历代志上 7 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

历代志上 7:1-40

以萨迦的后裔

1以萨迦的四个儿子是陀拉普瓦雅述伸仑2陀拉的儿子是乌西利法雅耶勒雅买易伯散示姆利,他们都是陀拉宗族的族长。在大卫执政年间,陀拉家共有两万二千六百个英勇的战士。 3乌西的儿子是伊斯拉希伊斯拉希的儿子是米迦勒俄巴底亚约珥伊示雅,他们五人都是族长。 4他们妻儿众多,因此各宗族中可以出征作战的共有三万六千人。 5按家谱的记载,以萨迦支派的各族中共有八万七千个英勇的战士。

便雅悯的后裔

6便雅悯的三个儿子是比拉比结耶叠7比拉的五个儿子是以斯本乌西乌薛耶利摩以利,他们都是族长,是英勇的战士。按家谱记载,他们宗族共有两万二千零三十四个战士。 8比结的儿子是细米拉约阿施以利以谢以利约乃暗利耶利摩亚比雅亚拿突亚拉篾9比结的儿子都是族长。按家谱的记载,他们宗族共有两万零二百个英勇的战士。 10耶叠的儿子是比勒罕比勒罕的儿子是耶乌斯便雅悯以忽基拿拿细坦他施亚希沙哈11这些耶叠的儿子都是族长,宗族中可以英勇作战的共一万七千二百人。 12以珥的儿子是书品户品亚黑的儿子是户伸

拿弗他利的后裔

13拿弗他利的儿子是雅薛沽尼耶色沙龙。他们都是辟拉的后代。

玛拿西的后裔

14玛拿西的妾是亚兰人,她给玛拿西生的儿子是亚斯列,另外还生了基列的父亲玛吉15玛吉娶了户品书品的妹妹玛迦玛拿西的次子名叫西罗非哈西罗非哈只有几个女儿。 16玛吉的妻子玛迦生了一个儿子,给他取名叫毗利施毗利施的兄弟名叫示利施示利施的儿子是乌兰利金17乌兰的儿子是比但。这些都是基列的子孙。基列玛吉的儿子,玛吉玛拿西的儿子。 18基列的妹妹哈摩利吉生了伊施何亚比以谢玛拉19示米大的儿子是亚现示剑利克希阿尼安

以法莲的后裔

20以法莲的后代有书提拉书提拉的儿子是比列比列的儿子是他哈他哈的儿子是以拉大以拉大的儿子是他哈21他哈的儿子是撒拔撒拔的儿子是书提拉以法莲的另外两个儿子以谢以列因为偷迦特人的牲畜而被当地人杀死了。 22他们的父亲以法莲为他们悲伤了多日,亲戚都来安慰他。 23后来,以法莲与妻子同房,妻子怀孕,生了一个儿子。以法莲因家里遭遇不幸,就给孩子取名叫比利亚7:23 比利亚”意思是“不幸”。24以法莲有一个女儿叫舍伊拉,她建了上伯·和仑、下伯·和仑乌羡·舍伊拉25比利亚的儿子是利法利悉利悉的儿子是他拉他拉的儿子是他罕26他罕的儿子是拉但拉但的儿子是亚米忽亚米忽的儿子是以利沙玛27以利沙玛的儿子是的儿子是约书亚28以法莲人的地业和住处包括伯特利及其四围的村庄、东部的拿兰、西部的基色及其四围的村庄、示剑及其四围的村庄,远至迦萨及其四围的村庄。 29玛拿西人的地业包括伯·善他纳米吉多多珥以及它们四围的村庄。这些是以色列之子约瑟的后代居住的地方。

亚设的后裔

30亚设的儿子是音拿亦施瓦亦施韦比利亚,女儿是西拉31比利亚的儿子是希别玛结玛结的儿子是比撒威32希别的儿子是雅弗勒朔默何坦,女儿是书雅33雅弗勒的儿子是巴萨宾哈亚施法。这三人是雅弗勒的儿子。 34朔默的儿子是亚希罗迦耶户巴亚兰35朔默的兄弟希连的儿子是琐法音那示利斯亚抹36琐法的儿子是书亚哈尼弗书阿勒比利音拉37比悉河得珊玛施沙益兰比拉38益帖的儿子是耶孚尼毗斯巴亚拉39乌拉的儿子是亚拉汉尼业利谢40这些都是亚设的后代。他们都是族长,是英勇的战士和杰出的首领。按照家谱的记载,他们宗族中可以出征作战的共有两万六千人。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 7:1-40

Wana Wa Isakari

17:1 Mwa 30:18; Hes 26:23; Mwa 46:13Wana wa Isakari walikuwa:

Tola, Pua, Yashubu na Shimroni; wote ni wanne.

