士师记 4 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

士师记 4:1-24

士师底波拉

1以笏死后,以色列人又做耶和华视为恶的事。 2耶和华把他们交在统治夏琐迦南耶宾手中。耶宾王的将军叫西西拉,住在夏罗设3耶宾王拥有九百辆铁战车,他残暴地压迫以色列人二十年。以色列人向耶和华呼求。

4当时做士师的是一位名叫底波拉的女先知,她是拉比多的妻子, 5经常坐在以法莲山区拉玛伯特利之间的底波拉棕树下,审理以色列人的事情。 6她派人去拿弗他利基低斯召来亚比挪庵的儿子巴拉,对他说:“以色列的上帝耶和华命你率领一万拿弗他利人和西布伦人上他泊山。 7祂必使耶宾的将军西西拉率领全军和战车到基顺河与你交战,祂必把西西拉交在你手中。” 8巴拉回答说:“你跟我去,我就去;你不跟我去,我就不去。” 9底波拉说:“好,我一定与你同去。不过,你这次出征一定得不到荣耀,因为耶和华要把西西拉交在一名妇人手上。”于是,他们一同前往基低斯10巴拉招聚了一万名拿弗他利人和西布伦人,底波拉与他一起出征。

11摩西的岳父何巴的后人基尼希百离开自己的族人,在基低斯附近撒拿音的橡树旁搭帐篷居住。

12西西拉得知亚比挪庵的儿子巴拉已经上了他泊山, 13便召集全军和九百辆铁战车离开夏罗设,向基顺河进军。 14底波拉巴拉说:“出击吧!今天耶和华要把西西拉交在你手中。看啊,耶和华已经率先出战了!”于是,巴拉率领一万人下了他泊山, 15进攻西西拉。耶和华使西西拉的战车和军队惊慌失措,败在巴拉刀下。西西拉弃车徒步逃跑, 16巴拉追击他的战车和军队,直到夏罗设西西拉全军都死于刀下,无一幸免。

17只有西西拉一人徒步逃到基尼希百的妻子雅亿的帐篷,因为耶宾王和希百家向来友好。 18雅亿出来迎接西西拉,对他说:“我主,请进,不用怕!”西西拉便走进帐篷,雅亿为他盖上毯子。 19西西拉说:“我口渴,请给我一点水吧。”雅亿打开皮袋给他奶喝,然后又给他盖上毯子。 20西西拉又说:“请你守着门口,倘若有人查问,你就说没人来过这里。” 21西西拉因疲劳过度,沉沉入睡。雅亿乘机拿起锤子和一根帐篷的橛子,悄悄地走到他身旁,把橛子钉进他的太阳穴,直插到地里。西西拉就这样死了。 22巴拉追来了,雅亿出来迎接他,对他说:“你找的人在这里,进来看看吧。”巴拉和她进了帐篷,见西西拉死在那里,太阳穴上还插着橛子。

23那天,上帝使以色列人战胜了迦南耶宾24以色列人越战越勇,最终消灭了耶宾王。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waamuzi 4:1-24

Debora

14:1 Amu 3:15; 2:11; 2:19Baada ya Ehudi kufa, Waisraeli wakafanya tena maovu machoni pa Bwana. 24:2 Kum 32:30; Yos 11:1; 1Sam 12:9; Za 83:9Hivyo Bwana akawatia mikononi mwa Yabini, mfalme wa Kanaani, aliyetawala huko Hazori. Jemadari wa jeshi lake alikuwa Sisera, aliyeishi huko Haroshethi-Hagoyimu4:2 Haroshethi-Hagoyimu ina maana Haroshethi ya Mataifa. 34:3 Yos 17:16; Amu 10:12; Za 106:42; Amu 1:19Kwa kuwa Sisera alikuwa na magari ya chuma yapatayo 900, naye alikuwa amewatesa Waisraeli kwa ukatili kwa muda wa miaka ishirini, Waisraeli wakamlilia Bwana wakaomba msaada.

44:4 Amu 5:1, 7, 12; Kut 15:20Debora, nabii mwanamke, mkewe Lapidothi, ndiye alikuwa anaamua Israeli wakati ule. 54:5 1Sam 14:2; 22; 6; Yos 18:25; 12:5-9; Mwa 35:8Debora alikuwa akiketi chini ya Mtende wa Debora uliokuwa kati ya Rama na Betheli katika nchi ya vilima ya Efraimu, nao Waisraeli wakaja kwake ili awaamue. 64:6 Amu 5:12-15; 1Sam 12:11; Ebr 11:32; Yos 12:22; Mwa 30:8; Amu 5:18; 6:35; Yos 19:22Akatuma wamwite Baraka mwana wa Abinoamu kutoka Kedeshi huko Naftali na kumwambia, “Bwana, Mungu wa Israeli, anakuagiza: ‘Nenda, chukua wanaume 10,000 toka Naftali na Zabuloni, mwende Mlima Tabori. 74:7 Yos 11:1; Amu 5:12; 1Fal 18:40; Za 83:9; Amu 1:2Nitamshawishi Sisera, jemadari wa jeshi la Yabini, pamoja na magari yake na jeshi lake, hadi Mto Kishoni na kumtia mikononi mwako.’ ”

8Baraka akamwambia, “Ukienda pamoja nami nitakwenda, lakini usipokwenda pamoja nami, sitakwenda.”

