哈该书 1 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

哈该书 1:1-15

耶和华命令百姓重建圣殿

1大流士王执政第二年六月一日,耶和华借着先知哈该撒拉铁的儿子犹大省长所罗巴伯约撒答的儿子大祭司约书亚说:

2“万军之耶和华说,‘这些百姓说,重建耶和华殿的时候还没到。’” 3因此,耶和华对先知哈该说: 4“这殿还是一片废墟,你们却住在华丽的房子里。 5万军之耶和华说,你们要认真反省自己的行为。 6你们种多收少,吃不饱,喝不足,穿不暖,挣来的工钱却放在漏口袋中。”

7万军之耶和华说:“你们要认真反省自己的行为。 8你们要上山伐木,重建这殿,好让我欢喜并得到尊崇。这是耶和华说的。 9你们盼望丰收,结果收的很少;你们把收成带回家,我却把它们吹走。这是什么缘故?万军之耶和华告诉你们,‘因为你们都忙于建自家的房子,任由我的殿一片废墟。 10所以,天不降雨露,地无出产。 11我让旱灾临到大地、群山、五谷、葡萄、橄榄等地里的出产以及人畜,使你们一切的劳碌付诸东流。’”

12撒拉铁的儿子犹大省长所罗巴伯约撒答的儿子大祭司约书亚和所有的余民1:12 余民”指“从流亡之地归回的人”。听到他们的上帝耶和华借先知哈该所讲的话,都顺服耶和华的话。百姓都敬畏耶和华。 13耶和华的使者哈该向百姓传达耶和华的话,说:“耶和华说,‘我与你们同在。’” 14耶和华感动撒拉铁的儿子犹大省长所罗巴伯约撒答的儿子大祭司约书亚和所有的余民,他们就动工建造他们的上帝万军之耶和华的殿, 15时值大流士王执政第二年六月二十四日。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hagai 1:1-15

Wito Wa Kuijenga Nyumba Ya Bwana

11:1 Ezr 4:24; 5:1-3; 2:2; 3:2; 1Nya 3:19; 6:15; Mt 1:12-13Katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario wa Uajemi, katika siku ya kwanza ya mwezi wa sita, neno la Bwana lilikuja kupitia kwa nabii Hagai kwenda kwa Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda na kwa Yoshua1:1 Yoshua kwa Kiebrania ni Yeshua, maana yake ni Yehova ni wokovu. mwana wa kuhani mkuu Yehosadaki:

21:2 Isa 13:4; 29:13Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Hawa watu husema, ‘Wakati haujawadia wa kujenga nyumba ya Bwana.’ ”

31:3 Ezr 5:1Kisha neno la Bwana likaja kupitia kwa nabii Hagai: 41:4 2Sam 7:2; Yer 33:12“Je, ni wakati wenu ninyi wa kuishi katika nyumba zenu zilizojengwa vizuri, wakati hii nyumba ikibaki, gofu?”

51:5 Mao 3:40; Hag 2:15-18Sasa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu. 61:6 Law 26:20; Isa 5:10; 9:20; 55:2; Amo 4:8; Hag 2:16; Zek 8:10Mmepanda vingi, lakini mmevuna haba. Mnakula lakini hamshibi, mnakunywa, lakini hamtosheki. Mnavaa nguo, lakini hamsikii joto. Mnapata mishahara, lakini inatoweka kama imewekwa kwenye mfuko uliotobokatoboka.”

7Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu. 81:8 Ay 22:3; Yer 13:11; 1Nya 14:1; Za 132:13-14; Kut 29:43Pandeni milimani mkalete miti na kujenga nyumba, ili nipate kuifurahia, na nitukuzwe,” asema Bwana. 91:9 Kum 28:38; Isa 5:10; Neh 13:11; Za 103:16; Eze 22:21“Mlitarajia mengi, kumbe, yametokea kidogo. Ulichokileta nyumbani nilikipeperusha. Kwa nini?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Ni kwa sababu ya nyumba yangu, inayobaki katika hali ya magofu, wakati kila mmoja wenu anajishughulisha na nyumba yake mwenyewe. 101:10 Kum 28:24; Mwa 27:28; 1Fal 17:1; 2Nya 6:26; Yer 3:3; Law 26:19; Yoe 1:18-19Kwa hiyo, kwa sababu yenu mbingu zimezuia umande wake na ardhi mavuno yake. 111:11 Kum 11:26; 28:22; Rut 1:1; 1Fal 17:1; Hag 2:17; Isa 5:6; 7:25; Hes 18:12Niliita ukame mashambani na milimani, kwenye nafaka, mvinyo mpya, mafuta pamoja na chochote kinachozalishwa na ardhi, juu ya watu na ngʼombe, pamoja na kazi za mikono yenu.”

121:12 Isa 1:9; 50:10; 55:11; Mt 28:20; Kum 31:12; Hag 2:2; Ezr 5:2; Mhu 12:13; Ay 36:11Kisha Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yoshua kuhani mkuu mwana wa Yehosadaki, pamoja na mabaki yote ya watu wakaitii sauti ya Bwana Mungu wao pamoja na ujumbe wa nabii Hagai, kwa sababu alikuwa ametumwa na Bwana Mungu wao. Watu walimwogopa Bwana.

131:13 Hes 14:9; 27:21; 2Nya 15:2; 36:15; Mwa 26:3; Rum 8:31; Isa 41:10; Mt 28:20Kisha Hagai, mjumbe wa Bwana, akawapa watu ujumbe huu wa Bwana: “Mimi niko pamoja nanyi,” asema Bwana. 141:14 Ezr 5:2; Za 110:3; 2Nya 36:22; Hag 2:21; 1Nya 6:15; 1Kor 15:58Kwa hiyo Bwana akachochea roho ya Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, na roho ya kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, pamoja na roho za mabaki yote ya watu. Walikuja wakaanza kufanya kazi katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wao, 151:15 Hag 2:10, 20; Ezr 4:24katika siku ya ishirini na nne mwezi wa sita, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario.