以赛亚书 63 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

以赛亚书 63:1-19

主报应列国

1这位身披红衣、

穿着华丽、充满力量、

以东波斯拉阔步而来的是谁呢?

“是宣告公义、

有拯救大能的我。”

2你的衣服为何是红色的,

好像榨酒池中踩踏葡萄者的衣服?

3“我独自在榨酒池踩踏,

万民中无人跟我在一起。

我在愤怒中踩踏他们,

在烈怒中践踏他们;

他们的血溅到我的衣服上,

染红了我的衣服。

4我心中定了报仇的日子,

我救赎我子民之年已经来临。

5我环顾四周,惊讶地看见无人帮助,无人扶持。

于是,在烈怒的推动下,

我用臂膀独自拯救。

6我在愤怒中践踏万民,

让他们饱尝我的烈怒,

把他们的血倒在地上。”

颂赞与祷告

7因耶和华为我们所做的一切,

我要述说祂的慈爱和祂可歌可颂的作为,

述说祂本着怜悯和大爱赐给以色列人的厚恩。

8祂说:“他们的确是我的子民,

不会背叛我。”

因此,祂做他们的救主。

9祂苦他们所苦,

亲自63:9 亲自”希伯来文是“祂面前的天使”。拯救他们。

祂本着慈爱和怜悯救赎了他们,

自古以来一直扶持、照顾他们。

10他们却叛逆,使祂的圣灵忧伤。

于是,祂与他们为敌,

亲自攻击他们。

11后来,他们想起古时候,

想起了摩西和他的百姓,便问,

带领百姓及其牧者摩西从海里出来的那位在哪里?

将自己的圣灵降在他们中间的那位在哪里?

12用荣耀的臂膀扶持摩西

在他们面前把海水分开,

使自己威名永存的那位在哪里?

13带领他们经过大海,

犹如马行平川不会失脚的那位在哪里?

14耶和华的灵使他们得到安歇,

犹如牲畜下到山谷。

耶和华啊,你就是这样引领你的子民,

以树立自己荣耀的名。

15求你从天上垂顾,

从你圣洁、荣耀的居所垂看。

你的热忱和大能在哪里呢?

难道你不再眷爱、怜悯我们吗?

16虽然亚伯拉罕不认识我们,

以色列不承认我们,

但你是我们的父亲。

耶和华啊,你是我们的父亲,

你自古以来就是我们的救赎主。

17耶和华啊!你为何使我们偏离你的路,

使我们硬着心不敬畏你呢?

求你为了你的仆人,

你的产业——以色列各支派而改变心意!

18你的圣民曾短暂地拥有你的圣所,

如今它已被我们的敌人踏平。

19我们如此沦落,

好像从未被你治理过,

从来不属于你。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 63:1-19

Siku Ya Mungu Ya Kisasi Na Ukombozi

163:1 Mwa 36:33; Amo 1:12; Yer 42:11; Sef 3:17; 2Nya 28:17; Isa 11:14; Ufu 19:13; Ay 9:4Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu,

kutoka Bosra, mwenye mavazi yaliyotiwa madoa mekundu?

Ni nani huyu, aliyevikwa joho la kifahari,

anayetembea kwa ukuu wa nguvu zake?

“Mimi ndimi, nisemaye katika haki,

mwenye nguvu wa kuokoa.”

263:2 Ufu 19:13; Mwa 49:11Kwa nini mavazi yako ni mekundu,

kama ya yule akanyagaye shinikizo la zabibu?

363:3 Amu 6:11; Ufu 19:15; Mao 1:15; Ufu 19:13; 14:19-20; Za 108:13“Nimekanyaga shinikizo la zabibu peke yangu;

kutoka mataifa hakuna mtu aliyekuwa pamoja nami.

Nimewaponda kwa miguu katika hasira yangu

na kuwakanyaga chini katika ghadhabu yangu;

damu yao ilitia matone kwenye mavazi yangu,

na kutia madoa nguo zangu zote.

463:4 Isa 1:24; Yer 50:15Kwa kuwa siku ya kisasi ilikuwa moyoni mwangu,

mwaka wa ukombozi wangu umefika.

563:5 2Fal 14:26; Isa 41:28; 59:16; Za 44:3; Yn 16:32; Isa 33:2Nilitazama, lakini hakuwepo yeyote wa kunisaidia,

nilishangaa kwa kuwa hakuwepo yeyote aliyetoa msaada;

hivyo mkono wangu wenyewe ndio ulionifanyia wokovu,

na ghadhabu yangu mwenyewe ndiyo iliyonitegemeza.

