但以理书 5 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

但以理书 5:1-31

墙上写字

1伯沙撒王盛宴款待一千大臣,与他们一同饮酒。 2王畅饮的时候,命人将先王尼布甲尼撒耶路撒冷圣殿中掳来的金银器皿拿来,供他与大臣、王后和妃嫔用来饮酒。 3于是,他们把从耶路撒冷上帝殿中掳来的金器拿来,王与大臣、王后和妃嫔便用这些器皿饮酒。 4他们一边饮酒,一边颂赞金、银、铜、铁、木、石所造的神明。

5突然,有人手的指头出现,在灯台对面王宫的粉墙上写字。王看见那只手在写字, 6脸色骤变,惊恐万分,两腿发软,双膝颤抖。 7他大声传令,召来巫师、占星家和占卜者,对这些巴比伦的智者说:“谁能读墙上的字,把意思告诉我,他必身穿紫袍,颈戴金链,在国中位居第三。” 8王所有的智者进来后,竟无人能读懂或把意思告诉王。 9伯沙撒王愈发恐惧,脸色苍白,他的大臣都不知所措。

10太后听到王和大臣的喊声,便来到宴会厅,对王说:“愿王万岁!不要惊慌失色。 11你国中有一个人,他有圣洁神明的灵。先王在世时,曾发现他有神明一样的灼见、悟性和智慧。先王尼布甲尼撒立他为术士、巫师、占星家和占卜者的首领。 12他有非凡的心智、知识和悟性,能解梦、释谜、解惑。他叫但以理,先王给他取名叫伯提沙撒。现在可以把他召来,他必能解释这些字的意思。”

13于是,但以理被带到王面前。王问他:“你就是先王从犹大掳来的但以理吗? 14我听说你有神明的灵,有灼见、悟性和非凡的智慧。 15我召智者和巫师来读这些字,为我解释字的意思,但他们都不能解释。 16我听说你能释梦、解惑。你若能读出墙上的字,把意思告诉我,你必身穿紫袍、颈戴金链,在我的国中位居第三。”

17但以理回答说:“你的礼物自己留着,你的赏赐可以给别人,不过我会为你读这些字,解释意思。 18王啊,至高的上帝曾将国位、权力、尊荣、威严赐给你的先王尼布甲尼撒19因为他有上帝所赐的大权,各族、各邦、各语种的人都在他面前战抖,充满恐惧。他操生杀大权,可随意擢升、罢黜。 20但他变得心高气傲、刚愎自用、狂妄自大,因而被革除王位、剥去尊荣。 21他从人群中被赶走,他的心变成兽心,他与野驴同住,像牛一样吃草,被天上的露水浸湿,直到他知道至高的上帝主宰世上万国,祂要把国赐给谁就赐给谁。

22伯沙撒啊,你是他的后裔,你虽然知道这一切事,仍不谦卑, 23竟在天上的主面前自大,命人拿来祂殿里的器皿,供你和大臣、王后、妃嫔用来饮酒,并颂赞不能看、不能听、一无所知、用金、银、铜、铁、木、石所造的神明,却不尊崇赐你生命气息、掌管你一举一动的上帝。

24“因此,上帝使指头出现,写下这些字, 25就是‘弥尼,弥尼,提客勒,乌法珥新’。 26这些字的意思是这样,弥尼——指上帝已经数算你国度的年日,使之到此为止; 27提客勒——指你已经被放在秤上称了,发现分量不够; 28乌法珥新5:28 乌法珥新”亚兰文是“毗勒斯”,即“乌法珥新”的单数格式。——指你的国要分裂,归给玛代人和波斯人。”

29于是,伯沙撒下令给但以理穿上紫袍,戴上金项链,又宣告他在国中位居第三。 30当夜,迦勒底伯沙撒被杀。 31玛代大流士六十二岁时夺取了王权。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Danieli 5:1-31

