历代志上 2 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

历代志上 2:1-55

以色列的后裔

1以色列的儿子是吕便西缅利未犹大以萨迦西布伦2约瑟便雅悯拿弗他利迦得亚设

犹大的后裔

3犹大的儿子是俄南示拉。这三人是迦南书亚的女儿生的。犹大的长子在耶和华眼中是个邪恶的人,因而被耶和华击杀了。 4犹大的儿媳她玛犹大生了法勒斯谢拉犹大共有五个儿子。 5法勒斯的儿子是希斯仑哈姆勒6谢拉的五个儿子是心利以探希幔甲各大拉7迦米的儿子是亚干,这亚干私藏本该毁灭的东西,连累了以色列人。 8以探的儿子是亚撒利雅

9希斯仑的儿子是耶拉篾迦勒2:9 迦勒”希伯来文是“基路拜”,“迦勒”的另一种拼法。10亚米拿达亚米拿达拿顺拿顺犹大人的首领。 11拿顺撒门撒门波阿斯12波阿斯俄备得俄备得耶西13耶西生长子以利押、次子亚比拿达、三子示米亚14四子拿坦业、五子拉代15六子阿鲜、七子大卫16他们的姊妹是洗鲁雅亚比该洗鲁雅的三个儿子是亚比筛约押亚撒黑17亚比该亚玛撒亚玛撒的父亲是以实玛利益帖

希斯仑的后裔

18希斯仑的儿子迦勒和妻子阿苏巴生了儿子,他也和耶略生了儿子。阿苏巴的儿子是耶设朔罢押墩19阿苏巴死后,迦勒又娶了以法她,生了户珥20户珥乌利乌利比撒列21希斯仑六十岁娶玛吉的女儿,与她生了西割玛吉基列的父亲。 22西割雅珥雅珥基列有二十三座城邑。 23后来基述人和亚兰人夺取了雅珥的城邑,包括基纳及其附近的六十个村落。这些人都是基列的父亲玛吉的后代。 24希斯仑死在迦勒·以法他后,他的妻子亚比雅给他生了亚施户亚施户提哥亚的父亲。

耶拉篾的后裔

25希斯仑的长子耶拉篾生了长子,又生了布拿阿连阿鲜亚希雅26耶拉篾的另一个妻子名叫亚他拉,是阿南的母亲。 27耶拉篾的长子的儿子是玛斯雅悯以结28阿南的儿子是沙迈雅大沙迈的儿子是拿答亚比述29亚比述的妻子名叫亚比孩,他们生了亚班摩利30拿答的儿子是西列亚遍西列死后没有留下儿子。 31亚遍的儿子是以示以示的儿子是示珊示珊的儿子是亚来32沙迈的兄弟雅大的儿子是益帖约拿单益帖死后没有留下儿子。 33约拿单的儿子是比勒撒萨。这些人都是耶拉篾的子孙。 34示珊没有儿子,只有女儿,还有一个名叫耶哈埃及仆人。 35示珊把女儿嫁给仆人耶哈,他们生了亚太36亚太拿单拿单撒拔37撒拔以弗拉以弗拉俄备得38俄备得耶户耶户亚撒利雅39亚撒利雅希利斯希利斯以利亚萨40以利亚萨西斯迈西斯迈沙龙41沙龙耶加米雅耶加米雅以利沙玛

迦勒的后裔

42耶拉篾的兄弟迦勒的长子是西弗的父亲米沙希伯仑的父亲玛利沙也是迦勒的儿子。 43希伯仑的儿子是可拉他普亚利肯示玛44示玛拉含拉含约干的父亲。利肯沙迈45沙迈的儿子是玛云玛云是伯·夙的父亲。 46迦勒的妾以法哈兰摩撒迦谢哈兰迦谐47雅代的儿子是利健约坦基珊毗力以法沙亚弗48迦勒的妾玛迦示别特哈拿49麦玛拿的父亲沙亚弗抹比拿基比亚的父亲示法迦勒的女儿是押撒50这些人都是迦勒的子孙。 以法她的长子户珥生基列·耶琳的父亲朔巴51伯利恒的父亲萨玛伯迦得的父亲哈勒52基列·耶琳的父亲朔巴的子孙是哈罗以和半数米努·哈人。 53基列·耶琳的各宗族是以帖人、布特人、舒玛人、密来人,从这些宗族中又衍生出琐拉人和以实陶人。 54萨玛的后代是伯利恒人、尼陀法人、亚他绿·伯·约押人、半数玛拿哈人、琐利人, 55以及住在雅比斯的文书世家特拉人、示米押人和苏甲人。这些都是基尼人,是利甲家族的祖先哈末的后代。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 2:1-55

Wana Wa Israeli

12:1 Mwa 32:28; 35:10; Kut 32:13; Hes 1:5-15; 13:4-15; Mwa 29:32; 1Fal 18:31Hawa ndio waliokuwa wana wa Israeli:

Reubeni, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Zabuloni, 2Dani, Yosefu, Benyamini, Naftali, Gadi na Asheri.