94:9 Yos 12:22; Amu 2:14Debora akamwambia, “Hakika nitakwenda pamoja nawe, lakini njia unayoiendea haitakupa heshima wewe, kwa kuwa Bwana atamtia Sisera mikononi mwa mwanamke.” Hivyo Debora akaenda pamoja na Baraka mpaka Kedeshi, 104:10 2Nya 36:23; Ezr 1:2; Isa 41:2; 42:6; 45:3; 46:11; 48:15mahali ambapo Baraka aliwaita Zabuloni na Naftali. Watu 10,000 wakamfuata Baraka, na Debora pia akaenda pamoja naye.

114:11 Mwa 15:19; Hes 10:29; Yos 24:26; Amu 9:6; Yos 19:33Basi Heberi, Mkeni, alikuwa amejitenga na Wakeni wengine, yaani, wazao wa Hobabu, mkwewe Mose, naye akapiga hema lake karibu na ule mti mkubwa wa mwaloni ulioko Saananimu, karibu na Kedeshi.

124:12 Yos 19:22Sisera alipoambiwa kuwa Baraka mwana wa Abinoamu alikuwa amepanda Mlima Tabori, 134:13 Yos 17:16; Amu 4:7; 5:19Sisera akakusanya pamoja magari yake yote 600 ya chuma na watu wote waliokuwa pamoja naye, kuanzia Haroshethi-Hagoyimu mpaka Mto wa Kishoni.

144:14 Amu 1:2; Kum 9:3; 1Sam 8:20; 2Sam 5:24; Za 68:7Ndipo Debora akamwambia Baraka, “Nenda! Hii ndiyo siku ambayo Bwana amemtia Sisera mikononi mwako. Je, Bwana hakukutangulia mbele yako?” Hivyo Baraka akashuka kutoka Mlima Tabori, akifuatwa na watu 10,000. 154:15 Kut 14:24; Za 18:14; Kut 14:28; Za 83:9-10Bwana akamfadhaisha Sisera na magari yake yote, pamoja na jeshi lake lote kwa upanga mbele ya Baraka, naye Sisera akaliacha gari lake na kukimbia kwa miguu. 164:16 Kut 14:28; Za 83:9-10Lakini Baraka akafuata magari pamoja na jeshi mpaka Haroshethi-Hagoyimu. Jeshi lote la Sisera likaanguka kwa upanga, wala hakuna hata mtu mmoja aliyesalia.

174:17 Amu 5:6, 24; Mwa 15:19; Yos 11; 1Sisera, hata hivyo, akakimbia kwa miguu mpaka kwenye hema la Yaeli, mkewe Heberi, Mkeni, kwa sababu palikuwa na uhusiano wa kirafiki kati ya Yabini mfalme wa Hazori na ukoo wa Heberi, Mkeni.

18Yaeli akaenda kumlaki Sisera na kumwambia, “Karibu, bwana wangu, karibu ingia ndani kabisa. Usiogope.” Basi Sisera akaingia ndani ya hema ya Yaeli, naye akamfunika kwa blanketi nene.

194:19 Mwa 18:8; Amu 5:25Akamwambia, “Nina kiu, tafadhali nipe maji ya kunywa.” Ndipo akafungua kiriba cha maziwa na kumpa akanywa, kisha akamfunika.

20Naye Sisera akamwambia, “Simama mlangoni pa hema na mtu yeyote akija na kukuuliza, ‘Je, kuna mtu yeyote hapa?’ sema, ‘Hapana.’ ”

214:21 Mwa 2:21; 15:12; 1Sam 26:12; Isa 29:10; Yon 1:5; Amu 5:26Ndipo Yaeli, mkewe Heberi, akatwaa kigingi cha hema, akachukua nyundo mkononi mwake, akamwendea polepole, akiwa amelala usingizi, akiwa amechoka. Akakigongomea kile kigingi kwenye paji la uso wake, kikapenya hata kuingia ardhini, naye akafa.

224:22 Amu 5:27Baraka akakaribia akimfuatia Sisera, Yaeli akatoka kumlaki. Akamwambia, “Njoo, nitakuonyesha mtu unayemtafuta.” Hivyo wakaingia ndani ya hema wakiwa wamefuatana na tazama Sisera alikuwa amelala humo, akiwa amekufa, na hicho kigingi cha hema kikiwa kimegongomewa kupitia paji la uso wake.

234:23 Neh 9:24; Za 18:47; 44:2; 47:3; 144:2; Yos 11; 1Basi siku ile Mungu akamshinda Yabini, mfalme wa Kanaani, mbele ya Israeli. 244:24 Za 83:9; 106:43Nao mkono wa Waisraeli ukaendelea kuwa na nguvu zaidi na zaidi dhidi ya Yabini, mfalme wa Kanaani, mpaka wakamwangamiza.