663:6 Isa 29:9; Mao 4:21; Isa 34:3; Ay 40:12Nilikanyaga mataifa kwa miguu katika hasira yangu,

katika ghadhabu yangu niliwalewesha,

na kumwaga damu yao juu ya ardhi.”

Kusifu Na Kuomba

763:7 Isa 54:8; Efe 2:4; Kut 18:9Nitasimulia juu ya wema wa Bwana,

kwa matendo ambayo apaswa kusifiwa,

sawasawa na yote ambayo Bwana

ametenda kwa ajili yetu:

naam, mambo mengi mema aliyoyatenda

kwa ajili ya nyumba ya Israeli,

sawasawa na huruma zake

na wema wake mwingi.

863:8 Mdo 9:4; Kut 14:19; 33:14; Kum 7:7-8; Ezr 9:9; Za 28:9; Ay 37:23Alisema, “Hakika wao ni watu wangu,

wana ambao hawatanidanganya”;

hivyo akawa Mwokozi wao.

963:9 Kut 14:19; 33:14; Kum 7:7-8; Ezr 9:9; Isa 48:20; Kum 1:31; 32:7; Za 28:9; Ay 37:23Katika taabu zao zote naye alitaabika,

na malaika wa uso wake akawaokoa.

Katika upendo wake na rehema zake aliwakomboa,

akawainua na kuwachukua siku zote zilizopita.

1063:10 Eze 20:8; Mdo 7:39-42; Efe 4:30; Za 106:40; 78:17; Isa 10:4; Yos 10:14Lakini waliasi,

na kumhuzunisha Roho Mtakatifu wake.

Hivyo aligeuka na kuwa adui yao,

na yeye mwenyewe akapigana dhidi yao.

1163:11 Kut 14:22, 30; Hes 11:17; Za 77:20Ndipo watu wake wakazikumbuka siku zilizopita,

siku za Mose na watu wake:

yuko wapi yeye aliyewaleta kupitia katikati ya bahari,

pamoja na wachungaji wa kundi lake?

Yuko wapi yule aliyeweka

Roho wake Mtakatifu katikati yao,

1263:12 Kut 14:21-22; Isa 11:15; Mwa 49:24aliyetuma mkono wake uliotukuka wenye nguvu

kuwa katika mkono wa kuume wa Mose,

aliyegawa maji ya bahari mbele yao,

ili kujipatia jina milele,

1363:13 Kum 32:12; Yer 31:9; Kut 14:24; Za 119:11aliyewaongoza kupitia kwenye vilindi?

Kama farasi katika nchi iliyo wazi,

wao hawakujikwaa,

1463:14 Kut 33:14; Kum 12:9kama ngʼombe washukao bondeni kwenye malisho,

walipewa pumziko na Roho wa Bwana.

Hivi ndivyo ulivyowaongoza watu wako

ili kujipatia mwenyewe jina tukufu.

1563:15 Za 80:14; Mao 3:50; 1Fal 22:19; 2:26; Hos 11:8; Kum 26:15; Isa 64:12Tazama chini kutoka mbinguni ukaone

kutoka kiti chako cha enzi

kilichoinuliwa juu, kitakatifu na kitukufu.

Uko wapi wivu wako na uweza wako?

Umetuzuilia wema wako na huruma zako.

1663:16 Ay 14:21; Gal 3:28; Isa 44:6; Kut 4:22; Yer 3:4; Yn 8:41; Isa 59:20Lakini wewe ni Baba yetu,

ingawa Abrahamu hatufahamu sisi

wala Israeli hatutambui;

wewe, Ee Bwana, ndiwe Baba yetu,

Mkombozi wetu tangu zamani za kale ndilo jina lako.

1763:17 Isa 6:10; 29:13; Hes 10:36; Mt 13:15; Mwa 20:13; Mao 3:9; Kut 4:21; 34:9Ee Bwana, kwa nini unatuacha twende mbali na njia zako,

na kuifanya mioyo yetu migumu hata hatukukuheshimu?

Rudi kwa ajili ya watumishi wako,

yale makabila ambayo ni urithi wako.

1863:18 Law 26:31; Dan 8:24; Za 74:3-8; Kum 4:26; Isa 28:18; Lk 21:24; Dan 8:13Kwa maana kwa muda mfupi watu wako walimiliki mahali pako patakatifu,

lakini sasa adui zetu wamepakanyaga mahali patakatifu pako.

1963:19 Isa 43:7; Yer 14:9Sisi tumekuwa kama wale ambao hujawatawala kamwe,

kama wale ambao hawajaitwa kwa jina lako.