列王纪下 15 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

列王纪下 15:1-38

亚撒利雅做犹大王

1以色列耶罗波安执政第二十七年,犹大亚玛谢的儿子亚撒利雅登基。 2他十六岁登基,在耶路撒冷执政五十二年。他母亲叫耶可利雅,是耶路撒冷人。 3亚撒利雅效法他父亲亚玛谢,做耶和华视为正的事。 4然而,他没有拆除丘坛,人们仍在那里献祭烧香。 5耶和华惩罚他,使他终生患麻风病。他另住别宫,他儿子约坦摄政,掌管宫中事务,治理国家。 6亚撒利雅其他的事及其一切所作所为都记在犹大的列王史上。 7亚撒利雅与祖先同眠后,葬在大卫城他的祖坟里。他儿子约坦继位。

撒迦利雅做以色列王

8犹大亚撒利雅执政第三十八年,耶罗波安的儿子撒迦利雅撒玛利亚登基做以色列王,执政六个月。 9他做耶和华视为恶的事,重蹈祖先的覆辙,没有离开尼八的儿子耶罗波安使以色列人犯的那些罪。 10雅比的儿子沙龙谋反,当众杀了撒迦利雅,篡位做了以色列王。 11撒迦利雅其他的事都记在以色列的列王史上。 12这件事应验了从前耶和华对耶户的应许:“你的子孙必做以色列王,一直到第四代。”

沙龙做以色列王

13犹大乌西雅执政第三十九年,雅比的儿子沙龙登基,在撒玛利亚执政一个月。 14迦底的儿子米拿现得撒撒玛利亚杀了沙龙,篡位做了以色列王。 15沙龙其他的事及其谋反的经过都记在以色列的列王史上。

米拿现做以色列王

16那时,米拿现得撒起兵攻打提斐萨及其四境。因为城中的居民不肯打开城门投降,他就杀光他们,剖开所有孕妇的肚腹。 17犹大亚撒利雅执政第三十九年,迦底的儿子米拿现撒玛利亚登基做以色列王,执政十年。 18他做耶和华视为恶的事,一生没有离开尼八的儿子耶罗波安使以色列人犯的那些罪。 19亚述普勒犯境,米拿现献给他三十七吨银子,以获得他的支持并巩固自己的王权。 20这些银子是米拿现以色列的所有富户征收来的,每人五百五十克。于是亚述王从以色列境内退兵回国。 21米拿现其他的事及其一切所作所为都记在以色列的列王史上。 22米拿现与祖先同眠后,他儿子比加辖继位。

比加辖做以色列王

23犹大亚撒利雅执政第五十年,米拿现的儿子比加辖撒玛利亚登基做以色列王,执政两年。 24他做耶和华视为恶的事,没有离开尼八的儿子耶罗波安使以色列人犯的那些罪。 25比加辖的一名将军、利玛利的儿子比加谋反,率领五十名基列人在撒玛利亚王宫里刺杀了比加辖亚珥歌伯亚利耶比加篡位做了以色列王。 26比加辖其他的事及其一切所作所为都记在以色列的列王史上。

比加做以色列王

27犹大亚撒利雅执政第五十二年,利玛利的儿子比加撒玛利亚登基做以色列王,执政二十年。 28他做耶和华视为恶的事,没有离开尼八的儿子耶罗波安使以色列人犯的那些罪。

29以色列比加执政期间,亚述提革拉·毗列色来犯,夺取了以云亚伯·伯·玛迦亚挪基低斯夏琐,占领了基列加利利拿弗他利全境,把那里的居民掳往亚述30乌西雅的儿子约坦执政第二十年,以拉的儿子何细亚谋反,杀了利玛利的儿子比加,篡位做了以色列王。 31比加其他的事及其一切所作所为都记在以色列的列王史上。

约坦做犹大王

32利玛利的儿子以色列比加执政第二年,犹大乌西雅的儿子约坦登基。 33他二十五岁登基,在耶路撒冷执政十六年。他母亲叫耶路莎,是撒督的女儿。 34约坦效法他父亲乌西雅,做耶和华视为正的事, 35但没有拆毁丘坛,人们仍在那里献祭烧香。他执政期间,曾建造耶和华殿的上门。 36约坦其他的事及作为都记在犹大的列王史上。 37那时,耶和华差遣亚兰利汛利玛利的儿子比加攻打犹大38约坦与祖先同眠后,葬在大卫城他的祖坟里。他儿子亚哈斯继位。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 15:1-38

Azaria Mfalme Wa Yuda

(2 Nyakati 26)

115:1 2Fal 14:21Katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Azaria mwana wa Amazia mfalme wa Yuda alianza kutawala. 2Alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na miwili. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu. 3Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Amazia baba yake alivyofanya. 4Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.

515:5 Law 13:46; Mwa 41:40Bwana akampiga mfalme kwa ukoma mpaka siku aliyokufa, naye aliishi katika nyumba iliyotengwa peke yake. Yothamu mwana wa mfalme akawa msimamizi wa jumba la mfalme, na akawatawala watu wa nchi.

