申命记 32 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

申命记 32:1-52

摩西之歌

1“诸天啊,请留心听;

大地啊,请听我说。

2愿我的教导如雨降下,

愿我的话语如露滴落,

像水滴滋润嫩草,

像甘霖浇灌草木。

3我要宣扬耶和华的名,

你们要颂赞我们上帝的伟大。

4“祂是磐石,

祂的作为完美,

祂按公义行事,

祂信实可靠,公平正直。

5狡诈、堕落的一代啊,

你们却对祂不忠,行事败坏,

不配做祂的儿女。

6愚昧无知的人啊,

你们就这样报答耶和华吗?

祂是你们的父,你们的创造主,

祂创造了你们,塑造了你们。

7“要回顾往昔,追溯历史;

问你们的父亲,

他们必回答你们;

问你们的长者,

他们必告诉你们。

8当初,至高者赐万国产业,

把人类分开,

祂依照天使32:8 天使”希伯来文是“以色列的儿子”。的数目,

为万族定疆界。

9以色列人属于耶和华,

雅各是祂的产业。

10“在荒凉的旷野,

在野兽吼叫的荒野,

耶和华找到他们,

庇护他们,看顾他们,

保护他们如同保护眼中的瞳仁,

11又如老鹰搅动窝巢,

盘旋在雏鹰之上,展开双翼,

背着雏鹰飞翔。

12耶和华独自带领他们,

身边没有外族神明。

13耶和华使他们驰骋在大地的高处,

吃田间的五谷,

磐石中的蜂蜜,

石头地产的油;

14吃牛酪和羊奶,

肥美的羔羊,

巴珊的绵羊和山羊,

上好的麦子;

喝葡萄汁酿的酒。

15“但耶书仑32:15 耶书仑”是以色列的昵称。吃饱喝足,

养肥长壮后,就得意忘形,

背弃造他们的上帝,

藐视救他们的磐石。

16他们拜外族的神明,令祂愤恨;

行可憎之事,惹祂发怒。

17他们祭拜的不是真神,

而是鬼魔,

是他们素不认识的新神明,

是他们祖先所不敬畏的。

18他们轻视生他们的磐石,

忘记养他们的上帝。

19“耶和华看见祂儿女的恶行,

就愤然厌弃他们,

20说,‘这堕落的子民,

不忠的儿女!

我要掩面不理他们,

看他们的结局如何。

21他们拜假神,让我愤恨;

供虚无之物,惹我发怒。

我要借无名之民挑起他们的嫉妒,

用愚昧的国民激起他们的怒气。

22我的怒火已经点燃,

要烧到阴间的尽头,

吞灭大地及其出产,

甚至烧毁山的根基。

23“‘我要使灾祸连连临到他们,

我的箭都射向他们。

24他们必饱受饥荒之苦,

被瘟疫和灾祸吞噬,

被猛兽和毒蛇袭击。

25外有刀剑杀戮,

内有恐惧笼罩,

少男、少女、婴儿、

老人无一幸免。

26我本要消灭他们,

使世人忘记他们;

27但我不愿让敌人夸口,

宣称这是他们的胜利,

而非我的作为。’

28以色列人愚昧无知,毫无见识。

29如果他们有智慧,

就能明白这一切、

知道自己的结局。

30若不是他们的磐石卖掉他们,

若不是耶和华抛弃他们,

一人怎能赶散他们千人?

二人怎能击溃他们万人?

31我们的敌人也承认他们的磐石不如我们的磐石。

32他们犹如来自所多玛

长在蛾摩拉的葡萄树,

结的葡萄粒粒有毒,串串苦涩;

33酿的酒如蛇的毒液,

如眼镜蛇的毒液。

34“祂说,‘我把这一切积存起来,

封在我的仓库里。

35申冤在我,我必报应,

到时候他们必站不住脚,

他们遭祸的日子近了,

他们的末日来了。’

36“耶和华见自己的子民力量衰竭,

奴隶和自由人所剩无几,

必为他们主持公道,

怜悯祂的仆人。

37祂必说,‘你们的神明在哪里?

庇护你们的磐石在哪里?

38它们吃你们祭牲的脂肪,

喝你们的奠酒。

让它们起来帮助你们,

庇护你们吧!