Yuda

Hadi Wana Wa Hesroni

32:3 Mwa 29:35; 38:2; Hes 26:19Wana wa Yuda walikuwa:

Eri, Onani na Shela. Hawa watatu walizaliwa kwake na mkewe Mkanaani, binti wa Shua. Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu machoni pa Bwana, kwa hiyo Bwana alimuua. 42:4 Mwa 38:11-30; 11:31; 38:29Tamari, mkwewe Yuda, alimzalia wana wawili: Peresi na Zera. Yuda alikuwa na jumla ya wana watano.

52:5 Mwa 46:12; Hes 26:21; Rut 4:18Wana wa Peresi walikuwa:

Hesroni na Hamuli.

62:6 1Fal 4:31Wana wa Zera walikuwa:

Zimri, Ethani, Hemani, Kalkoli na Dara. Jumla ya wana wa Zera walikuwa watano.

72:7 Yos 7:1; 6:18; 1Nya 4:1Mwana wa Karmi alikuwa:

Akari,2:7 Akari maana yake Taabisha; pia anaitwa Akani (Yos 6:1-26; 22:20). ambaye alileta taabu kwa Waisraeli kwa kukiuka onyo la kutokuchukua vitu vilivyokuwa vimewekwa wakfu.

8Mwana wa Ethani alikuwa:

Azariya.

92:9 Hes 26:21Wana wa Hesroni walikuwa:

Yerameeli, Ramu na Kalebu.

Kuanzia Ramu Mwana Wa Hesroni

102:10 Lk 3:32-33; Kut 6:23; Hes 1:7; Rut 4:19Ramu alimzaa

Aminadabu, na Aminadabu akamzaa Nashoni, kiongozi wa kabila la Yuda. 11Nashoni akamzaa Salmoni, Salmoni akamzaa Boazi, 122:12 Rut 2:1; 4:17Boazi akamzaa Obedi, Obedi akamzaa Yese.

132:13 Rut 4:17; Isa 16:6Yese akawazaa

Eliabu mwanawe wa kwanza; wa pili Abinadabu, wa tatu Shimea,2:13 Au: Shima, maana yake Sifa njema (pia 1Sam 16:9; 17:13). 14wa nne Nethaneli, wa tano Radai, 15wa sita Osemu, na wa saba Daudi. 162:16 1Sam 26:6; 2Sam 2:18; 2:13Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili. Wana wa Seruya walikuwa watatu: Abishai, Yoabu na Asaheli. 172:17 2Sam 17:25Abigaili alikuwa mama yake Amasa, ambaye baba yake alikuwa Yetheri, Mwishmaeli.

Kalebu Mwana Wa Hesroni

18Kalebu mwana wa Hesroni akazaa wana na mkewe Azuba (na pia na Yeriothi). Hawa ndio wana Azuba aliomzalia Kalebu: Yesheri, Shobabu na Ardoni. 192:19 1Nya 2:42, 50Azuba alipofariki, Kalebu akamwoa Efrathi, ambaye alimzalia Huri. 202:20 Kut 32:2; 35:30; 2Nya 1:5Huri akamzaa Uri, Uri akamzaa Bezaleli.

212:21 Hes 21:1Hatimaye, Hesroni akakutana kimwili na binti wa Makiri babaye Gileadi (ambaye alimwoa alipokuwa na umri wa miaka sitini), naye akamzaa Segubu. 22Segubu akamzaa Yairi, ambaye alitawala miji ishirini na mitatu katika Gileadi. 232:23 Hes 32:41; 32:42; Yos 13:30; Kum 3:14(Lakini Geshuri na Aramu wakateka miji ya Hawoth-Yairi, pamoja na Kenathi na viunga vyake; jumla ilikuwa miji sitini.) Wote hawa walikuwa wazao wa Makiri babaye Gileadi.

242:24 1Nya 4:5; 2Nya 11:6; 20:20; 2Sam 14:2; Neh 3:5; Yer 6:1Baada ya Hesroni kufa huko Efrathi, Abiya mjane wa Hesroni akamzalia Ashuru, aliye baba wa Tekoa.

