创世记 30 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

创世记 30:1-43

1拉结见自己没有给雅各生孩子,就嫉妒姐姐。她对雅各说:“你给我孩子,不然我还不如死了!” 2雅各气愤地说:“使你不能生育的是上帝,难道我能代替上帝吗?” 3拉结说:“你去跟我的婢女辟拉同房吧,这样她可以为我生孩子,我也可以留下后代。” 4于是拉结把婢女辟拉给丈夫做妾,雅各辟拉同房。 5辟拉怀了孕,为雅各生下一个儿子。 6拉结说:“上帝为我申了冤,也听了我的恳求,赐给我一个儿子。”拉结就给孩子取名叫30:6 ”意思是“申冤”。7拉结的婢女辟拉又怀孕,为雅各生了第二个儿子。 8拉结说:“我跟姐姐相争,我得胜了。”她就给这孩子取名叫拿弗他利30:8 拿弗他利”意思是“相争”。

9利亚见自己不再生育,就把婢女悉帕雅各做妾。 10悉帕雅各生了一个儿子。 11利亚说:“真幸运!”她便给孩子取名叫迦得30:11 迦得”意思是“幸运”。12悉帕又给雅各生了第二个儿子, 13利亚说:“我真有福啊!妇女们会说我有福!”她就为孩子取名亚设30:13 亚设”意思是“有福”。

14在收麦子的季节,吕便在田间找到一些风茄,拿回家给母亲利亚拉结知道后,对利亚说:“请给我一些你儿子找到的风茄。” 15利亚说:“你抢了我丈夫还不够吗?现在还要抢我儿子的风茄吗?”拉结回答说:“你给我风茄,今夜雅各就跟你同房。” 16那天晚上,雅各从田间回来,利亚就出来迎接他说:“你要来跟我同房,因为我已经用儿子的风茄把你雇下来了。”于是,那天晚上雅各便跟利亚同房。 17上帝答应利亚的祈求,使她怀孕,为雅各生了第五个儿子。 18利亚说:“我把婢女送给丈夫做妾,现在上帝给我报酬了。”因此,她就为孩子取名叫以萨迦30:18 以萨迦”意思是“报酬”。

19后来,利亚又怀孕,给雅各生下第六个儿子。 20她说:“上帝赐给我珍贵的礼物,现在我丈夫会尊重我,因为我给他生了六个儿子。”于是,她就给这个儿子取名叫西布伦30:20 西布伦”意思是“尊重”。21后来,利亚又生了一个女儿,给她取名叫底娜

22上帝眷顾拉结,听了她的祷告,使她可以生育。 23她就怀孕,生了一个儿子,说:“上帝除去了我的羞辱。” 24她给孩子取名叫约瑟30:24 约瑟”意思是“增添”。,又说:“愿上帝再给我添一个儿子!”

雅各与拉班的协议

25拉结约瑟以后,雅各拉班说:“请让我走吧!我想回故乡, 26请你让我和妻儿一同回去吧!她们都是我替你工作得来的,你知道我怎样努力为你工作。”

27拉班却挽留他,说:“如果你肯赏光,请你留下来!因为我占卜得知上帝为了你的缘故才赐福给我。 28你要多少酬劳,只管说出来,我一定会给你。”

29雅各回答说:“你知道我怎样努力地服侍你,照顾你的牲畜。 30我来以前,你的财产很少。上帝因为我的到来而赐福给你,使你财产大增。但我自己什么时候才能兴家立业呢?”

31拉班问:“我该给你什么呢?”雅各说:“你不用给我什么,只要你答应一件事,我就继续照料你的羊群。 32今天让我从你的羊群中挑出黑色或有斑点的绵羊,以及有斑点的山羊作为我的薪酬。 33以后,如果你在给我作薪酬的羊群中发现白色的绵羊或没有斑点的山羊,就算是我偷的。这样你可以知道我是否诚实。”

34拉班说:“好,就照你的话做!” 35当天,拉班把有条纹或斑点的公山羊以及有斑点或夹杂白纹的母山羊,连同黑色的绵羊都挑出来,交给自己的儿子们看管。 36然后,他离开雅各,彼此相隔三天的路程。雅各继续为他照料其余的羊。

37雅各折下一些杨树、杏树和枫树的嫩枝,削掉部分树皮,露出白色的条纹, 38然后把这些嫩枝插在羊喝水的水槽和水沟里。羊群来喝水时互相交配。 39它们对着这些树枝交配,就生下有条纹和有斑点的羊羔。 40雅各把这些羊羔分出来,使它们与拉班的羊各在一处。他把自己的羊安置在一处,不与拉班的羊搀杂在一起。 41每当肥壮的羊交配时,雅各就把有条纹的枝子插在水沟里,使羊对着树枝交配。 42但如果交配的羊是瘦弱的,他就不插枝子。这样,瘦弱的羊归拉班,肥壮的羊归雅各43因此,雅各变得极其富有,拥有很多羊、骆驼、驴和仆婢。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 30:1-43

1Raheli alipoona hamzalii Yakobo watoto, akamwonea ndugu yake wivu. Hivyo akamwambia Yakobo, “Nipe watoto, la sivyo nitakufa!”