Maandishi Ukutani

15:1 1Fal 3:15; Mk 6:21; Es 3:1; Yer 50:35; Dan 7:1; 8:1Mfalme Belshaza alifanya karamu kubwa kwa ajili ya maelfu ya wakuu wake na akanywa mvinyo pamoja nao. 25:2 2Nya 36:10; Yer 52:19; Es 1:7; Mit 20:1; Isa 21:5; 2Fal 24:13; Es 2:14; Dan 1:2Wakati Belshaza alipokuwa akinywa mvinyo wake, aliamuru viletwe vile vikombe vya dhahabu na fedha ambavyo Nebukadneza baba yake alikuwa amevichukua kutoka hekaluni huko Yerusalemu, ili mfalme na wakuu wake, wake zake na masuria wake waweze kuvinywea. 3Kwa hiyo wakavileta vile vikombe vya dhahabu ambavyo vilikuwa vimechukuliwa kutoka Hekalu la Mungu huko Yerusalemu, naye mfalme na wakuu wake, wake zake na masuria wake wakavinywea. 45:4 Es 1:10; Ufu 9:20; Za 115:4-8; Amu 16:24; Hag 2:19; Za 135:15-18Walipokuwa wakinywa mvinyo, wakaisifu miungu ya dhahabu na fedha, ya shaba, chuma, miti na mawe.

5Ghafula vidole vya mkono wa mwanadamu vilitokea na kuandika juu ya ukuta, karibu na kinara cha taa ndani ya jumba la mfalme. Mfalme akatazama kitanga kilivyokuwa kikiandika. 65:6 Dan 4:5; Za 22:14; Nah 2:10; Ay 4:15; Isa 7:2; Eze 7:17Uso wa mfalme ukageuka rangi, naye akaogopa sana, kiasi kwamba magoti yake yaligongana na miguu yake ikalegea.

75:7 Isa 44:25; 47:13; Dan 4:6-7; Mwa 41:42; Dan 2:5-6, 48; 6:2-3; Mwa 41:8; Isa 19:3; 44:25; Yer 50:35; Es 10:3Mfalme akawaita wasihiri, wanajimu na waganga waletwe, naye akawaambia hawa wenye hekima wa Babeli, “Yeyote asomaye maandishi haya na kuniambia maana yake atavikwa nguo za zambarau, na kuvikwa mkufu wa dhahabu shingoni mwake, naye atafanywa mtawala wa cheo cha tatu katika ufalme.”

85:8 Dan 2:10, 27; 4:18; Mwa 41:8; 41:8; Kut 8:18Ndipo watu wote wa mfalme wenye hekima wakaingia, lakini hawakuweza kusoma yale maandishi wala kumwambia mfalme maana yake. 95:9 Za 48:5; Isa 21:4Basi Mfalme Belshaza akazidi kujawa na hofu, na uso wake ukageuka rangi zaidi. Wakuu wake wakapigwa na bumbuazi.

105:10 Neh 2:3; Dan 3:9Malkia5:10 Au: Mama yake mfalme. aliposikia sauti za mfalme na wakuu wake, alikuja katika ukumbi wa karamu. Akasema, “Ee mfalme, uishi milele! Usishtuke! Usibadilike rangi kiasi hicho! 115:11 Mwa 41:38; Dan 4:8-9; 1:17; 2:47-48; 2:22; Mwa 41:38; Dan 2:22Yuko mtu katika ufalme wako ambaye ana roho ya miungu mitakatifu ndani yake. Wakati wa baba yako, mtu huyo alionekana kuwa na ufahamu, akili na hekima kama ile ya miungu. Mfalme Nebukadneza baba yako, yaani nasema mfalme baba yako, alimweka kuwa mkuu wa waganga, wasihiri, wanajimu na waaguzi. 125:12 Dan 1:7; 6:3; Hes 12:8; Eze 28:3Mtu huyu Danieli, ambaye mfalme alimwita Belteshaza, alionekana kuwa na akili nyepesi, maarifa na ufahamu, pia uwezo wa kufasiri ndoto, kueleza mafumbo na kutatua matatizo magumu. Mwite Danieli, naye atakuambia maana ya haya maandishi.”

135:13 Es 2:5-6; Dan 6:13Hivyo Danieli akaletwa mbele ya mfalme, naye mfalme akamuuliza, “Je, wewe ndiwe Danieli, mmoja wa watu wa uhamisho walioletwa na mfalme baba yangu kutoka Yuda? 14Nimesikia kwamba roho ya miungu iko ndani yako, na kwamba una ufahamu, akili na hekima ya pekee. 155:15 Dan 4:18Watu wenye hekima na wasihiri waliletwa mbele yangu ili kusoma maandishi haya na kuniambia maana yake, lakini hawakuweza kunifafanulia. 165:16 Mwa 41:15; 42; Es 5:3; Dan 2:6; Mwa 41:15, 42Basi nimesikia kwamba unaweza kutoa tafsiri na kutatua matatizo magumu. Ikiwa unaweza kusoma maandishi haya na kuniambia maana yake, utavikwa nguo za zambarau na mkufu wa dhahabu shingoni mwako, nawe utafanywa mtawala wa tatu katika ufalme.”