6Matukio mengine ya utawala wa Azaria na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? 715:7 Isa 6:1Azaria akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika Mji wa Daudi, na Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.

Zekaria Mfalme Wa Israeli

8Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Zekaria mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, naye akatawala miezi sita. 9Akafanya maovu machoni pa Bwana, kama baba zake walivyofanya. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.

1015:10 2Fal 12:20Shalumu mwana wa Yabeshi akafanya shauri baya dhidi ya Zekaria. Akamshambulia mbele ya watu, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme. 11Matukio mengine ya utawala wa Zekaria yameandikwa kwenye kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli. 1215:12 2Fal 10:30Kwa hiyo neno la Bwana lililonenwa kwa Yehu likatimia, kwamba, “Wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”

Shalumu Mfalme Wa Israeli

13Shalumu mwana wa Yabeshi akawa mfalme katika mwaka wa thelathini na tisa wa Uzia mfalme wa Yuda, naye akatawala katika Samaria kwa mwezi mmoja. 1415:14 1Fal 15:33; 2Fal 12:20Kisha Menahemu mwana wa Gadi akaenda kutoka Tirsa mpaka Samaria. Akamshambulia Shalumu mwana wa Yabeshi huko Samaria, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.

15Matukio mengine ya utawala wa Shalumu, na mauaji aliyoyafanya, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.

1615:16 2Fal 8:12; Hos 13:16Wakati ule, akianzia Tirsa, Menahemu alishambulia Tifsa na kila mtu ndani yake, na wale waliokuwa maeneo jirani, kwa sababu walikataa kufungua malango yao. Akaiangamiza Tifsa yote, na kuwapasua matumbo wanawake wote wenye mimba.

Menahemu Mfalme Wa Israeli

17Katika mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Menahemu mwana wa Gadi akawa mfalme wa Israeli, akatawala huko Samaria kwa miaka kumi. 18Akatenda maovu machoni pa Bwana. Katika wakati wa utawala wake wote, hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.

1915:19 1Nya 5:6, 26Kisha Pulu mfalme wa Ashuru akaishambulia Israeli. Menahemu mfalme wa Israeli akampa talanta elfu moja za fedha15:19 Talanta 1,000 za fedha ni sawa na tani 34. ili amsaidie na kumwezesha katika utawala wake. 2015:20 2Fal 12:18Menahemu akatoza fedha hizi kwa nguvu kutoka kwa Israeli. Kila mtu tajiri alilazimika kuchanga shekeli hamsini za fedha15:20 Shekeli 50 za fedha ni sawa na gramu 600. ambazo alipewa mfalme wa Ashuru. Basi mfalme wa Ashuru akajiondoa na hakuendelea kuikalia nchi.

21Matukio mengine ya utawala wa Menahemu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli? 22Menahemu akalala pamoja na baba zake. Naye Pekahia mwanawe akawa mfalme baada yake.

Pekahia Mfalme Wa Israeli

23Katika mwaka wa hamsini wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, akatawala miaka miwili. 24Pekahia akafanya uovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda. 2515:25 2Nya 28:6; Isa 7:1Mmoja wa maafisa wake wakuu, Peka mwana wa Remalia, akafanya shauri baya dhidi yake. Akachukua watu hamsini wa Gileadi pamoja naye, akamuua Pekahia, pamoja na Argobu na Aria, katika ngome ya jumba la kifalme huko Samaria. Kwa hiyo Peka akamuua Pekahia, naye akaingia mahali pake kuwa mfalme.

26Matukio mengine ya utawala wa Pekahia na yote aliyoyafanya yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.

Peka Mfalme Wa Israeli

2715:27 2Nya 28:6; Isa 7:4Katika mwaka wa hamsini na mbili wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Peka mwana wa Remalia akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala miaka ishirini. 28Akafanya maovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.

2915:29 1Nya 5:26; Yer 50:17; Isa 14:6, 17Wakati wa utawala wa Peka mfalme wa Israeli, Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alikuja na kuteka Iyoni, Abel-Beth-Maaka, Yanoa, Kedeshi na Hazori. Akateka miji ya Gileadi na Galilaya, pamoja na nchi yote ya Naftali, na kuwahamishia watu wote Ashuru. 3015:30 2Fal 17:1Kisha Hoshea mwana wa Ela akafanya shauri baya dhidi ya Peka mwana wa Remalia. Akamshambulia na kumuua, kisha akaingia mahali pake kuwa mfalme katika mwaka wa ishirini wa Yothamu mwana wa Uzia.

31Matukio mengine ya utawala wa Peka na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?

Yothamu Mfalme Wa Yuda

(2 Nyakati 27)

3215:32 1Nya 5:17Katika mwaka wa pili wa utawala wa Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli, Yothamu mwana wa Uzia mfalme wa Yuda alianza kutawala. 33Alikuwa na miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki. 3415:34 1Fal 14:8Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya. 35Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko. Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana.

36Matukio mengine ya utawala wa Yothamu na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? 3715:37 2Fal 16:5(Katika siku hizo, Bwana akaanza kuwatuma Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia dhidi ya Yuda.) 38Yothamu akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi, mji wa baba zake. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.