士师记 5 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

士师记 5:1-31

底波拉和巴拉之歌

1那一天,底波拉巴拉高唱凯歌:

2以色列的首领身先士卒,

民众前仆后继,

你们要赞美耶和华!

3君王和首领啊,请留心细听!

我要向耶和华歌唱,

我要歌颂以色列的上帝耶和华。

4耶和华啊,当你从西珥出来,

走过以东时,

大地震动,

天上降雨。

5西奈山的耶和华面前,

以色列的上帝耶和华面前,

群山震动。

6亚拿的儿子珊迦雅亿的时代,

大路行人绝迹,

旅客绕道而行。

7底波拉以色列之母以前,

以色列的乡村人烟稀少。

8以色列人选择新的神明,

便战祸临门,

四万以色列人中找不到一矛一盾。

9我的心追随以色列的首领,

追随民中踊跃出征的人。

你们要赞美耶和华!

10“你们骑白驴的、坐绣花毯子的、步行的,

都要倾听。

11歌乐手聚集在井旁,

传扬耶和华和祂以色列子民的胜利。

耶和华的子民都来到城门口。

12底波拉啊,来吧,来吧,

歌唱吧!

亚比挪庵的儿子巴拉啊,来吧,

带走你的战俘吧!

13幸存的以色列人响应他们的首领,

耶和华的子民为我攻击勇士。

14他们有些来自原属亚玛力人的以法莲

有些来自便雅悯

统领出自玛吉

将官出自西布伦

15以萨迦的首领与底波拉同往,

以萨迦人随巴拉同去,

众人一起冲进山谷,

吕便人却犹豫不决。

16吕便人为什么坐在羊圈中听悠悠笛声?

他们举棋不定。

17基列人留在约旦河对岸。

人为什么停留在船上?

亚设人在海岸静坐,

在港口逗留。

18西布伦人和拿弗他利人却拼死鏖战沙场。

19迦南诸王来战,

来到米吉多河边的他纳交战,

却没有掠走金银。

20星辰从天上、从它们的轨道攻击西西拉

21古老的基顺河冲走了敌人。

我的心啊,要奋勇向前!

22蹄声隆隆,

骏马疾驰!

23“耶和华的天使说,

‘要咒诅米罗斯

要重重地咒诅米罗斯的居民,

因为他们没有帮助耶和华,

没有帮助耶和华攻击强敌。’

24基尼希百的妻子雅亿是妇人中最有福的,

是住帐篷的妇人中最有福的。

25西西拉求水,

雅亿给他奶喝,

用珍贵的碗盛上奶酪。

26雅亿左手拿起橛子,

右手拿起工匠的锤子,

猛击西西拉

打碎了他的头,

刺透了他的太阳穴。

27西西拉屈身倒下,

死在她脚前,

一动不动地躺在那里。

28“他母亲凭窗远眺,

隔着窗棂喊道,

‘为什么他的战车迟迟不回?

为什么还听不到车轮声?’

29聪明的宫女安慰她,

她却依然自言自语,

30‘莫非他们在搜索、瓜分战利品?

也许每人得到一两个少女,

西西拉也会分得从俘虏身上夺来的绣花彩巾。’

31耶和华啊,

愿你的敌人都像西西拉一样灭亡!

愿爱你的人如升起的太阳,

光辉熠熠!”

此后,以色列安享太平四十年。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waamuzi 5:1-31

Wimbo Wa Debora

15:1 Amu 4:4, 6; Kut 15:1; Za 32:7Ndipo Debora na Baraka mwana wa Abinoamu wakaimba wimbo huu:

25:2 2Nya 17:16; Za 110:3“Wakuu katika Israeli wanapoongoza,

wakati watu wanapojitoa

kwa hiari yao wenyewe:

mhimidini Bwana!

35:3 Kut 15:1; Za 27; 6“Sikieni hili, enyi wafalme!

Sikilizeni, enyi watawala!

Nitamwimbia Bwana, nitaimba;

kwa wimbo nitamhimidi Bwana,

Mungu wa Israeli.

45:4 Kut 13:21; Hes 24:18; Kut 33:2; 2Sam 22:8; Za 18:7; 77:18; 82:5; Isa 2:19-21; 64:3; Yer 10; 10; 50:46; 51:29; Yoe 3:16; Nah 1:5; Hab 3:6; Za 68:8; 77:17“Ee Bwana, ulipotoka katika Seiri,

ulipopita katika mashamba ya Edomu,

nchi ilitetemeka, mbingu nazo zikamwaga,

naam, mawingu yakamwaga maji.

55:5 Kut 19:18; Za 29:6; 46:3; 77:18; 114:4; Isa 64:3Milima ilitetemeka mbele za Bwana,

hata ule wa Sinai,

mbele za Bwana,

Mungu wa Israeli.

65:6 Amu 3:31; 4:17; Law 26:22; Isa 33:8; Za 125:5; Isa 59:8“Katika siku za Shamgari mwana wa Anathi,

katika siku za Yaeli,

barabara kuu hazikuwa na watu;

wasafiri walipita njia za kando.

75:7 Amu 4:4Mashujaa walikoma katika Israeli,

walikoma mpaka mimi, Debora, nilipoinuka,

nilipoinuka kama mama katika Israeli.

85:8 Kum 32:17; Amu 2:13; Yos 2:5; Hes 25:7Walipochagua miungu migeni,

vita vilikuja katika malango ya mji,

hapakuonekana ngao wala mkuki

miongoni mwa mashujaa 40,000 katika Israeli.

9Moyo wangu u pamoja na wakuu wa Israeli,

pamoja na wale wanaojitoa wenyewe

kwa hiari yao miongoni mwa watu.

Mhimidini Bwana!

