历代志上 15 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

历代志上 15:1-29

约柜被运到耶路撒冷

1大卫大卫城为自己建造宫殿,并为上帝的约柜预备地方,支搭帐篷。 2大卫说:“除了利未人以外,谁也不可抬上帝的约柜,因为耶和华只拣选他们抬上帝的约柜,永远事奉祂。”

3大卫召集以色列人到耶路撒冷,要把耶和华的约柜抬到他所预备的地方。 4大卫又召集了亚伦的子孙和利未人: 5哥辖的后代乌列族长和他的一百二十个族人; 6米拉利的后代亚帅雅族长和他的二百二十个族人; 7革顺的后代约珥族长和他的一百三十个族人; 8以利撒番的后代示玛雅族长和他的二百个族人; 9希伯仑的后代以列族长和他的八十个族人; 10乌薛的后代亚米拿达族长和他的一百一十二个族人。

11大卫召来撒督亚比亚他两位祭司以及利未乌列亚帅雅约珥示玛雅以列亚米拿达12对他们说:“你们是利未人的族长,你们和你们的族人都要洁净自己,好将以色列的上帝耶和华的约柜抬到我所预备的地方。 13先前你们没有抬约柜,我们也没有按规矩求问我们的上帝耶和华,以致祂向我们发怒。” 14于是祭司和利未人就洁净自己,好将以色列的上帝耶和华的约柜抬上来。 15利未人按照耶和华借摩西颁布的命令,用杠把上帝的约柜抬在肩上。

16大卫又吩咐利未人的族长去派他们的族人做歌乐手,伴着琴瑟和钹的乐声欢唱。 17于是,利未人指派约珥的儿子希幔和他的亲族比利迦的儿子亚萨,以及他的亲族米拉利的后代古沙雅的儿子以探18协助他们的亲族有撒迦利雅雅薛示米拉末耶歇乌尼以利押比拿雅玛西雅玛他提雅以利斐利户弥克尼雅,以及守门的俄别·以东耶利

19歌乐手希幔亚萨以探负责敲铜钹, 20撒迦利雅雅薛示米拉末耶歇乌尼以利押玛西雅比拿雅负责鼓瑟,调用高音。 21玛他提雅以利斐利户弥克尼雅俄别·以东耶利亚撒西雅负责带领弹琴,调用低音。 22利未人的族长基拿尼雅善于歌唱,是歌乐手的领班。 23比利迦以利加拿负责看守约柜。 24祭司示巴尼约沙法拿坦业亚玛赛撒迦利雅比拿亚以利以谢负责在上帝的约柜前吹号,俄别·以东耶希亚也负责看守约柜。

25大卫以色列的长老以及千夫长去俄别·以东家,高高兴兴地将耶和华的约柜抬上来。 26耶和华上帝恩待抬约柜的利未人,他们就献上七头公牛和七只公羊为祭物。 27大卫和抬约柜的利未人、歌乐手及其领班基拿尼雅都穿上细麻衣,大卫还穿上细麻布的以弗得。 28以色列人把耶和华的约柜抬了上来,一路上欢呼吹角、鸣号、敲钹、鼓瑟、弹琴,大声奏乐。 29耶和华的约柜进大卫城的时候,扫罗的女儿米甲从窗户往外看,看见大卫王在兴高采烈地跳舞,心里就轻视他。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Nyakati 15:1-29

Sanduku La Agano Laletwa Yerusalemu

(2 Samweli 6:12-22)

115:1 Za 132:1-5; 2Sam 6:17; 1Nya 17:1-5; Mdo 7:46Baada ya Daudi kujijengea nyumba zake katika Mji wa Daudi, akatengeneza sehemu kwa ajili ya Sanduku la Mungu, kisha akasimamisha hema kwa ajili yake. 215:2 Hes 3:6; Kum 31:9, 25; 2Nya 29:11; Hes 4:2, 15; Kum 10:5; Yos 3:3Kisha Daudi akasema, “Hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kulibeba Sanduku la Mungu isipokuwa Walawi peke yao, kwa sababu Bwana aliwachagua kulibeba Sanduku la Bwana na kuhudumu mbele zake milele.”

315:3 1Nya 13:5; 1Fal 8:1Daudi akawakusanya Israeli wote huko Yerusalemu ili kulipandisha Sanduku la Bwana na kulileta hadi kwenye sehemu aliyokuwa ametengeneza kwa ajili yake. 4Kisha Daudi akawakusanya pamoja wazao wa Aroni na Walawi:

515:5 Kut 6:16-18Kutoka wazao wa Kohathi,

Urieli kiongozi na ndugu zake 120,

6Kutoka wazao wa Merari,

Asaya kiongozi na ndugu zake 220.

7Kutoka wazao wa Gershoni,15:7 Namna nyingine ya kutaja Gershomu.

Yoeli kiongozi na ndugu zake 130.

815:8 Kut 6:22Kutoka wazao wa Elisafani,

Shemaya kiongozi na ndugu zake 200.

915:9 Hes 26:58; Kut 6:18Kutoka wazao wa Hebroni,

Elieli kiongozi na ndugu zake 80.

