利未记 15 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

利未记 15:1-33

有关漏症患者的条例

1耶和华对摩西亚伦说: 2“你们把以下条例告诉以色列人。

“如果有男人患了漏症,他下体的排泄物是不洁净的。 3不论他下体的排泄物止住与否,他都是不洁净的。 4他睡过的床或坐过的东西都不洁净。 5凡碰到他睡过的床的人都不洁净,必须洗衣、沐浴,等到傍晚才能洁净。 6凡坐他坐过之物的人都不洁净,必须洗衣、沐浴,等到傍晚才能洁净。 7凡碰到他的人都不洁净,必须洗衣、沐浴,等到傍晚才能洁净。 8如果他吐唾沫在一个洁净的人身上,那人便不洁净,必须洗衣、沐浴,等到傍晚才能洁净。 9他骑过的鞍子是不洁净的。 10凡碰到他坐过之物的人都不洁净,要等到傍晚才能洁净。碰到这些东西的人都不洁净,必须洗衣、沐浴,等到傍晚才能洁净。 11如果他没有洗手就碰到别人,那人便不洁净,必须洗衣、沐浴,等到傍晚才能洁净。 12必须打碎他摸过的陶器,用水清洗他摸过的木器。 13他病愈后,必须经过七天的洁净期,要洗净衣服,用清水沐浴,这样就洁净了。 14第八天,他要把两只斑鸠或雏鸽带到会幕门前,在耶和华面前交给祭司献祭, 15一只作赎罪祭,一只作燔祭。这样,祭司便在耶和华面前为他的漏症赎了罪。

有关遗精的条例

16“男人若遗精,便不洁净,必须沐浴全身,等到傍晚才能洁净。 17沾了精液的衣物或皮革都不洁净,必须用水清洗,等到傍晚才能洁净。 18如果男女同房,二人都不洁净,必须沐浴,等到傍晚才能洁净。

有关女人月经的条例

19“女人在月经期间,要不洁净七天。凡接触到她的人都不洁净,要等到傍晚才能洁净。 20月经期间,她躺过或坐过的东西都不洁净。 21凡碰过她床的人都不洁净,必须洗衣、沐浴,等到傍晚才能洁净。 22人若碰到她坐过的地方,也不洁净,必须洗衣、沐浴,等到傍晚才能洁净。 23不论是她的床,还是她坐的东西,碰到的人都不洁净,要等到傍晚才能洁净。 24男人若与她同房,沾染了她的经血,就要不洁净七天,他躺过的床也不洁净。

25“女人若在经期以外多日血漏或经期过长,在此期间便不洁净,像在经期内一样。 26在血漏期间,她躺的床或坐的东西都不洁净,像在经期内一样。 27凡碰到这些东西的人都不洁净,必须洗衣、沐浴,等到傍晚才能洁净。 28血漏停止后,她要等七天才洁净。 29第八天,她要把两只斑鸠或雏鸽带到会幕门口,交给祭司献祭, 30一只作赎罪祭,一只作燔祭。这样,祭司便在耶和华面前为她赎了血漏的不洁之罪。 31你们要使以色列人远离不洁之物,免得他们因玷污我的圣幕而死亡。”

32以上是为患漏症的人,包括遗精、 33行经的女人、患漏症的男女、与不洁净女人同房的男人所设立的条例。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Walawi 15:1-33

Kutokwa Na Umajimaji Usababishao Unajisi

1Bwana akawaambia Mose na Aroni, 215:2 Law 22:4; Hes 5:2; 2Sam 3:29; Mt 9:20; Mk 5:25; Lk 8:43“Semeni na Waisraeli mwaambie: ‘Wakati mtu yeyote anapotokwa na usaha mwilini, usaha huo ni najisi. 3Iwe unaendelea kutiririka kutoka mwilini mwake au umeziba, utamfanya kuwa najisi. Hivi ndivyo usaha wake utakavyomletea unajisi:

4“ ‘Kitanda chochote atakacholalia mtu mwenye kutokwa na usaha kitakuwa najisi, na chochote atakachokalia kitakuwa najisi. 515:5 Law 11:24-25; 14:8; 17:15; Ebr 9:10Yeyote atakayegusa kitanda chake ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni. 6Yeyote atakayeketi juu ya kitu chochote alichokalia mwenye kutokwa na usaha, ni lazima afue nguo zake, na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.

715:7 Law 22:4-5“ ‘Yeyote atakayemgusa mtu mwenye kutokwa na usaha, ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.

815:8 Hes 12:14; Ay 30:10; 2Kor 7:1“ ‘Ikiwa mtu mwenye kutokwa na usaha atamtemea mate mtu yeyote ambaye ni safi, mtu huyo ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.

9“ ‘Kila tandiko ambalo mtu huyo atalikalia wakati wa kupanda mnyama litakuwa najisi, 1015:10 Hes 19:10na yeyote atakayegusa kitu chochote alichokuwa amekalia atakuwa najisi mpaka jioni. Yeyote atakayeinua vitu hivyo ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.