230:2 2Fal 5:7; Mwa 16:2Yakobo akamkasirikia, akamwambia, “Je, mimi ni badala ya Mungu, ambaye amekuzuia usizae watoto?”

330:3 Mwa 16:2Ndipo Raheli akamwambia, “Hapa yupo Bilha, mtumishi wangu wa kike. Kutana naye kimwili ili aweze kunizalia watoto na kwa kupitia yeye mimi pia niweze kuwa na uzao.”

430:4 Mwa 16:3-4Hivyo Raheli akampa Yakobo Bilha awe mke wake. Yakobo akakutana naye kimwili, 5Bilha akapata mimba, naye akamzalia Yakobo mwana. 630:6 Za 35:24; 1Sam 1:20; Yos 19:40Ndipo Raheli akasema, “Mungu amenipa haki yangu, amesikiliza maombi yangu na kunipa mwana.” Kwa sababu hiyo akamwita Dani.30:6 Dani maana yake Anahukumu, yaani Mungu amenipa haki yangu.

7Bilha mtumishi wa kike wa Raheli akapata mimba tena, akamzalia Yakobo mwana wa pili. 830:8 Hos 12:3-4; Hes 1:42Ndipo Raheli akasema, “Nilikuwa na mashindano makubwa na ndugu yangu, nami nimeshinda.” Kwa hiyo akamwita Naftali.30:8 Naftali maana yake Nimeshindana nami nimeshinda.

930:9 Mwa 29:16Lea alipoona kuwa amekoma kuzaa watoto, alimchukua mtumishi wake wa kike Zilpa, naye akampa Yakobo awe mke wake. 10Mtumishi wa Lea yaani Zilpa, akamzalia Yakobo mwana. 1130:11 Mwa 35:26; Kut 1:4Ndipo Lea akasema, “Hii ni bahati nzuri aje!” Kwa hiyo akamwita Gadi.

12Mtumishi wa kike wa Lea akamzalia Yakobo mwana wa pili. 1330:13 Lk 1:48Ndipo Lea aliposema, “Jinsi gani nilivyo na furaha! Wanawake wataniita furaha.” Kwa hiyo akamwita Asheri.30:13 Asheri maana yake Nimefurahi, yaani Mungu amenifurahisha.

1430:14 Wim 7:13Wakati wa kuvuna ngano, Reubeni akaenda shambani akakuta tunguja, ambazo alizileta kwa Lea mama yake. Raheli akamwambia Lea, “Tafadhali nakuomba unipe baadhi ya tunguja za mwanao.”

1530:15 Isa 7:13Lakini Lea akamwambia, “Haikukutosha kumtwaa mume wangu? Je, utachukua na tunguja za mwanangu pia?”

Raheli akasema, “Vema sana! Yakobo atakutana nawe kimwili leo usiku, kwa malipo ya tunguja za mwanao.”

16Kwa hiyo Yakobo alipokuja kutoka shambani jioni ile, Lea akaenda kumlaki, akamwambia, “Lazima ukutane nami kimwili. Nimekukodisha kwa tunguja za mwanangu.” Kwa hiyo akakutana naye kimwili usiku ule.

1730:17 Mwa 25:21Mungu akamsikiliza Lea, naye akapata mimba akamzalia Yakobo mwana wa tano. 1830:18 Hes 1:8, 24Ndipo Lea akasema, “Mungu amenizawadia kwa kumpa mume wangu mtumishi wangu wa kike.” Kwa hiyo akamwita Isakari.30:18 Isakari maana yake Zawadi, yaani Mungu amenizawadia.

19Lea akapata mimba tena akamzalia Yakobo mwana wa sita. 2030:20 1Pet 3:7Ndipo Lea aliposema, “Mungu amenizawadia kwa zawadi ya thamani sana. Wakati huu mume wangu ataniheshimu kwa sababu nimemzalia wana sita.” Kwa hiyo akamwita Zabuloni.30:20 Zabuloni maana yake Heshima.

2130:21 Mwa 34:1Baadaye akamzaa mtoto wa kike akamwita Dina.30:21 Dina maana yake Tetea haki, yaani Mungu amenitetea katika mashindano yangu.