Yerameeli Mwana Wa Hesroni

25Wana wa Yerameeli mzaliwa wa kwanza wa Hesroni walikuwa:

Ramu mzaliwa wake wa kwanza, Buna, Oreni, Osemu na Ahiya. 26Yerameeli alikuwa na mke mwingine, aliyeitwa Atara, aliyekuwa mama yake Onamu.

27Wana wa Ramu mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli walikuwa:

Maasi, Yamini na Ekeri.

28Wana wa Onamu walikuwa:

Shamai na Yada.

Wana wa Shamai walikuwa:

Nadabu na Abishuri.

29Mke wa Abishuri aliitwa Abihaili, ambaye alimzalia Abani na Molidi.

30Wana wa Nadabu walikuwa

Seledi na Apaimu, lakini Seledi alikufa bila kuzaa watoto.

31Apaimu akamzaa:

Ishi ambaye alikuwa baba wa Sheshani.

Sheshani akamzaa Alai.

32Wana wa Yada, nduguye Shamai walikuwa:

Yetheri na Yonathani. Yetheri alikufa bila kuzaa watoto.

33Wana wa Yonathani walikuwa:

Pelethi na Zaza.

Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yerameeli.

34Sheshani hakuwa na watoto wa kiume, ila wasichana tu.

Alikuwa na mtumishi Mmisri aliyeitwa Yarha. 35Sheshani akamwoza huyu mtumishi wake Yarha binti yake, akamzalia mwana jina lake Atai.

362:36 1Nya 11:41Atai akamzaa Nathani,

Nathani akamzaa Zabadi,

37Zabadi akamzaa Eflali,

Eflali akamzaa Obedi,

38Obedi akamzaa Yehu,

Yehu akamzaa Azaria,

39Azaria akamzaa Helesi,

Helesi akamzaa Eleasa,

40Eleasa akamzaa Sismai,

Sismai akamzaa Shalumu,

41Shalumu akamzaa Yekamia,

naye Yekamia akamzaa Elishama.

Koo Za Kalebu

42Wana wa Kalebu nduguye Yerameeli walikuwa:

Mesha mzaliwa wake wa kwanza alimzaa Zifu, naye mwanawe Maresha akamzaa Hebroni.

43Hebroni alikuwa na wana wanne:

Kora, Tapua, Rekemu na Shema. 44Shema alikuwa baba yake Rahamu na Rahamu alikuwa baba wa Yorkeamu na Rekemu alikuwa baba wa Shamai. 452:45 Yos 15:55; 15:58Shamai akamzaa Maoni na Maoni akamzaa Beth-Suri.

46Efa, suria wa Kalebu alikuwa mamaye Harani, Mosa na Gazezi. Harani alikuwa baba wa Gazezi.

47Wana wa Yadai walikuwa:

Regemu, Yothamu, Geshani, Peleti, Efa na Shaafu.

48Maaka suria wa Kalebu alikuwa mamaye Sheberi na Tirhana. 492:49 Yos 15:31; 15:16Pia Maaka akamzaa Shaafu babaye Madmana, na Sheva babaye Makbena na Gibea. Kalebu alikuwa na binti jina lake Aksa. 502:50 1Nya 4:4; 2:19Hawa ndio waliokuwa wazao wa Kalebu.

Wana wa Huri, mzaliwa mkuu wao wa Efrathi, walikuwa:

Shobali akamzaa Kiriath-Yearimu, 51Salma akamzaa Bethlehemu, naye Harefu akamzaa Beth-Gaderi.

52Wazao wa Shobali, baba yake Kiriath-Yearimu, walikuwa:

Haroe, nusu ya wakazi wa mji wa Menuhothi, 532:53 2Sam 23:38pamoja na koo za Kiriath-Yearimu ambazo ni: Waithiri, Waputhi, Washumathi na Wamishrai. Kutokana na watu hawa walizaliwa Wasorathi na Waeshtaoli.

542:54 Ezr 2:22; Neh 12:28Wazao wa Salma walikuwa:

Bethlehemu, Wanetofathi, Atroth-Beth-Yoabu, nusu ya Wamanahathi, Wasori, 552:55 Mwa 15:19; Amu 1:16; Yos 19:35; 2Fal 10:15, 23; Yer 35:2-19; Amu 4:11; Hes 24:21-22pamoja na koo za waandishi zilizoishi katika mji wa Yabesi: yaani Watirathi, Washimeathi na Wasukathi. Hawa ndio Wakeni waliotokana na Hamathi, baba wa nyumba ya Rekabu.