39“‘你们要知道,

唯有我是上帝;

除我之外,别无他神。

我掌管生死,我打伤、我医治;

无人能逃出我的掌心。

40我向天伸手,

凭我的永恒起誓,

41我要磨快闪亮的剑,

主持公道,报应仇敌,

惩罚恨我的人。

42我要使我的箭饱饮鲜血,

被杀被掳之人的血;

我的剑要吞噬人肉,

敌人将领的肉。’

43“列邦啊,

你们当与祂的子民一同欢乐!

因为祂要为自己的仆人报血仇,

报应祂的仇敌,

洁净祂的土地和子民。”

44摩西的儿子约书亚把这首诗歌读给会众听。

摩西的遗嘱

45读完后,摩西又对以色列人说: 46“要谨记我今天警告你们的话,要吩咐你们的子孙谨遵这律法上的话。 47这律法不是空话,而是你们的生命。你们若遵守这律法,就必长住在约旦河对岸你们将要占领的土地上。”

预言摩西的死

48当天,耶和华对摩西说: 49“你去耶利哥对面的摩押,登上亚巴琳山区的尼波山,观看我要赐给以色列人作产业的迦南50之后,你会死在山上,归到你祖先那里,如亚伦何珥山离世归祖一样。 51因为在旷野,在加低斯米利巴泉旁,你和亚伦对我不忠,没有在以色列人中尊我为圣。 52所以,你只能远远地观看我要赐给以色列人的土地,却不能进去。”

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 32:1-52

132:1 Za 49:1; Mik 1:2; Yer 2:12; Kum 4:26; Isa 1:2Sikilizeni, enyi mbingu, nami nitasema;

sikia, ee nchi, maneno ya kinywa changu.

232:2 2Sam 23:4; Za 107:20; Isa 9:8; 55:11; Mik 5:7; Za 65:10; 68:9; 72:8; 147:8Mafundisho yangu na yanyeshe kama mvua,

na maneno yangu na yashuke kama umande,

kama manyunyu juu ya majani mabichi,

kama mvua tele juu ya mimea myororo.

332:3 Za 118:17; 145:6; Kut 33:16-19; 34:4-6; Kum 3:24Nitalitangaza jina la Bwana.

Naam, sifuni ukuu wa Mungu wetu!

432:4 Mwa 49:24; 2Sam 22:31; Za 18:30; 19:7; Kum 4:35; Za 92:15; Mwa 18:25Yeye ni Mwamba, kazi zake ni kamilifu,

njia zake zote ni haki.

Mungu mwaminifu ambaye hakosei,

yeye ni mnyofu na mwenye haki.

532:5 Kum 31:29; Mt 17:17; Lk 9:41; Mdo 2:40Wamefanya mambo ya upotovu mbele zake;

kwa aibu yao, wao si watoto wake tena,

lakini ni kizazi kilicho kiovu na kilichopotoka.

632:6 Za 116:12; 94:8; Yer 5:21; Kut 4:22; 2Sam 7:24; Isa 63:16Je, hii ndiyo njia ya kumlipa Bwana,

enyi watu wajinga na wasio na busara?

Je, yeye siye Baba yenu, Muumba wenu,

aliyewafanya ninyi na kuwaumba?

732:7 Za 44:1; 74:2; 74:2; 77:5; Isa 51:9; 63:9; Kum 4:32; Yos 8:8; 20:4; Za 78:4; Isa 46:9; Kut 10:2; 13:14; Ay 15:18Kumbuka siku za kale;

tafakari vizazi vya zamani vilivyopita.

Uliza baba yako, naye atakuambia,

wazee wako, nao watakueleza.

832:8 Za 7:8; Mwa 11:8; Mdo 8:1; Za 74:17; Hes 23:9; Kum 33:12; 28; Yer 23:6; Mdo 17:26Aliye Juu Sana alipowapa mataifa urithi wao,

alipogawanya wanadamu wote,

aliweka mipaka kwa ajili ya mataifa

sawasawa na hesabu ya wana wa Israeli.

932:9 Za 16:5; 73:26; 119:57; 142:5; Yer 10:16; Kum 9:29; 1Sam 26:19; 1Fal 8:51-53Kwa kuwa fungu la Bwana ni watu wake,

Yakobo kura yake ya urithi.

1032:10 Kum 1:19; 8:15; Ay 12:24; Za 107:40; 32:10; Yer 31:22; Za 17:8; Mit 7:2; Hos 13:5; Zek 2:8Katika nchi ya jangwa alimkuta,

katika nyika tupu ivumayo upepo.

