士师记 12 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

士师记 12:1-15

耶弗他打败以法莲人

1后来,以法莲人召集军队,渡过约旦河来到撒分。他们对耶弗他说:“你为什么不召我们一起去攻打亚扪人呢?我们要把你和你的房子一起烧掉。” 2耶弗他说:“我和我的人民与亚扪人激战时,我曾召你们参战,你们却不肯来援救我们。 3我见你们不来援救,只好冒死去迎战亚扪人,耶和华把敌人交在了我手中。你们今天为什么来攻打我呢?” 4以法莲人说:“你们这些在以法莲玛拿西境内的基列人不过是以法莲的逃亡者。”于是,耶弗他号召基列人起来迎战以法莲人,打败了他们。 5基列人占据约旦河各渡口,不让以法莲人过去。如果有以法莲的逃兵请求过河,基列人便问他:“你是以法莲人吗?”如果他否认, 6他们就让他说“示播列”。因为以法莲人咬字不清,如果有人把“示播列”说成“西播列”,基列人便抓住他,在那里处死他。那时,有四万二千名以法莲人被杀。

7耶弗他以色列的士师六年,死后葬在基列的一座城里。

以比赞、以伦、押顿

8耶弗他死后,伯利恒以比赞以色列的士师。 9他有三十个儿子、三十个女儿,他从别的宗族给儿子们娶来三十个媳妇,又把女儿都嫁到别的宗族。他做以色列的士师七年, 10死后葬在伯利恒11以比赞死后,西布伦以伦以色列的士师十年。 12他死后葬在西布伦亚雅仑13以伦死后,比拉顿希列的儿子押顿以色列的士师。 14他有四十个儿子、三十个孙子,他的儿孙每人骑一头驴。押顿以色列的士师八年, 15死后葬在以法莲比拉顿,在亚玛力人的山区。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waamuzi 12:1-15

Yefta Na Efraimu

112:1 Yos 13:27; Amu 11:1; 8:1Watu wa Efraimu wakaita majeshi yao, wakavuka kwenda Zafoni, wakamwambia Yefta, “Kwa nini mmekwenda kupigana na Waamoni bila kutuita ili twende pamoja nawe? Basi tutaichoma moto nyumba yako, pamoja nawe ukiwa ndani yake.”

2Yefta akajibu, “Mimi na watu wangu tulikuwa na ugomvi mkubwa na Waamoni, hata ingawa niliwaita hamkuniokoa katika mkono wao. 312:3 Amu 9:17; Kum 20:7; 1Sam 19:5; Ay 13:14Nilipoona kuwa hamkunipa msaada nikauhatarisha uhai wangu na nikavuka kupigana na Waamoni. Naye Bwana akanipatia ushindi dhidi yao. Sasa kwa nini mnanijia leo ili kupigana nami?”

412:4 1Fal 17:1; Mwa 46:20; Isa 9:21; 19:2Ndipo Yefta akakusanya watu wa Gileadi pamoja na kupigana na Efraimu. Wagileadi wakawashinda Efraimu, kwa kuwa Waefraimu walisema, “Ninyi Wagileadi ni watoro mliotoroka toka Efraimu na Manase.” 512:5 Yos 2:5-7; Amu 3:28Wagileadi wakaviteka vivuko vya Yordani dhidi ya hao Waefraimu, kisha ilikuwa yeyote yule aliyenusurika katika Efraimu aliposema, “Niache nivuke,” hao watu wa Gileadi walimuuliza, “Je wewe ni Mwefraimu?” Kama alijibu “Hapana,” 6walimwambia, “Sawa, sema ‘Shibolethi.’ ” Iwapo alitamka, “Sibolethi,” kwa sababu hakuweza kutamka hilo neno sawasawa, walimkamata na kumuua hapo kwenye vivuko vya Yordani. Waefraimu 42,000 waliuawa wakati huo.

7Yefta akawa mwamuzi wa Waisraeli kwa muda wa miaka sita. Basi Yefta akafa, akazikwa katika mmojawapo wa miji ya Gileadi.

Ibzani, Eloni Na Abdoni

812:8 Mwa 35:19Baada yake, Ibzani wa Bethlehemu akawa mwamuzi wa Israeli. 9Alikuwa na wana thelathini na binti thelathini. Akawaoza binti zake kwa watu wengine nje ya ukoo wake, na kuwatwalia wanawe wanawake thelathini toka nje ya ukoo wake. Ibzani akawa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka saba. 10Ibzani akafa, akazikwa huko Bethlehemu.

11Baada yake Eloni, Mzabuloni, akawa mwamuzi wa Israeli, naye akawaamua kwa muda wa miaka kumi. 1212:12 Yos 10:12Kisha Eloni akafa, akazikwa katika Aiyaloni, katika nchi ya Zabuloni.

1312:13 2Sam 23:30; 1Nya 11:31; 27:14Baada yake, Abdoni mwana wa Hileli, Mpirathoni, akawa mwamuzi wa Israeli. 1412:14 Amu 8:30; 5:10; 10:4Naye akazaa wana arobaini na wana wa wanawe thelathini waliopanda punda sabini. Akawa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka minane. 1512:15 Amu 5:14Ndipo Abdoni mwana wa Hileli, Mpirathoni, akafa, naye akazikwa huko Pirathoni katika Efraimu, katika nchi ya vilima ya Waamaleki.