哈巴谷书 3 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

哈巴谷书 3:1-19

哈巴谷的祷告

1以下是哈巴谷先知的祷告,采用流离调3:1 流离调是希伯来诗歌的一种曲调。

2耶和华啊,我听过你的威名;

耶和华啊,我对你的作为充满敬畏。

求你如今再次彰显你的作为,

求你发怒的时候仍以怜悯为念。

3上帝从提幔来,

圣者从巴兰山来。(细拉)

祂的荣耀遮蔽诸天,

颂赞祂的声音响彻大地。

4祂的荣光犹如太阳的光辉,

祂的手射出光芒,

其中蕴藏着大能。

5瘟疫行在祂前面,

灾病跟在祂脚后。

6祂停下,大地就震动;

祂观看,万民就战栗。

古老的山岳崩裂,

远古的丘陵塌陷,

但祂的作为永远不变。

7我看见古珊的帐篷遭难,

米甸人的幔子颤抖。

8耶和华啊,你是向江河发怒吗?

你乘着得胜的战车而来,

是向江河生气吗?

是向海洋发怒吗?

9你拿出弓,要射出许多箭羽。(细拉)

你以江河分开大地。

10群山看见你就战栗,

大雨倾盆,

深渊翻腾,波浪滔天。

11你射出的箭闪闪发光,

你的枪熠熠生辉,

以致日月都停在天上。

12你怀着烈怒走遍大地,

践踏万国。

13你出来是为了拯救你的子民,

拯救你膏立的王。

你打垮邪恶之人的首领,

从头到脚彻底毁灭他们。(细拉)

14他们的军队如旋风而至,

要驱散我们,

他们以暗中吞噬贫民为乐,

但你用他们的矛刺透他们的头颅。

15你骑马践踏汹涌的大海。

16我听到这些,

就胆战心惊,嘴唇哆嗦,

四肢无力,双腿发抖。

但我仍要静候灾难临到入侵者的日子。

17即使无花果树不发芽,

葡萄树不结果,

橄榄树无收成,

田地不产粮,

圈里没有羊,

棚里没有牛,

18我仍要因耶和华而欢欣,

因拯救我的上帝而喜乐。

19主耶和华是我的力量,

祂使我的脚如母鹿的蹄,

稳行在高处。

这首歌交给乐长,用弦乐器伴奏。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Habakuki 3:1-19

Maombi Ya Habakuki

1Sala ya nabii Habakuki iliyoimbwa kwa shigionothi.3:1 Ni kifaa cha uimbaji chenye nyuzi; pia maombi kutumia kifaa hiki.

23:2 Ay 26:14; Za 119:120; 90:16; 44:1; 85:6; Isa 54:8Bwana, nimezisikia sifa zako;

nami naogopa kwa matendo yako, Ee Bwana.

Fufua kazi yako katikati ya miaka,

katikati ya miaka tangaza habari yako;

katika ghadhabu kumbuka rehema.

33:3 Mwa 36:11, 15; Isa 31:1; Hes 10:12; Za 48:10Mungu alitoka Temani,

yeye Aliye Mtakatifu kutoka Mlima Parani.

Utukufu wake ulifunika mbingu,

na sifa zake zikaifunika dunia.

43:4 Isa 18:4; Ay 9:6Mngʼao wake ulikuwa kama jua lichomozalo;

mionzi ilimulika kutoka mkononi mwake,

ambako nguvu zake zilifichwa.

53:5 Law 26:25Tauni ilimtangulia;

maradhi ya kuambukiza yalifuata nyayo zake.

63:6 Za 46:2; 114:1-6; 18:7; Kut 19:18; 23:31; Kum 32:8; Hes 21:24, 34; Mwa 49:26; 21:33Alisimama, akaitikisa dunia;

alitazama, na kuyafanya mataifa yatetemeke.

Milima ya zamani iligeuka mavumbi

na vilima vilivyozeeka vikaanguka.

Njia zake ni za milele.

73:7 Mwa 25:2; Hes 25:15; Amu 7:24-25; Kut 15:14Niliona watu wa Kushani katika dhiki,

na makazi ya Midiani katika maumivu makali.

83:8 Kut 7:20; 14:21, 22; 2Fal 2:11; Za 77:16; 68:17Ee Bwana, uliikasirikia mito?

Je, ghadhabu yako ilikuwa dhidi ya vijito?

Je, ulighadhibikia bahari

ulipoendesha farasi wako

na magari yako ya ushindi?

93:9 Kum 32:23; Za 7:12-13Uliufunua upinde wako

na kuita mishale mingi.

Uliigawa dunia kwa mito;

103:10 Za 77:16; 98:7; 93:3milima ilikuona ikatetemeka.

Mafuriko ya maji yakapita huko;

vilindi vilinguruma

na kuinua mawimbi yake juu.

113:11 Yos 10:13; Za 18:14; 144:6; Zek 9:14Jua na mwezi vilisimama kimya mbinguni

katika mngʼao wa mishale yako inayoruka,

na katika mngʼao wa mkuki wako umeremetao.

123:12 Za 44:2, 3; Mik 4:13; Isa 41:15Kwa ghadhabu ulipita juu ya dunia,

na katika hasira ulikanyaga mataifa.

133:13 Kut 13:21; Za 20:6; 28:8; 68:21; 2Sam 5:20; 23:1Ulikuja kuwaokoa watu wako,

kumwokoa uliyemtia mafuta.

Ulimponda kiongozi wa nchi ya uovu,

ukamvua toka kichwani hadi wayo.

143:14 Amu 7:22; Za 64:2-5Kwa mkuki wake mwenyewe ulitoboa kichwa chake

wakati mashujaa wake walifurika nje kwa kishindo kututawanya,

wakifurahi kama walio karibu kutafuna

wale wanyonge waliokuwa mafichoni.

153:15 Ay 9:8; Kut 15:8Ulikanyaga bahari kwa farasi wako,

ukisukasuka maji makuu.

163:16 Ay 4:14; Za 37:7Nilisikia na moyo wangu ukagonga kwa nguvu,

midomo yangu ikatetemeka kwa hofu niliposikia sauti;

uchakavu ukanyemelea mifupa yangu,

na miguu yangu ikatetemeka.

Hata hivyo nitasubiri kwa uvumilivu siku ya maafa

kuyajilia mataifa yaliyotuvamia.

173:17 Yoe 1:10-18; 2Kor 4:8, 9; Yer 5:17Ingawa mtini hauchanui maua

na hakuna zabibu juu ya mizabibu,

ingawaje mzeituni hauzai,

na hata mashamba hayatoi chakula,

iwapo hakuna kondoo katika banda,

wala ngʼombe katika zizi,

183:18 Za 42:5; 97:12; Isa 61:10; Kut 15:2; Lk 1:47; Flp 4:4hata hivyo nitashangilia katika Bwana,

nitamfurahia Mungu Mwokozi wangu.

193:19 Kum 32:13; 33:29; Za 27:1; 46:1-5; 18:33Bwana Mwenyezi ni nguvu yangu;

huifanya miguu yangu kama miguu ya ayala,

huniwezesha kupita juu ya vilima.

Kwa kiongozi wa uimbaji. Kwa vinanda vyangu vya nyuzi.