Alimhifadhi na kumtunza;

akamlinda kama mboni ya jicho lake,

1132:11 Kut 19:4; Za 17:8; 18:10-19; 61:4kama tai avurugaye kiota chake,

na kurukaruka juu ya makinda yake,

ambaye hutanda mabawa yake kuwadaka,

na huwachukua kwenye mabawa yake.

1232:12 Za 106:9; Isa 63:13; Yer 31:32; Kum 4:35; Amu 2:12; Za 18:31; 81:9; Isa 43:12; 45:5Bwana peke yake alimwongoza;

hakuwepo mungu mgeni pamoja naye.

1332:13 Kum 33:29; 2Sam 22:34; Za 18:33; Isa 33:16; 58:14; Eze 36:2; Ebr 3:19; Kum 8:8; 33:24; Ay 29:6Akamfanya apande sehemu zilizoinuka za nchi,

akamlisha kwa mavuno ya mashamba.

Akamlea kwa asali toka mwambani,

na kwa mafuta kutoka mwamba mgumu,

1432:14 Hes 21:33; Za 65:9; 81:16; 147:14; Mwa 49:11kwa jibini na maziwa kutoka makundi ya ngʼombe

na kutoka makundi ya mbuzi,

kwa mafuta ya wana-kondoo na mbuzi,

kwa kondoo dume wazuri wa Bashani,

na kwa ngano nzuri.

Ukanywa damu ya zabibu inayotoa povu.

1532:15 Kum 33:5; 26; Isa 44:2; Kum 31:20; Yer 5:28; Kum 31:16; Isa 1:4, 28; 58:2; 65:11; Yer 15:6; Eze 14:5; Mwa 49:24Yeshuruni32:15 Yeshuruni maana yake ni Yeye aliye mnyofu, yaani Israeli (ona pia Kum 33:26; Isa 44:2). alinenepa na kupiga teke;

alikuwa na chakula tele,

akawa mzito na akapendeza sana.

Akamwacha Mungu aliyemuumba,

na kumkataa Mwamba Mwokozi wake.

1632:16 1Kor 10:22; Kum 31:17; 1Fal 14:9Wakamfanya Mungu kuwa na wivu kwa miungu yao migeni,

na kumkasirisha kwa sanamu zao

za machukizo.

1732:17 Kut 32:8; 22:20; 1Kor 10:20; Kum 28:64; Amu 5:8Wakatoa dhabihu kwa pepo, ambao si Mungu:

miungu wasiyoijua,

miungu iliyojitokeza siku za karibuni,

miungu ambayo baba zenu hawakuiogopa.

1832:18 Amu 3:7; 1Sam 12:9; Za 44:17, 20; 106:21; Yer 2:32; Eze 23:35; Hos 8:14; 13:6Mkamwacha Mwamba, aliyewazaa ninyi;

mkamsahau Mungu aliyewazaa.

1932:19 Law 26:30; Za 78:59; Amo 6:8; Yer 44:21-23; Za 106:40Bwana akaona hili, akawakataa,

kwa sababu alikasirishwa

na wanawe na binti zake.

2032:20 Kum 31:17; Za 4:6; 44:24; Kum 9:23Akasema, “Nitawaficha uso wangu,

nami nione mwisho wao utakuwa nini,

kwa kuwa wao ni kizazi kilichopotoka,

watoto ambao si waaminifu.

2132:21 Hes 25:11; 1Kor 10:22; 1Fal 16:13, 26; 2Fal 17:15; Yer 8:19; Yon 2:8; Rum 10:19; Za 31:6; Yer 2:8; 10:8; 16:19Wamenifanya niwe na wivu

kwa kile ambacho si mungu,

na kunikasirisha kwa sanamu zao

zisizokuwa na thamani.

Nitawafanya wawaonee wivu wale ambao si taifa.

Nitawafanya wakasirishwe

na taifa lile lisilo na ufahamu.

2232:22 Za 7:11; Hes 16:31-35; Za 18:7-8; Yer 15:14; Mao 4:11; Amo 7:4; Law 26:20Kwa maana moto umewashwa kwa hasira yangu,

ule uwakao hadi kwenye vina vya mauti.

Utateketeza dunia pamoja na mazao yake,

na kuwasha moto katika misingi ya milima.

2332:23 Kum 29:21; 2Sam 22:15; Ay 6:4; Za 7:13; 18:14; 45:5; 77:17; 120:4; Isa 5:28; 49:2; Eze 5:16; Hab 3:9-11“Nitalundika majanga juu yao

na kutumia mishale yangu dhidi yao.