10Kutoka wazao wa Uzieli,

Aminadabu kiongozi na ndugu zake 112.

1115:11 1Nya 12:28; 1Sam 22:20Kisha Daudi akawaita makuhani Sadoki na Abiathari, pamoja na Walawi Urieli, Asaya, Yoeli, Shemaya, Elieli na Aminadabu. 1215:12 Kut 29:10; Law 11:44; Eze 48:11; Yn 17:17; Law 10:3; 2Nya 5:11; 29:5, 15; Rum 12:1-2Akawaambia, “Ninyi ndio viongozi wa jamaa za Walawi. Ninyi pamoja na Walawi wenzenu inawapasa mjitakase na kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli hadi mahali ambapo nimetengeneza kwa ajili yake. 1315:13 1Fal 8:4; 2Sam 6:3; 1Nya 13:11Ilikuwa ni kwa sababu hii, ninyi Walawi, hamkulipandisha Sanduku la Bwana mara ya kwanza, hata ikasababisha Bwana Mungu wetu kuwaka hasira dhidi yetu. Hatukumuuliza jinsi ya kufanya ili tupate kulileta jinsi alivyoagiza.” 14Kwa hiyo makuhani pamoja na Walawi wakajitakasa ili kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli. 1515:15 Kut 25:14; Hes 4:5-15Nao Walawi wakalichukua Sanduku la Mungu mabegani mwao wakitumia mipiko, kama vile Mose alivyoamuru sawasawa na neno la Bwana.

1615:16 Ezr 2:41; Neh 11:23; Amo 6:5; Ay 21:12; Za 68:25; 1Nya 6:31; 13:8; Za 33:2Daudi akawaambia viongozi wa Walawi kuwaweka ndugu zao waimbaji ili waimbe nyimbo za shangwe, wakiwa na vyombo vya uimbaji: zeze, vinubi na matoazi.

1715:17 1Nya 6:33-44Basi Walawi wakawaweka Hemani mwana wa Yoeli; kutoka miongoni mwa ndugu zake, Asafu mwana wa Berekia; kutoka miongoni mwa ndugu zao Wamerari, Ethani mwana wa Kushaiya; 1815:18 2Sam 6:10; 1Nya 26:4-5hawa ndio waliochaguliwa kuwa wasaidizi wao: Zekaria, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaya, Maaseya, Matithia, Elifelehu, Mikneya, pamoja na mabawabu Obed-Edomu na Yehieli.

1915:19 1Nya 16:12-13; 29:26Waimbaji Hemani, Asafu na Ethani walichaguliwa kupiga matoazi ya shaba; 20Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Maaseya na Benaya walikuwa wapiga zeze kufuatana na sauti ya alamothi,15:20 Huenda ni aina ya uimbaji. 21na Matithia, Elifelehu, Mikneya, Obed-Edomu, Yehieli na Azazia walikuwa wapiga vinubi, wakiongozwa kwa kufuata sauti ya sheminithi.15:21 Huenda ni aina ya uimbaji. 22Kenania kiongozi wa Walawi alikuwa msimamizi wa uimbaji; huu ndio uliokuwa wajibu wake kwa sababu alikuwa stadi katika hilo.

23Berekia na Elikana walikuwa mabawabu kwa ajili ya Sanduku. 2415:24 2Nya 5:12; Hes 10:8; 2Nya 29:26; Za 81:3Shebania, Yoshafati, Nethaneli, Amasai, Zekaria, Benaya na Eliezeri, makuhani, walikuwa wapiga tarumbeta mbele ya Sanduku la Mungu. Obed-Edomu na Yehiya waliwekwa pia kuwa mabawabu wa Sanduku.

2515:25 2Sam 16:12-13; 2Nya 5:2; Yer 3:16; Kum 12:7, 18; Ezr 6:16Basi Daudi pamoja na wazee wa Israeli na majemadari wa vikosi vya elfu wakaenda ili kulipandisha Sanduku la Agano la Bwana kutoka nyumba ya Obed-Edomu kwa shangwe. 2615:26 Ay 42:8; Hes 23:1-4, 29Kwa sababu Mungu alikuwa amewasaidia Walawi waliokuwa wanalichukua Sanduku la Agano la Bwana, mafahali saba na kondoo dume saba walitolewa dhabihu. 27Basi Daudi alikuwa amevaa joho la kitani safi, kama walivyokuwa wamevaa Walawi wote waliokuwa wanalichukua lile Sanduku, waimbaji nao walivaa vivyo hivyo, pamoja na Kenania aliyekuwa anaongoza nyimbo za waimbaji. Daudi alivaa pia kisibau cha kitani safi. 2815:28 Kut 19:13; 1Nya 13:8Hivyo Israeli wote wakalipandisha Sanduku la Agano la Bwana kwa shangwe, wakipiga pembe za kondoo dume, tarumbeta, matoazi, wakipiga zeze na vinubi.

2915:29 2Sam 6:16; Mdo 2:13Sanduku la Agano la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akicheza na kusherehekea, akamdharau moyoni mwake.