历代志上 18 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

历代志上 18:1-17

大卫的胜利

1后来,大卫打败并征服了非利士人,夺取了迦特及其周围的村庄。 2他又打败了摩押人,使他们称臣、进贡。 3琐巴哈大底谢出来要巩固他在幼发拉底河一带的权势,大卫打败了他,一直攻到哈马4俘获一千辆战车、七千骑兵、两万步兵,砍断拉战车的马匹的蹄筋,只留下够拉一百辆战车的马匹。 5大马士革亚兰人前来支援琐巴哈大底谢大卫杀了他们两万二千人, 6还派军驻守亚兰国的大马士革亚兰人臣服大卫,向他进贡。耶和华使大卫无往而不胜。 7大卫夺走哈大底谢侍从的金盾牌,带回耶路撒冷8又从哈大底谢统治的提巴两座城中夺走大量的铜。后来所罗门用这些铜制造铜海、铜柱及各种铜器。

9哈马陀乌听说大卫打败琐巴哈大底谢全军, 10就派儿子哈多兰带着许多金银铜器去朝见大卫王,向他请安,祝贺他打败了哈大底谢。因为陀乌常常和哈大底谢交战。 11于是,大卫把这些器皿和他从以东摩押亚扪非利士亚玛力各国夺来的金银都分别出来,奉献给耶和华。

12洗鲁雅的儿子亚比筛在盐谷击杀了一万八千名以东人。 13大卫以东驻兵,以东人都臣服他。耶和华使他无往而不胜。

14大卫在全以色列秉公行义,治理百姓。 15那时,洗鲁雅的儿子约押做元帅,亚希律的儿子约沙法做史官, 16亚希突的儿子撒督亚比亚他的儿子亚希米勒做祭司长,沙威沙做书记, 17耶何耶大的儿子比拿雅统管基利提人和比利提人。大卫王的众子都在他左右做首领。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 18:1-17

Ushindi Wa Daudi

(2 Samweli 8:1-18)

1Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Gathi pamoja na vijiji vinavyouzunguka kutoka utawala wa Wafilisti.

218:2 Hes 24:17; 21:29Pia Daudi akawashinda Wamoabu, wakawa watumishi wake, nao wakawa wanamletea ushuru.

318:3 1Nya 19:6; Mwa 2:14; 15:18; Kum 11:24; 2Sam 8:3Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mfalme wa Soba, hadi Hamathi, wakati alikwenda kuimarisha utawala wake katika Mto Frati. 418:4 Mwa 49:6; 2Sam 8:4Daudi akateka magari ya vita 1,000 miongoni mwa magari yake, waendesha hayo magari ya kukokotwa na farasi 7,000 na askari wa miguu 20,000. Daudi akakata mishipa ya miguu ya nyuma ya farasi wote wakokotao magari, ila akabakiza 100.

518:5 2Fal 16:9; 1Nya 19:6Waaramu wa Dameski, walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao. 618:6 1Nya 17:8; Mit 21:31; Za 91:14; 121:8Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski. Basi Waaramu wakawa watumwa wa Daudi, na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.

7Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu. 818:8 1Fal 7:23; 2Nya 4:12-16Kutoka miji ya Tibhathi na Kuni, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Daudi akatwaa shaba nyingi sana, ambayo Solomoni aliitumia kutengenezea ile Bahari ya shaba, zile nguzo na vifaa mbalimbali vya shaba.

9Tou mfalme wa Hamathi aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri mfalme wa Soba, 1018:10 2Sam 8:10akamtuma mwanawe, Hadoramu kwa Mfalme Daudi ili kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Mfalme Hadadezeri, kwa kuwa alikuwa amepigana vita mara nyingi na Tou. Hadoramu akamletea Daudi vifaa mbalimbali vya dhahabu, fedha na shaba.

1118:11 Hes 24:18-20Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu aliyokuwa ameitwaa katika mataifa yote haya: Edomu na Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki.

1218:12 1Fal 11:15; 2Sam 7:13; 2Fal 14:7; 2Nya 25:11Abishai mwana wa Seruya akawaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi. 1318:13 Mwa 27:29; Hes 24:18; 1Sam 10:3; 13:3; 14:1Akaweka kambi za askari walinzi huko Edomu, nao Waedomu wote wakawa watumishi wa Daudi. Bwana akampa Daudi ushindi kila alipokwenda.

Maafisa Wa Daudi

1418:14 1Nya 29:26; 11:1-6Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote. 1518:15 2Sam 5:6-8Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu; 1618:16 2Sam 8:17; 1Nya 6:8; 24; 6Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Shausha alikuwa mwandishi; 1718:17 1Sam 30:14; 2Sam 8:18naye Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa maafisa wakuu katika utumishi wa mfalme.