27:2 2Sam 24:1-2; 1Nya 21:1-5; 27:1Wana wa Tola walikuwa:

Uzi, Refaya, Yerieli, Yahmai, Ibsamu na Shemueli waliokuwa viongozi wa jamaa zao. Wakati wa utawala wa Mfalme Daudi, wazao wa Tola walioorodheshwa kama wapiganaji katika ukoo wao walikuwa watu 22,600.

37:3 1Nya 5:24Mwana wa Uzi alikuwa:

Izrahia.

Wana wa Izrahia walikuwa:

Mikaeli, Obadia, Yoeli na Ishia. Wote hawa watano walikuwa wakuu wao. 4Kulingana na ukoo wa jamaa zao, walikuwa na watu hodari wa vita wapatao 36,000, kwa sababu walikuwa na wanawake na watoto wengi.

5Jamaa ya watu waliokuwa wapiganaji hodari kutoka koo zote za Isakari, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, jumla yao walikuwa 87,000.

Wana Wa Benyamini

67:6 Mwa 46:21; Hes 26:38Wana watatu wa Benyamini walikuwa:

Bela, Bekeri na Yediaeli.

7Wana wa Bela walikuwa:

Esboni, Uzi, Uzieli, Yeremothi na Iri; walikuwa viongozi wa jamaa zao; wote ni watano. Watu wapiganaji walioorodheshwa katika ukoo wao walikuwa 22,034.

8Wana wa Bekeri walikuwa:

Zemira, Yoashi, Eliezeri, Elioenai, Omri, Yeremothi, Abiya, Anathothi na Alemethi. Hawa wote walikuwa wana wa Bekeri. 97:9 Kum 10:8Orodha ya ukoo wao iliyoandikwa viongozi wa jamaa zao walikuwa wapiganaji 20,200.

10Mwana wa Yediaeli alikuwa:

Bilhani.

Wana wa Bilhani walikuwa:

Yeushi, Benyamini, Ehudi, Kenaana, Zethani, Tarshishi na Ahishahari. 11Hawa wana wote wa Yediaeli walikuwa viongozi wa jamaa zao. Kulikuwako wanaume wapiganaji 17,200 waliokuwa tayari kwenda vitani.

127:12 Hes 26:38-39Washupimu na Wahupimu walikuwa wazao wa Iri. Wahushimu walikuwa wazao wa Aheri.

Wana Wa Naftali

137:13 Mwa 30:8; 46:24Wana wa Naftali walikuwa:

Yahzieli, Guni, Yeseri na Shalumu; hao walikuwa wazao wa Bilha.

Wana Wa Manase

147:14 Mwa 41:51; Yos 17:1; Hes 26:30Wana wa Manase walikuwa:

Asirieli alikuwa mzao wake kutokana na suria wake wa Kiaramu. Huyu suria akamzaa Makiri baba wa Gileadi. 157:15 Hes 26:33; 36:1-12; 27:1-11Makiri akatwaa mke kutoka miongoni mwa Wahupimu na Washupimu. Jina la dada yake aliitwa Maaka. Mwana wa pili wa Makiri aliitwa Selofehadi, ambaye alikuwa na wasichana tu. 16Maaka mkewe Makiri akamzaa mwana aliyemwita Pereshi. Jina la nduguye lilikuwa Shereshi. Wana wa Pereshi walikuwa Ulamu na Rakemu.

177:17 Hes 26:30; 1Sam 12:11Mwana wa Ulamu alikuwa:

Bedani.