175:17 2Fal 5:16Ndipo Danieli akamjibu mfalme, “Waweza kubaki na zawadi zako mwenyewe na kumpa mtu mwingine zawadi zako. Hata hivyo, nitasoma maandishi kwa mfalme na kumwambia maana yake.

185:18 Yer 27:7; Dan 4:36; Yer 28:14; Dan 2:37-38“Ee mfalme, Mungu Aliye Juu Sana alimpa baba yako Nebukadneza utawala, ukuu, utukufu na fahari. 195:19 Dan 2:12-13; 3:6; Yer 25:9; Dan 4:22Kwa sababu ya nafasi ya juu aliyompa baba yako, kabila zote za watu, mataifa na watu wa kila lugha walimhofu na kumwogopa. Wale ambao mfalme alitaka kuwaua, aliwaua; wale aliotaka kuwaacha hai, aliwaacha hai; wale aliotaka kuwapandisha cheo, aliwapandisha; aliotaka kuwashusha, aliwashusha. 205:20 Dan 4:30; Yer 13:18; Ay 40:12; Eze 31:10-11; Isa 14:12; Yer 43:10; Dan 8:8Lakini moyo wake ulipokuwa na majivuno na kuwa mgumu kwa kiburi, aliondolewa kutoka kwa kiti chake cha ufalme na kuvuliwa utukufu wake. 215:21 Eze 17:24; Kut 9:14-16; Dan 4:16-17Akafukuzwa mbali na wanadamu na kupewa akili ya mnyama, akaishi pamoja na punda-mwitu, akala majani kama ngʼombe, nao mwili wake ukaloweshwa kwa umande wa mbingu, mpaka alipotambua kwamba Mungu Aliye Juu Sana ndiye mtawala juu ya falme za wanadamu na kwamba humtawaza juu yao yeyote amtakaye.

225:22 Kut 10:3; 2Nya 33:23“Lakini wewe mwanawe, ee Belshaza, hukujinyenyekeza, ingawa ulifahamu haya yote. 235:23 Ufu 13:6; Isa 14:13; Hes 2:19; Yer 50:29; Ufu 9:20; Ay 12:10; Mdo 17:28; Yer 44:9; Ay 31:4; Za 115:4-8; Hab 2:19; Isa 13:11; Yer 10:23; 48:26Badala yake, umejiinua dhidi ya Bwana wa mbingu. Uliletewa vikombe vya Hekalu lake, nawe na wakuu wako, wake zako na masuria wako mlivitumia kwa kunywea mvinyo. Ukaisifu miungu ya fedha na dhahabu, ya shaba, chuma, miti na mawe, miungu ambayo haiwezi kuona, au kusikia wala kufahamu. Lakini hukumheshimu Mungu ambaye anaushikilia uhai wako na njia zako zote mkononi mwake. 24Kwa hiyo ameutuma mkono ule ulioandika maneno.

25“Haya ndiyo maneno yaliyoandikwa:

mene, mene, tekeli na peresi

265:26 Yer 27:7; Isa 13:9“Hii ndiyo maana ya maneno haya:

Mene: Mungu amezihesabu siku za utawala wako na kuukomesha.

275:27 Za 62:9; Yer 6:30; Ay 6:2Tekeli: Wewe umepimwa katika mizani na umeonekana umepungua.

285:28 Isa 13:17; Yer 50:41-43; Dan 6:28; Yer 7:27Peresi: Ufalme wako umegawanywa na kupewa Wamedi na Waajemi.”

295:29 Mwa 41:42; Dan 2:6Ndipo kwa amri ya Belshaza, Danieli akavikwa nguo za zambarau na mkufu wa dhahabu shingoni, tena akatangazwa kuwa mtawala wa tatu katika ufalme.

305:30 Isa 21:9; Yer 51:31; 50:35Usiku ule ule, Belshaza mfalme wa Wakaldayo akauawa, 315:31 Yer 50:41; Dan 11:1; Isa 13:3naye Dario Mmedi akashika ufalme akiwa na miaka sitini na miwili.