2432:24 Mwa 26:1; 41:55; 42:5; 2Sam 24:13; 1Nya 21:12; Kum 28:22; Za 91:6; Mwa 37:20; Ay 20:16; Za 58:4; Yer 8:17; Amo 5:18-19; Mik 7:17; Ay 20:16Nitatuma njaa kali dhidi yao maradhi mabaya,

yateketezayo na tauni ya kufisha;

nitawapelekea meno makali ya wanyama mwitu,

na sumu ya nyoka wale watambaao mavumbini.

2532:25 Isa 24:17; Yer 14:18; Mao 1:20; Eze 7:15; 2Kor 7:5; 2Nya 36:17; Isa 13:18; Yer 4:31; Mao 2:21Barabarani upanga utawakosesha watoto;

nyumbani mwao hofu itatawala.

Vijana wao wa kiume na wa kike wataangamia,

pia watoto wachanga na wazee wenye mvi.

2632:26 Kum 4:27; Hes 14:12; Ay 18:17; Za 34:16; 37:28; 109:15; Isa 14:20Nilisema ningewatawanya

na kufuta kumbukumbu lao

katika mwanadamu.

2732:27 Kum 9:26-28; Za 140:8; Isa 11:13; Yer 40:2-3Lakini nilihofia dhihaka za adui,

adui asije akashindwa kuelewa,

na kusema, ‘Mikono yetu imeshinda;

Bwana hakufanya yote haya.’ ”

2832:28 Isa 1:3; 5:13; 27:11; Yer 8:7Wao ni taifa lisilo na akili,

hakuna busara ndani yao.

2932:29 Kum 5:29; Za 81:13; Isa 47:7; Mao 1:9Laiti wangekuwa na hekima wangefahamu hili,

na kutambua mwisho wao utakuwa aje!

3032:30 Law 26:8; Amu 2:14; 3:8; 4:2; 10:7; 1Sam 12:9; Hes 21:34; 1Sam 23:7; Za 31:18; 44:12; 106:41; Isa 50:1; 54:6Mtu mmoja angewezaje kufukuza elfu moja,

au wawili kufukuza elfu kumi,

kama si kwamba Mwamba wao amewauza,

kama si kwamba Bwana amewaacha?

3132:31 Mwa 49:24; Kut 14:25Kwa kuwa mwamba wao si kama Mwamba wetu,

sawasawa na vile adui zetu wanavyokiri.

3232:32 Yer 23:14; Ay 6:4; 20:16; Kum 29:18Mzabibu wao unatoka kwenye mzabibu wa Sodoma,

na kutoka kwenye mashamba ya Gomora.

Zabibu zake zimejaa sumu,

na vishada vyake vimejaa uchungu.

3332:33 Za 58:4Mvinyo wao ni sumu ya nyoka,

sumu yenye kufisha ya swila.

3432:34 Ay 14:17; Yer 2:22; Hos 13:12“Je, hili sikuliweka akiba

na kulifungia kwenye vyumba vyangu vya hazina?

3532:35 Mwa 4:24; Yer 51:6; Mwa 30:2; Kut 32:34; Za 54:5; Rum 12:19; Ebr 10:30; Za 17:5; 35:6; 37:31; 38:16; 66:9; 73:2; 94:18; 121:3; Mit 4:19; Yer 23:12; Eze 7:8-9Ni juu yangu kulipiza kisasi; nitalipiza.

Wakati utakapowadia, mguu wao utateleza;

siku yao ya maafa ni karibu,

na maangamizo yao yanawajia haraka.”

3632:36 Ebr 10:30; Amo 7:3; Law 26:43-45; Kum 30:1-3; Amu 2:18; Za 90:13; 102:13; 103:13; 106:45; 135:14; Yoe 2:14; 1Fal 14:10; 21:21; 2Fal 9:8Bwana atawahukumu watu wake,

na kuwahurumia watumishi wake

atakapoona nguvu zao zimekwisha

wala hakuna yeyote aliyebaki,

mtumwa au aliye huru.

3732:37 Amu 10:14; Yer 2:28; 11:12Atasema: “Sasa iko wapi miungu yao,

mwamba walioukimbilia,

3832:38 Hes 25:1-2; Yer 11:12; 44:8; 25miungu wale waliokula mafuta ya dhabihu zao

na kunywa mvinyo wa sadaka zao za vinywaji?

Wainuke basi, wawasaidie!