Hawa ndio waliokuwa wana wa Gileadi mwana wa Makiri, mwana wa Manase. 187:18 Yos 17:2Dada yake aliyeitwa Hamolekethi aliwazaa Ish-Hodi, Abiezeri na Mahla.

19Wana wa Shemida walikuwa:

Ahiani, Shekemu, Liki na Aniamu.

Wana Wa Efraimu

207:20 Mwa 41:52; Hes 26:35; Mwa 48:14-20; Kum 33:13, 17; Za 60:7; 108:8Wana wa Efraimu walikuwa:

Shuthela, ambaye alimzaa Beredi,

Beredi akamzaa Tahathi, Tahathi akazaa Eleada,

Eleada akamzaa Tahathi, 21Tahathi akamzaa Zabadi,

na Zabadi akamzaa Shuthela.

Ezeri na Eleadi waliuawa na wenyeji wa Gathi walipokuwa wamekwenda huko kuwanyangʼanya mifugo yao. 227:22 Mwa 37:34-35; Yos 7:6; 2Sam 3:31; Ay 2:11; Za 69:11; Yoe 2:13; Yn 1:19Baba yao Efraimu akawaombolezea kwa siku nyingi, na jamaa zake wakaja kumfariji. 237:23 Mwa 35:18; 1Sam 4:21; 1Nya 4:9Kisha akakutana kimwili na mke wake tena, naye akachukua mimba, akamzalia mwana. Akamwita Beria, kwa sababu ya misiba iliyoipata nyumba yake. 247:24 Yos 10:10; 16:3, 5; 16:3; 1Sam 13:18; 2Nya 8:5Beria alikuwa na binti jina lake Sheera. Huyu ndiye aliijenga miji ya Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, pamoja na Uzen-Sheera.

25Beria akamzaa pia Refa, naye Refa akamzaa Reshefu,

Reshefu akamzaa Tela, Tela akamzaa Tahani,

26Tahani akamzaa Ladani, Ladani akamzaa Amihudi,

Amihudi akamzaa Elishama, 277:27 Hes 13:8, 16Elishama akamzaa Nuni,

Nuni akamzaa Yoshua.

287:28 Yos 10:33; 16:7Nchi zao na makazi yao yalijumuisha Betheli na vijiji vilivyouzunguka, Naarani ilikuwa upande wa mashariki, Gezeri pamoja na vijiji vyake upande wa magharibi, pia Shekemu na vijiji vyake hadi kufikia Aya na vijiji vyake. 297:29 Yos 17:11; 11:2; 1Fal 9:15; Amu 1:22-29Katika mipaka ya Manase walikuwepo Beth-Shani, Taanaki, Megido na Dori pamoja na vijiji vyake. Wana wa Yosefu mwana wa Israeli waliishi katika miji hii.

Wana Wa Asheri

307:30 Mwa 40:17; Hes 26:44; Mwa 49:20; Kum 33:24Wana wa Asheri walikuwa:

Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera.

31Wana wa Beria walikuwa:

Heberi na Malkieli, aliyekuwa baba yake Birzaithi.

32Heberi akawazaa Yafleti, Shomeri na Hothamu, na Shua dada yao.

33Wana wa Yafleti walikuwa:

Pasaki, Bimhali na Ashvathi.

Hawa walikuwa wana wa Yafleti.

34Wana wa Shemeri walikuwa:

Ahi, Roga, Yehuba na Aramu.

35Wana wa Helemu ndugu yake walikuwa:

Sofa, Imna, Sheleshi na Amali.

36Wana wa Sofa walikuwa:

Sua, Harneferi, Shuali, Beri, Imra, 37Bezeri, Hodu, Shama, Shilsha, Ithrani7:37 Kwa jina lingine Yetheri. na Beera.

38Wana wa Yetheri walikuwa:

Yefune, Pispa na Ara.

39Wana wa Ula walikuwa:

Ara, Hanieli na Risia.

407:40 Kum 2:14Hawa wote ndio waliokuwa wazao wa Asheri, viongozi wa jamaa zao, watu bora, mashujaa walio hodari na viongozi maarufu. Idadi ya watu waliokuwa tayari kwa vita, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, walikuwa 26,000.