Песнь 69
(Заб. 39:14-18)
1Дирижёру хора. Песнь Давуда. В напоминание.
2Всевышний, скорее избавь меня!
Поспеши мне на помощь, Вечный!
3Пусть все, кто желает моей смерти,
будут пристыжены и посрамлены.
Пусть все, кто хочет моей погибели,
в бесчестии повернут назад.
4Пусть возвратятся со стыдом
говорящие мне: «Ага! Ага!»
5Пусть ликуют и радуются о Тебе
все ищущие Тебя,
Пусть те, кто любит Тебя за Твоё спасение,
всегда говорят: «Велик Всевышний!»
6Я же беден и нищ.
Поспеши ко мне, Всевышний!
Ты – помощь моя и мой избавитель;
Вечный, не замедли!
Zaburi 69
Kilio Cha Kuomba Msaada Wakati Wa Dhiki
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi.” Zaburi ya Daudi.
169:1 Za 42:7; 32:6; Yon 2:5Ee Mungu, niokoe,
kwa maana maji yamenifika shingoni.
269:2 Ay 30:19Ninazama kwenye vilindi vya matope,
pasipo mahali pa kukanyaga,
Nimefika kwenye maji makuu,
mafuriko yamenigharikisha.
369:3 Za 6:6; 119:82Nimechoka kwa kuomba msaada,
koo langu limekauka.
Macho yangu yanafifia,
nikimtafuta Mungu wangu.
469:4 Yn 15:25; Za 25:19; 35:19; 38:19; 40:14; 119:95; Isa 32:7Wale wanaonichukia bila sababu
ni wengi kuliko nywele za kichwa changu;
wengi ni adui kwangu bila sababu,
wale wanaotafuta kuniangamiza.
Ninalazimishwa kurudisha
kitu ambacho sikuiba.
569:5 Za 38:5; 44:21Ee Mungu, wewe unajua upumbavu wangu,
wala hatia yangu haikufichika kwako.
6Ee Bwana, ewe Bwana Mwenye Nguvu Zote,
wakutumainio wasiaibishwe
kwa ajili yangu;
wakutafutao wasifedheheshwe kwa ajili yangu,
Ee Mungu wa Israeli.
769:7 Yer 15:15; Za 39:8; 44:15Kwa maana nimestahimili dharau kwa ajili yako,
aibu imefunika uso wangu.
869:8 Ay 19:13-15; Za 31:11; 38:11; Isa 53:3; Yn 7:5Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu,
mgeni kwa wana wa mama yangu mwenyewe.
969:9 Yn 2:17; Rum 15:3; Za 89:50-51Kwa kuwa wivu wa nyumba yako unanila,
matukano ya wale wanaokutukana yameniangukia.
1069:10 Za 35:13Ninapolia na kufunga,
lazima nivumilie matusi.
1169:11 2Sam 3:31; Za 35:13Ninapovaa nguo ya gunia,
watu hunidharau.
1269:12 Mwa 18:1; 23:10; Ay 30:9Wale wanaoketi mlangoni wananisimanga,
nimekuwa wimbo wa walevi.
1369:13 Isa 49:8; 2Kor 6:2; Za 17:7; 51:1Lakini Ee Bwana, ninakuomba,
kwa wakati ukupendezao;
katika upendo wako mkuu, Ee Mungu,
unijibu kwa wokovu wako wa hakika.
1469:14 Za 69:2; 144:7Uniokoe katika matope,
usiniache nizame;
niokoe na hao wanichukiao,
kutoka kwenye vilindi vya maji.
1569:15 Za 36:6; 68:22; Hes 21:33; Yer 22:2069:15 Za 28:1; 124:4, 5; Hes 16:33Usiache mafuriko yanigharikishe
au vilindi vinimeze,
au shimo lifumbe kinywa chake juu yangu.
1669:16 Za 63:3Ee Bwana, unijibu, kwa wema wa upendo wako;
kwa huruma zako nyingi unigeukie.
1769:17 Za 22:24; 143:7; 50:15; 66:14Usimfiche mtumishi wako uso wako,
uharakishe kunijibu, kwa sababu niko katika shida.
1869:18 Za 49:15Njoo karibu uniokoe,
nikomboe kwa sababu ya adui zangu.
1969:19 Za 22:6Unajua jinsi ninavyodharauliwa,
kufedheheshwa na kuaibishwa,
adui zangu wote unawajua.
2069:20 Ay 16:2; Isa 63:5; Za 142:4Dharau zimenivunja moyo
na nimekata tamaa,
nimetafuta wa kunihurumia, lakini sikumpata,
wa kunituliza, lakini sikumpata.
2169:21 Hes 6:3; Lk 23:36; Mt 27:34, 48; Mk 15:23, 36; Yn 19:28-30Waliweka nyongo katika chakula changu
na walinipa siki nilipokuwa na kiu.
2269:22 1Sam 28:9; Ay 18:10Meza iliyoandaliwa mbele yao na iwe mtego,
nayo iwe upatilizo na tanzi.
2369:23 Rum 11:9-10Macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona,
nayo migongo yao iinamishwe daima.
2469:24 Za 79:6; Yer 10:25Uwamwagie ghadhabu yako,
hasira yako kali na iwapate.
2569:25 Law 26:43; Mt 23:38; Mdo 1:20Mahali pao na pawe ukiwa,
wala asiwepo yeyote atakayeishi katika mahema yao.
2669:26 Ay 19:22; Zek 1:15Kwa kuwa wanawatesa wale uliowajeruhi,
na kuzungumza juu ya maumivu ya wale uliowaumiza.
2769:27 Neh 4:5; Za 109:14Walipize uovu juu ya uovu,
usiwaache washiriki katika wokovu wako.
2869:28 Kut 32:32-33; Lk 10:20; Eze 13:9Wafutwe kutoka kitabu cha uzima
na wasiorodheshwe pamoja na wenye haki.
2969:29 Za 20:1Mimi niko katika maumivu na dhiki;
Ee Mungu, wokovu wako na unihifadhi.
3069:30 Za 28:7; 34:3Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo,
nami nitamtukuza kwa kumtolea shukrani.
3169:31 Za 50:9-13; 51:16Hili litampendeza Bwana kuliko ngʼombe dume,
zaidi ya fahali akiwa na pembe na kwato zake.
3269:32 Za 34:2; 22:26Maskini wataona na kufurahi:
ninyi mnaomtafuta Mungu, mioyo yenu na iishi!
3369:33 Za 12:5Bwana huwasikia wahitaji
wala hadharau watu wake waliotekwa.
3469:34 Za 96:11; 98:7; Isa 44:23Mbingu na dunia zimsifu,
bahari na vyote viendavyo ndani yake,
3569:35 Oba 1:17; Ezr 9:9; Za 51:18kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni
na kuijenga tena miji ya Yuda.
Kisha watu watafanya makao yao humo na kuimiliki,
3669:36 Za 25:13; 37:29watoto wa watumishi wake watairithi
na wale wote walipendao jina lake
wataishi humo.