105:10 Mwa 49:11; Amu 12:14; 10:4“Nanyi mpandao punda weupe,

mkiketi juu ya matandiko ya thamani,

nanyi mtembeao barabarani,

fikirini 115:11 1Sam 12:7; Dan 9:16; Mik 6:5juu ya sauti za waimbaji

mahali pa kunyweshea maji.

Wanasimulia matendo ya haki ya Bwana,

matendo ya haki ya mashujaa wake

katika Israeli.

“Ndipo watu wa Bwana

walipoteremka malangoni pa mji.

125:12 Za 44:23; 57:8; Isa 51:9, 17; Amu 4:4-6; Za 68:18; Efe 4:8‘Amka, amka! Debora!

Amka, amka, uimbe!

Ee Baraka! Inuka,

chukua mateka wako uliowateka,

ee mwana wa Abinoamu.’

13“Ndipo mabaki ya watu

wakashuka dhidi ya wenye nguvu,

watu wa Bwana,

wakashuka dhidi ya mashujaa wenye nguvu.

145:14 Mwa 41:52; Amu 1:29; 3:13; Hes 34:21; Mwa 50:23Kutoka Efraimu wakaja watu, ambao chimbuko lao ni Amaleki;

Benyamini akiwa miongoni

mwa watu waliokufuata.

Kutoka Makiri wakashuka viongozi,

na kutoka Zabuloni wale washikao

fimbo ya jemadari.

155:15 Mwa 50:18; Amu 4:4-6Wakuu wa Isakari walikuwa pamoja na Debora;

naam, Isakari alikuwa pamoja na Baraka,

wakija nyuma yake kwa mbio

wakielekea bondeni.

Katika jamaa za Reubeni,

palikuwa na kujihoji kukubwa moyoni.

165:16 Mwa 49:11; Hes 32; 1Kwa nini ulikaa katikati ya mazizi ya kondoo

kusikiliza sauti ya filimbi zinazoita makundi?

Kwa jamaa za Reubeni,

palikuwa na kujihoji kukubwa moyoni.

175:17 Yos 12:2; 17:7; 19:29Gileadi alikaa ngʼambo ya Yordani.

Naye Dani, kwa nini alikaa

kwenye merikebu siku nyingi?

Asheri alikaa kwa utulivu ufuoni mwa bahari,

akikaa kwenye ghuba zake ndogo.

185:18 Mwa 30:20; 30:8; Za 68:27; Amu 9:6Watu wa Zabuloni walihatarisha maisha yao,

vilevile nao watu wa Naftali.

195:19 Yos 11:5; Amu 4; 13; Ufu 16:16; Yos 12:21; Amu 1:27“Wafalme walikuja na kufanya vita;

wafalme wa Kanaani walipigana

huko Taanaki karibu na maji ya Megido,

lakini hawakuchukua fedha wala nyara.

205:20 Yos 10:11Kutoka mbinguni nyota zilipigana,

nyota kutoka njia zake

zilipigana na Sisera.

215:21 Amu 4:7; Yos 1:6Mto wa Kishoni uliwasomba,

ule mto wa zamani, mto wa Kishoni.

Songa mbele, ee nafsi yangu,

kwa ujasiri!

225:22 Yer 8:16Ndipo kwato za farasi zikafanya mshindo:

farasi wake wenye nguvu

huenda mbio kwa kurukaruka.

23Malaika wa Bwana akasema, ‘Merozi alaaniwe.

Walaaniwe watu wake kwa uchungu,

kwa kuwa hawakuja kumsaidia Bwana,

kumsaidia Bwana dhidi ya hao wenye nguvu.’

245:24 Lk 1:42; Amu 4:17; Mwa 15:19“Yaeli abarikiwe kuliko wanawake wote,

mkewe Heberi, Mkeni,

abarikiwe kuliko wanawake wote

waishio kwenye mahema.

255:25 Mwa 18:8; Amu 4:19Aliomba maji, naye akampa maziwa;

kwenye bakuli la heshima

akamletea maziwa mgando.

26Akanyoosha mkono wake

akashika kigingi cha hema,

mkono wake wa kuume

ukashika nyundo ya fundi.

Akampiga Sisera kwa nyundo,

akamponda kichwa chake,

akamvunjavunja na kumtoboa

paji lake la uso.

27Aliinama miguuni pa Yaeli,

akaanguka; akalala hapo.

Pale alipoinama miguuni pake,

alianguka;

pale alipoinamia, ndipo alipoanguka,

akiwa amekufa.

285:28 Yos 2:15; Mit 7:6“Kupitia dirishani mamaye Sisera alichungulia;

nyuma ya dirisha alilia, akasema,

‘Mbona gari lake linachelewa kufika?

Mbona vishindo vya magari yake

vimechelewa?’

29Wanawake wenye busara

kuliko wengine wote wakamjibu;

naam, husema moyoni mwake,

305:30 Kut 15:9; 1Sam 30:24; Za 68:12; 45:14; Eze 16:10; 2Sam 1:24‘Je, hawapati na kugawanya nyara:

msichana mmoja au wawili kwa kila mtu,

mavazi ya rangi mbalimbali kwa Sisera kuwa nyara,

mavazi ya rangi mbalimbali yaliyotariziwa,

mavazi yaliyotariziwa vizuri kwa ajili ya shingo yangu:

yote haya yakiwa nyara?’

315:31 Hes 10:35; 2Sam 23:4; Ay 37:21; Za 19:4; 89:36; Isa 18:4; 2Sam 18:32; Amu 3:11“Adui zako wote na waangamie, Ee Bwana!

Bali wote wakupendao na wawe kama jua

lichomozavyo kwa nguvu zake.”

Hivyo nchi ikawa na amani kwa miaka arobaini.