2230:22 Mwa 11:30Ndipo Mungu akamkumbuka Raheli, akasikia maombi yake na akafungua tumbo lake. 2330:23 Isa 4:1; Lk 1:25Akapata mimba na akamzaa mwana na kusema, “Mungu ameniondolea aibu yangu.”

2430:24 Mwa 35:17Akamwita Yosefu30:24 Yosefu maana yake Yeye na aongeze, yaani Mungu na aniongezee. na kusema, “Bwana na anipe mwana mwingine.”

Makundi Ya Yakobo Yaongezeka

2530:25 Mwa 24:54Baada ya Raheli kumzaa Yosefu, Yakobo akamwambia Labani, “Nipe ruhusa nirudi katika nchi yangu. 26Nipe wake zangu na watoto, ambao nimetumika kuwapata, nami niende zangu. Unajua ni kazi kiasi gani ambayo nimekufanyia.”

2730:27 Mwa 26:24Lakini Labani akamwambia, “Ikiwa nimepata kibali machoni pako, tafadhali ukae. Nimegundua kwa njia ya uaguzi kwamba Bwana amenibariki kwa sababu yako.” 2830:28 Mwa 29:15Akaongeza kumwambia, “Taja ujira wako nami nitakulipa.”

29Yakobo akamwambia, “Unajua jinsi ambavyo nimekutumikia na jinsi ambavyo wanyama wako walivyolishwa vizuri chini ya uangalizi wangu. 30Kidogo ulichokuwa nacho kabla sijaja kimeongezeka sana, naye Bwana amekubariki popote nilipokuwa. Lakini sasa, ni lini nitashughulikia mambo ya nyumba yangu mwenyewe?”

31Labani akamuuliza, “Nikupe nini?”

Yakobo akamjibu, “Usinipe chochote lakini kama utanifanyia jambo hili moja, nitaendelea kuchunga na kuyaangalia makundi yako. 3230:32 Mwa 31:8, 12Niruhusu nipite katika makundi yako yote leo niondoe humo kila kondoo mwenye mabakabaka au madoadoa, kila mwana-kondoo mweusi na kila mbuzi mwenye madoadoa au mabakabaka. Hawa watakuwa ujira wangu. 33Uadilifu wangu utanishuhudia siku zijazo, kila utakapochunguza ujira ambao umenilipa mimi. Mbuzi yeyote wangu ambaye hana mabakabaka wala madoadoa, au mwana-kondoo ambaye si mweusi, atahesabika ameibwa.”

34Labani akasema, “Ninakubali na iwe kama ulivyosema.” 35Siku ile ile Yakobo akawaondoa beberu wote waliokuwa na mistari au madoadoa na mbuzi wake wote waliokuwa na mistari au madoadoa (wote waliokuwa na alama nyeupe juu yao) na wana-kondoo weusi wote, akawaweka chini ya uangalizi wa wanawe. 36Kisha Labani akamwacha Yakobo kwa mwendo wa safari ya siku tatu kati yake na Yakobo, wakati Yakobo akiendelea kuchunga lile kundi la Labani lililobaki.

3730:37 Yer 1:11Hata hivyo, Yakobo, akachukua fito mbichi zilizokatwa wakati huo huo za miti ya mlubna, mlozi na mwaramoni akazibambua ili mistari myeupe ionekane katika fito hizo. 3830:38 Kut 2:16Kisha akaweka fito alizozibambua kwenye mabirika yote ya kunyweshea mifugo, ili ziwe mbele ya makundi walipokuja kunywa maji. Wanyama walipokuja kunywa maji, hali wakiwa wanahitaji mbegu, 39wakapandwa hizo fito zikiwa mbele yao. Wanyama waliopata mimba mbele ya hizo fito walizaa wanyama wenye mistari, madoadoa na mabakabaka. 40Yakobo akawatenga wadogo wa kundi peke yao, lakini akazielekeza nyuso za hao waliobaki kwenye wale wenye mistari na weusi waliokuwa mali ya Labani. Hivyo akatenga makundi yake mwenyewe, na wala hakuwachanganya na wanyama wa Labani. 41Kila mara wanyama wenye nguvu walipohitaji mbegu, Yakobo aliweka zile fito kwenye mabirika mbele ya hao wanyama, ili wapandwe karibu na hizo fito, 42lakini ikiwa wanyama walikuwa wadhaifu hakuziweka hizo fito. Hivyo wanyama wadhaifu wakawa wa Labani, na wanyama wenye nguvu wakawa wa Yakobo. 4330:43 Mwa 12:16Kwa njia hii Yakobo akastawi sana, tena akawa na makundi makubwa, watumishi wa kike na wa kiume na ngamia na punda.