自己的脚,

自讨苦吃。

7愚人口中说箴言,

如同跛子空有腿。

8把尊荣给愚人,

就像把石子绑在甩石器上。

9愚人口中说箴言,

如同醉汉握荆棘。

10雇用愚人或路人,

如同弓箭手乱箭伤人。

11愚人一再重复愚昧事,

就像狗回头吃所吐的。

12自以为有智慧的人,

还不如愚人有希望。

13懒惰人说:“路上有狮子,

街上有猛狮。”

14懒惰人赖在床上滚来滚去,

就像门在门轴上转来转去。

15懒惰人手放在餐盘,

却懒得送食物进嘴。

16懒惰人自以为比七个善于应对的人更有智慧。

17插手他人的纠纷,

犹如揪狗的耳朵。

18-19欺骗邻舍还说是开玩笑,

如同疯子乱抛火把、乱射箭。

20没有木柴,火自然熄灭;

没有闲话,争端便平息。

21好斗之人煽动争端,

如同余火加炭、火上加柴。

22闲言闲语如可口的美食,

轻易进入人的五脏六腑。

23火热的嘴,邪恶的心,

犹如瓦器镀了层银。

24怨恨人的用美言掩饰自己,

心中却藏着诡诈。

25纵然他甜言蜜语,你也不可信他,

因为他心中充满各种可憎之事。

26虽然他用诡计掩饰怨恨,

他的邪恶必被会众揭穿。

27挖陷阱的,必自陷其中;

滚石头的,必自伤己身。

28撒谎的舌恨它所害的人,

谄媚的嘴带来毁灭。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 26:1-28

126:1 Isa 32:6; 1Sam 12:17; Mit 19:10Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno,

ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.

226:2 Hes 23:8; Kum 23:5Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake

au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi,

ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.

326:3 Za 32:9; Mit 10:13Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda,

nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!

426:4 Isa 36:21Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake,

ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.

526:5 Mt 16:14; 21:24-27; Mit 3:7Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake,

ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.

626:6 Mit 10:26Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara,

ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.

726:7 Mit 26:9Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia

ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.

826:8 Mit 26:1Kama kufunga jiwe kwenye kombeo,

ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.

926:9 Mit 26:7Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi

ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.

10Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo,

ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.

1126:11 Kut 8:15; Za 85:8; 2Pet 2:22Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake,

ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.

1226:12 Ufu 3:17; Mit 29:20Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima

machoni pake mwenyewe?

Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.

1326:13 Mit 6:6-11; 24:30-34; 22:13Mvivu husema, “Yuko simba barabarani,

simba mkali anazunguka mitaa!”

1426:14 Mit 6:9Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake,

ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.

1526:15 Mit 19:24Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani,

naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.

16Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe,

kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.

17Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio,

ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.

18Kama mtu mwendawazimu

atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,

1926:19 Efe 5:4ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema,

“Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”

2026:20 Mit 22:10Bila kuni moto huzimika;

pasipo uchongezi ugomvi humalizika.

2126:21 Mit 14:17Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto,

ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.

2226:22 Mit 18:8; Eze 22:9Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu;

huingia sehemu za ndani sana za mtu.

2326:23 Lk 22:48Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo

ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.

2426:24 Za 31:18; 41:6; Mit 10:18; Za 31:18; 41:6Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake,

lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.

2526:25 Za 28:3; Yer 9:4-8Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini,

kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.

26Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu,

lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.

2726:27 Za 7:15-16; 35:8; Mhu 10:8; Mit 28:10; Es 6:13; 7:9Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake,

kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.

2826:28 Mit 13:6; 29:5; Za 12:3Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza,

nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.