Wawapeni basi ulinzi!

3932:39 Isa 41:4; 43:10; 44:7; 46:4; 48:12; 1Sam 2:6; 2Fal 5:7; Za 68:20; Yn 11:25-26; Kut 15:26; Ay 5:18; 15:11; Za 147:3; Isa 6:10; 19:22; 30:26; 53:5; 57:18; Yer 33:6; Hos 6:1; Mal 4:2; 1Pet 2:24; Ay 9:12; 10:7; Za 7:2; 50:22; Isa 43:13; Dan 4:35; Hos 5:14“Tazama basi, Mimi mwenyewe, Mimi Ndiye!

Hakuna mungu mwingine ila Mimi.

Mimi ninaua na Mimi ninafufua,

Mimi nimejeruhi na Mimi nitaponya,

wala hakuna awezaye kuokoa kutoka mkononi mwangu.

4032:40 Mwa 14:22; 21:23; Ufu 1:18Ninainua mkono wangu kuelekea mbinguni na kusema:

Hakika kama niishivyo milele,

4132:41 Amu 7:20; Za 7:12; 45:3; Isa 27:1; 34:6; 66:16; Yer 12:12; Eze 21:9-10; Za 149:7; Yer 46:10; Neh 1:2; Za 137:8; Yer 25:14; 50:29; 51:24, 56wakati ninapounoa upanga wangu unaometameta

na mkono wangu unapoushika ili kutoa hukumu,

nitalipiza kisasi juu ya adui zangu

na kuwalipiza wale wanaonichukia.

4232:42 2Sam 2:26; Yer 12:12; 44:1; 46:10-14Nitailevya mishale yangu kwa damu,

wakati upanga wangu ukitafuna nyama:

damu ya waliochinjwa pamoja na mateka,

vichwa vya viongozi wa adui.”

4332:43 Za 137:6; Isa 25:9; 65:18; 66:10; Rum 15:10; 2Fal 9:7; Ufu 6:10; Isa 1:24; Yer 9:9; Za 65:3; 79:9Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake,

kwa kuwa atailipiza damu ya watumishi wake,

atalipiza kisasi juu ya adui zake

na kufanya upatanisho

kwa ajili ya nchi na watu wake.

4432:44 Hes 13:8, 16Mose na Yoshua32:44 Yoshua, yaani Yehoshea kwa Kiebrania, maana yake ni Yehova ni Mwokozi. mwana wa Nuni wakaja, wakanena maneno yote ya wimbo watu wakiwa wanasikia. 45Mose alipomaliza kuyasoma maneno haya yote kwa Israeli wote, 4632:46 Kum 6:6; Yn 1:17; 7:19; Kum 6:7akawaambia, “Yawekeni moyoni maneno yote ambayo nimewatangazia kwa makini siku hii ya leo, ili kwamba mpate kuwaagiza watoto wenu wayatii kwa bidii maneno yote ya sheria hii. 4732:47 Kum 30:20; 33:25; Kut 23:26; Isa 65:22Siyo maneno matupu tu kwenu, bali ni uzima wenu. Kwa hayo mtaishi maisha marefu katika nchi mnayovuka Yordani kuimiliki.”

Mose Aelezwa Kuhusu Kifo Chake

4832:48 Hes 27:12Siku hiyo hiyo Bwana akamwambia Mose, 4932:49 Hes 27:12; 32:3; 22:1; Law 14:34“Kwea katika mapangano ya Mlima Abarimu hadi kilima cha Nebo kilichoko Moabu, ngʼambo ya Yeriko, na uitazame Kanaani, nchi ninayowapa Waisraeli kama milki yao wenyewe. 5032:50 Mwa 25:8; Hes 27:13; 20:22; 29Utafia kwenye mlima huo unaokwea na kukusanyika pamoja na watu wako, kama ndugu yako Aroni alivyofia juu ya Mlima Hori naye akakusanyika kwa watu wake. 5132:51 Eze 47:19; Hes 13:21; 20:11-13; 27:14Hii ni kwa sababu ninyi wawili mlivunja uaminifu nami mbele ya Waisraeli kwenye maji ya Meriba-Kadeshi katika Jangwa la Sini, na kwa sababu hamkuuinua utakatifu wangu miongoni mwa Waisraeli. 5232:52 Kum 34:1-3; 3:27Kwa hiyo, utaiona tu nchi kwa mbali; wewe hutaingia nchi ninayowapa watu wa Israeli.”