11“ ‘Yeyote atakayeguswa na mtu anayetokwa na usaha bila kunawa mikono yake kwa maji, ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.

1215:12 Law 6:28; 11:32“ ‘Chungu cha udongo kitakachoguswa na mtu huyo ni lazima kivunjwe, na kifaa chochote cha mbao kitaoshwa kwa maji.

1315:13 Law 8:33; 14:8; Hes 12:14; 19:11“ ‘Wakati mtu atakapotakasika kutoka usaha wake, anapaswa kuhesabu siku saba kwa utakaso wake. Ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji safi, naye atatakasika. 1415:14 Law 14:22; Hes 6:10-14Siku ya nane, atachukua hua wawili au makinda mawili ya njiwa, aje mbele za Bwana kwenye ingilio la Hema la Kukutania, na kumpa kuhani. 1515:15 Law 5:7; 14:18-19, 31; Ebr 9:14; 10:1Kuhani atavitoa dhabihu, mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi na huyo mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Kwa njia hii atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya huyo mtu kwa sababu ya kutokwa usaha kwake.

1615:16 Kum 23:10-11; Law 22:4; 15:18; 1Sam 21:4“ ‘Wakati mtu akitokwa na shahawa, ni lazima aoge mwili mzima kwa maji, na atakuwa najisi mpaka jioni. 17Vazi lolote ama ngozi yoyote yenye shahawa juu yake ni lazima ioshwe kwa maji, na itakuwa najisi mpaka jioni. 18Ikiwa mtu atalala na mwanamke, na kukawa na kutoka kwa shahawa, ni lazima wote waoge kwa maji, nao watakuwa najisi mpaka jioni.

1915:19 Law 12:2; Eze 36:17“ ‘Ikiwa mwanamke atatokwa na damu ya kawaida ya mwezi, atakuwa najisi kwa siku saba, na yeyote atakayemgusa atakuwa najisi mpaka jioni.

20“ ‘Chochote atakacholalia wakati wake wa hedhi kitakuwa najisi, na chochote atakachokikalia kitakuwa najisi. 21Yeyote atakayegusa kitanda chake ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni. 2215:22 2Kor 7:1; Eze 36:17Yeyote atakayegusa chochote atakachokalia ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni. 23Kiwe ni kitanda ama chochote alichokuwa amekikalia, ikiwa mtu yeyote atakigusa, atakuwa najisi mpaka jioni.

2415:24 Law 12:2; 18:19; 20:18; Eze 18:6“ ‘Ikiwa mwanaume atalala naye na ile damu ya mwezi ikamgusa, atakuwa najisi kwa siku saba; kitanda chochote atakachokilalia huyo mwanaume kitakuwa najisi.

2515:25 Mt 9:20; Lk 8:43; Mk 5:25“ ‘Ikiwa mwanamke atatokwa na damu kwa siku nyingi zaidi ya siku zake za mwezi, au amekuwa na damu inayoendelea zaidi ya kipindi chake, atakuwa najisi kwa kipindi chote cha shida hiyo, kama ilivyokuwa katika siku za hedhi yake. 26Kitanda chochote atakachokilalia huyo mwanamke wakati anaendelea kutokwa na damu kitakuwa najisi, kama kilivyokuwa kitanda chake wakati wa siku zake za hedhi, na chochote atakachokalia kitakuwa najisi, kama wakati wake wa hedhi. 27Yeyote agusaye vitu hivyo atakuwa najisi; ni lazima afue nguo zake na kuoga kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.

28“ ‘Wakati atakapotakasika kutoka hedhi yake, ni lazima ahesabu siku saba, na baada ya hapo atakuwa safi kwa kawaida ya ibada. 2915:29 Law 14:22; 15:30; 5:10; 14:20, 31; 18:19; 2Sam 11:4; Mk 5:25; Lk 8:43Siku ya nane ni lazima achukue hua wawili au makinda mawili ya njiwa, na kumletea kuhani kwenye mlango wa Hema la Kukutania. 30Kuhani atatoa dhabihu, mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na huyo mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Kwa njia hii, atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana kwa sababu ya unajisi wa kutokwa damu kwake.

3115:31 Law 20:3; Hes 5:3; 19:13, 20; 2Sam 15:25; 2Fal 21:7; Za 33:14; 74:7; 76:2; Eze 5:11; 23:38“ ‘Ni lazima uwatenge Waisraeli kutokana na vitu ambavyo vinawafanya najisi, ili wasife katika unajisi wao kwa kunajisi makao yangu,15:31 Yaani maskani ya Mungu. ambayo yapo katikati yao.’ ”

32Haya ni masharti kwa ajili ya mtu mwenye kutokwa na usaha, kwa ajili ya yeyote atakayetokwa na shahawa, 33kwa ajili ya mwanamke katika siku zake za hedhi, kwa ajili ya mwanaume au mwanamke atokwaye na usaha, na kwa ajili ya mwanaume alalaye na mwanamke ambaye ni najisi kwa kawaida ya ibada.